Jamani mi siku hizi nashangaa sana, hivi kumbe kazi ni ishu kiasi hiki? Yaani hakuna uhusiano wa nafasi za kazi na watu wanaotakiwa kufanyiwa usaili. Mfano PSPF walitoa nafasi 8 za nafasi ya Operation Officer, leo nimeona wameita watu 1422 kwa ajili ya usaili, pia walitoa nafasi 7 za madereva, na wameita watu 185 kwa ajili ya usaili. Jamani hata kama ajira ndio ishu hivi kuna uhusiano wa nafasi na watu wanaoitwa kwenye usaili? Hata kama kuna Written, Oral, Practical yote hayo ya nini? Hivi hakuna sheria inayosimamia idadi maalumu ya watu wa kuwafanyia usaili kulingana na nafasi zilizopo? Mi nilikuwa nadhani ingekuwa 1:3 au hata 1:5 siyo mbaya, au ma - great thinker mnaonaje?