UWT na BAWACHA sasa kupata uhai

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Mabaraza haya ya Wanawake ya CCM na CHADEMA,kwa mujibu wa Rasimu ya Katiba mpya, sasa yamepewa uhai mpya. Yatatakiwa kulea,kukuza na kuimarisha viongozi watarajiwa wa nchi hii. Mabaraza haya yatatutolea mgombea mmoja kwa kila jimbo la Uchaguzi wa Wabunge (Majimbo yote yakiwa 35) Tanzania Bara na Zanzibar. Ni wakati muafaka sasa kwa UWT na BAWACHA kuanza kazi ya kutukuka. Kazi rasmi za kisiasa kutuandalia viongozi. Na kazi ianze sasa! Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Mabaraza haya ya Wanawake ya CCM na CHADEMA,kwa mujibu wa Rasimu ya Katiba mpya, sasa yamepewa uhai mpya. Yatatakiwa kulea,kukuza na kuimarisha viongozi watarajiwa wa nchi hii. Mabaraza haya yatatutolea mgombea mmoja kwa kila jimbo la Uchaguzi wa Wabunge (Majimbo yote yakiwa 35) Tanzania Bara na Zanzibar. Ni wakati muafaka sasa kwa UWT na BAWACHA kuanza kazi ya kutukuka. Kazi rasmi za kisiasa kutuandalia viongozi. Na kazi ianze sasa! Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Mkuu mimi napingana kabisa na hili wazo la kuwa na wabunge waili kila jimbo, hakuna logic yoyote. UWT na BAWACHA watuletee wabunge/viongozi ambao ni vichwa sio kwa kivuli cha jinsia. Wameondoa viti maaulum lakini wamerudisha kwa mlango wa nyuma eti lazima kuwe na mbunge Me na KE. Haina maana kabisa. Tuseme hapana kwa wabunge wawili.
 
Wakuu nisaidieni nielewe hapa,

Hivi huu ndio mwisho wa wabunge wa majimboni ?

Huu ndio mwisho wa majimbo Tanzania Bara na Zanzibar ?

MSAADA TAFADHALI
 
Wewe ndio unatakiwa uheshimu watu wenye jinsia tofauti na yako, anti Vu ni mtu kama wewe na kuwa shoga ni maumbile yake.
Kuwa shoga ni hiari kabisa na wala siyo maumbile. Acha kutetea ubaradhuli.


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Utakuwa ni yule anti Vu? yule shoga mzee wa karibu na ofisi za chama?
Si mimi Mkuu. Nakuheshimu sana na nayaheshimu mawazo yako.Lakini,kuwa makini katika kuchangia kwako mwanangu Nduka. Kwanini usijadili mada na kuleta masuala ya ajabuajabu. Si vyema Mkuu.
 
Last edited by a moderator:
This is a very good boost for CHADEMA!

Hakuna kitu hapo, Hiyo ni Janja ya Chama cha mapinduzi baada ya kuona kinakoelekea kitakosa kabisa uwakilishi kinakuja na njia Mbadala. Hili si ndio kama lile la kumpata muongoza mjengo? Eti genda.
Angalia Taifa kama USA na mataifa mengene ya Magharibi yanayosema kuwe na Me na Ke bungeni, Wao wamebalance vipi?. USA Ina kama 16% ya Ke bungeni sisi tunalazimishwa. Wao hawana viti maalumu wala upendeleo, Kupigania kura majimboni mwendo mmoja kwa nini nasi watu wasitafute kura badala ya kusubiri wapewe????????????????
Hizo gharama za kuongeza hao wabumbe wa Pili kwa kila jimbo ni bora zikaajiri walimu nchini kuliko kusubiri msaada wa Jamaica.
 
Wabunge wa vyama wanatokana na vyama vyao sio jumuia au baraza la chama. Haya mabaraza ni kwa siasa za ndani. Nadhani wabunge wote wanapigiwa kura na wanachi wote tusipokuwa waangalifu kuruhusu hilo italeta usumbufu kwenye kupiga kura itabidi watu wakaguliwe nanii ili kujua jinsia yao.
 
huu mfumo wa lazima mwanamke jimboni sidhani kama ni mzuri .Japo pia kuwafanya wabunge wa nafasi maalum ni kuwalemaza.Wanawake wasibebwe kwa jinsi yoyote ile ,ili kuweka balance ya uwakilishi.
 
Back
Top Bottom