nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
BARAZA Kuu la Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT), limewaonya baadhi ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambao wameanza kujipanga na kuweka mikakati binafsi ya kuwania nafasi ya urais 2015 kwa kuwa jambo hilo ni hatari kwa chama.
Mbali na hilo, pia UWT imeonya tabia ya baadhi ya viongozi wa chama na serikali kukemeana hadharani na kwenye majukwaa kwa kutafuta umaarufu wa kisiasa badala ya kutumia vikao sahihi vya chama.
Hayo yanatokana na maazimio ya kikao cha Baraza Kuu ambalo lilikutana Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo lilijadili mambo mbalimbali likiwemo la kutathimini changamoto zilizokikabili chama katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwishoni mwa mwaka jana.
Hivi katibuni, Umoja wa Vijana wa CCM ulifanya kikao cha Baraza Kuu mkoani Dodoma na kutoa maazimio mbalimbali, likiwamo la kuwakemea na kuwatisha wanachama wa CCM wanaokikosoa hadharani badala ya kwenye vikao, na kuweka bayana kuwa chama kisiwateue kuwania nyadhifa mbalimbali baadaye.
Akizungumza na Majira, Katibu Mkuu wa UWT, Bi. Amina Makilagi alisema mbali na kukemea tabia hiyo, pia jumuiya hiyo imewataka wanachama wote wa CCM kurejea utamaduni wa kujitolea kwa moyo ndani ya chama na kuachana na tabia iliyojengeka miongoni mwa wanachama wake ya kudai malipo wakati wa shughuli za kujenga chama.
Pia UWT iliazimia suala la kuimarisha uhai wake na wa CCM kwa ujumla ambapo iliwahimiza wanachama kuendelea kuimarisha uhai wa jumuiya na chama kwa kuingiza wanachama wapya na kulipa ada kwa mujibu wa katiba na pia iliazimia kuandaa mpango utakaowajengea wanawake uwezo wa kuchangia maoni katika mabadiliko ya katiba ya nchi yanayotarajiwa kufanyika.
"Mbali na hayo, UWT na chama ni lazima viendelee kujiimarisha kiuchumi kwa kuboresha rasilimali na miradi yake ili kuondokana na tabia ya utegemezi...na katika kujiimarisha zaidi UWT itaweka utaratibu maalumu wenye msingi thabiti wa kuajiri kulingana na mahitaji ya soko la sasa la ajira na kwa kuzingatia maendeleo ya sayansi na teknolojia," alisema Bi. Makilagi.
Katika suala la kulinda amani na utulivu, baraza hilo lilivitaka vyama vya siasa kuepuka kutumia vibaya fursa na haki za sheria ya vyama vya siasa kufanya maandamano na kuendesha mikutano kwa nia ya kueneza siasa za uchochezi na chuki miongoni mwa wananchi kwa lengo la kuwahamasisha wananchi kuichukia serikali yao.
"Kwa upande wa wanawake, baraza liliwataka kuepukana na siasa za uchochezi zinazoenezwa na CHADEMA kwani zinawagawa wananchi kisiasa na kiitikadi badala yake wajizatiti kufanya kazi za kujiletea maendeleo," alisema Bi. Makilagi.
Akizungumzia ilani ya CCM, aliitaka serikali kuendelea kuboresha sekondari za kata kwa kuwa zimepanua fursa ya kupata elimu kwa watoto wengi wa kike na pia kupunguza kwa kiwango kikubwa tatizo la mimba za utotoni.
Wakati akifungua kikao cha baraza hilo Mwenyekiti wa UWT, Bi. Sophia Simba aliwataka wanawake kuvunja ukimya kwa kujibu mapigo yanayoelekezwa kwa CCM na vyama vya upinzani kwa kuwa siasa zimebadilika kwa kiasi kikubwa.
Mbali na hilo, pia UWT imeonya tabia ya baadhi ya viongozi wa chama na serikali kukemeana hadharani na kwenye majukwaa kwa kutafuta umaarufu wa kisiasa badala ya kutumia vikao sahihi vya chama.
Hayo yanatokana na maazimio ya kikao cha Baraza Kuu ambalo lilikutana Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo lilijadili mambo mbalimbali likiwemo la kutathimini changamoto zilizokikabili chama katika uchaguzi mkuu uliofanyika mwishoni mwa mwaka jana.
Hivi katibuni, Umoja wa Vijana wa CCM ulifanya kikao cha Baraza Kuu mkoani Dodoma na kutoa maazimio mbalimbali, likiwamo la kuwakemea na kuwatisha wanachama wa CCM wanaokikosoa hadharani badala ya kwenye vikao, na kuweka bayana kuwa chama kisiwateue kuwania nyadhifa mbalimbali baadaye.
Akizungumza na Majira, Katibu Mkuu wa UWT, Bi. Amina Makilagi alisema mbali na kukemea tabia hiyo, pia jumuiya hiyo imewataka wanachama wote wa CCM kurejea utamaduni wa kujitolea kwa moyo ndani ya chama na kuachana na tabia iliyojengeka miongoni mwa wanachama wake ya kudai malipo wakati wa shughuli za kujenga chama.
Pia UWT iliazimia suala la kuimarisha uhai wake na wa CCM kwa ujumla ambapo iliwahimiza wanachama kuendelea kuimarisha uhai wa jumuiya na chama kwa kuingiza wanachama wapya na kulipa ada kwa mujibu wa katiba na pia iliazimia kuandaa mpango utakaowajengea wanawake uwezo wa kuchangia maoni katika mabadiliko ya katiba ya nchi yanayotarajiwa kufanyika.
"Mbali na hayo, UWT na chama ni lazima viendelee kujiimarisha kiuchumi kwa kuboresha rasilimali na miradi yake ili kuondokana na tabia ya utegemezi...na katika kujiimarisha zaidi UWT itaweka utaratibu maalumu wenye msingi thabiti wa kuajiri kulingana na mahitaji ya soko la sasa la ajira na kwa kuzingatia maendeleo ya sayansi na teknolojia," alisema Bi. Makilagi.
Katika suala la kulinda amani na utulivu, baraza hilo lilivitaka vyama vya siasa kuepuka kutumia vibaya fursa na haki za sheria ya vyama vya siasa kufanya maandamano na kuendesha mikutano kwa nia ya kueneza siasa za uchochezi na chuki miongoni mwa wananchi kwa lengo la kuwahamasisha wananchi kuichukia serikali yao.
"Kwa upande wa wanawake, baraza liliwataka kuepukana na siasa za uchochezi zinazoenezwa na CHADEMA kwani zinawagawa wananchi kisiasa na kiitikadi badala yake wajizatiti kufanya kazi za kujiletea maendeleo," alisema Bi. Makilagi.
Akizungumzia ilani ya CCM, aliitaka serikali kuendelea kuboresha sekondari za kata kwa kuwa zimepanua fursa ya kupata elimu kwa watoto wengi wa kike na pia kupunguza kwa kiwango kikubwa tatizo la mimba za utotoni.
Wakati akifungua kikao cha baraza hilo Mwenyekiti wa UWT, Bi. Sophia Simba aliwataka wanawake kuvunja ukimya kwa kujibu mapigo yanayoelekezwa kwa CCM na vyama vya upinzani kwa kuwa siasa zimebadilika kwa kiasi kikubwa.