Uwezo wa watu kufikiri na kutenda; Je, huwa unaendana na nchi aliyopo?

Plsm

Senior Member
Aug 19, 2021
177
266
Je, Uwezo wa mtu kufikiri na kutenda, unaendana na nchi aliyopo?

Kuna mambo ukiyatafakari saana, unaweza kuona kwamba, uhusiano kati ya mtu uwezo wake wa kufikiri na kutenda kunatokana na nchi aliyopo,kuna nchi zina watu wasomi, ambapo mambo yao huendeshwa kitaalamu na kiuweledi wa kutosha, lakini zipo nchi ambazo nazo zinawasomi wa level ileile, lakini kwa jinsi zinavyoendesha mambo yake utadhani hao waliosoma, ni sawa na jamii ya wasiosoma tu na kwamba hawana msaada, msaada wao ni kudhibiti kila anayehoji uwezo wao wa taaluma zao! hii ni mbaya sana

Changamoto nyingine ni kwamba, Zipo nchi ambazo zinajivunia mabadiriko makubwa yanayotokana na matunda ya watu wake kwa kazi nzuri wafanyazo wasomi wake na kunufaisha zaidi watu woke, tofauti kabisa na ilivyo kwa baadhi ya nchi ambazo wasomi wake hawana msaada kabisa kwa watu wao, kazi yao na sifa yao kubwa, hujivunia kwa kujiongezea mishahara tena nyongeza hiyo ya mishahara, haitokani wa weledi na matunda bora ya kazi zao maofisini, ni kuwachangisha tu wananchi na kisha wao kujiongezea mishahara na kupangiana safari mbalimbali nje ya nchi zao na kujlipa posho kubwa kubwa, wakati huohuo nchi utakuta inautajiri mkubwa wa rasilimali asili, Cha kushangaza zaidi, hata wale ambao hawana elimu kubwa kwenye nchi hizo zenye msaada wa wasomi wake, uelewa wao katika mambo mbalimbali juu ya kinachoendelea katika nchi zao, unaweza kudhani elimu zao ndogo, ndiyo uwezo wa watu wenye elimu kubwa kwenye taifa lingine.

Nchi, za watu kama hao, kila jambo hupimwa kwa kutumia vigezo vya leo na miaka mingi ijayo, ikilinganishwa na baadhi ya nchi zenye watu wenye uwezo mdogo wa kufikiri na kutenda, ambapo watu wake hupima mambo yake kwa kutumia vigezo vya leo na kesho tu! elimu ya namna hii hauwezi ukasema imemkomboa mwananchi na kiongozi huyo

katika nchi watu wake ambapo fikra zao na utendaji kazi ulio chini mno, raia wake ni kama kuku broiler, mchinjanji huchukua kuku mmoja baada ya mwingine na hakuna anayepiga kelele, wote ni kimya wakiwa wamepanga foleni zamu kwa zamu

Nchi kama hizo, maendeleo kwao ni magumu saana na hata yakipatikana ni ya maumivu makubwa kwa makundi makubwa ya watu, huku kundi dogo likibadirisha vitu vya anasa kila uchwao na kundi hili kuishi kama liko peponi

Shida zinazotukabiri hasa katika nchi zetu hizi ni uhasama mkubwa uliomo katika vyama na katika suala zima la siasa!

Hatujawahi kabisa kukubali uwezo binafsi wa mtu na tukajivunia watu hao ndani ya chama hata nje ya chama, hiki ndicho kinachotafuna mataifa yenye watu aina hizi, Kwenye mataifa yenye watu wanaokubali uwezo wa mmojammoja, watu wenye uwezo mkubwa hutunzwa kama mboni ya jicho kwa ajili ya mambo ya nchi zao, tofauti na nchi hizi zingine ambapo mwenye uwezo mkubwa anaweza kutafuutwa ikiwezekana apotezwe! Jamani haya mambo yapo mjuwe!

Kwa mantiki hiyo, mataifa yenye watu kama hao, wasiokubali uwezo wa watu wao, huishi kwa mashindano na kwa makundi makundi ya kisiasa ili kusaka madaraka pasina kujali uwezo wao wa kushughurikia kero za wananchi

Na kwa kuwa nchi kama hizo, wananchi wake kulingana na nchi waliopo, huwa kama kuku broiler, muda ukifika wa uchaguzi huletewa pumba tena ili mchinjaji akiwa anachinja, wengine wakiendelea kudonoa pumba mdogomdogo wakisubiri maumivu yao

Je, ni kweli sasa, kuna tofauti ya kufikiri na kutenda kulingana na nchi uliyopo?

Mwingine anaweza kusema, Wa Africa ndivyo tulivyo, lakini kuna waafrica ambao wako nje ya bala la Africa wakifanya mambo makubwa sana, tunayo mifano mingi kwa watu wenye ngozi nyeusi waliowahi kufanya mambo makubwa na yakawa historical mpaka leo!
 
Mfano mdogo tu, kwa sasa karibu kila taifa lipo katika hali ya kubana matumizi kulingana na hali ya mwenendo wa uchumi duniani, lakini utakuta yapo mataifa mengine ambayo ndiyo kwanza wanashindana kutumbua kodi za wananchi wake, na ndiyo maana huwenda kuna uwezekano kabisa wa kimazingira kwa mtu kuwa na fikira duni kulingana na nchi aliyopo!
 
Hii mada yako umechanganya vitu vingi sana.

Maendeleo, uwezo wa watu kufikiri na nchi aliyopo, demokrasia, nk

Sijui kwanini umezunguka kote huko, kama issue ni maendeleo, au matumizi mabovu ya mali ya umma, tatizo haliletwi na nchi aliyopo au uwezo wa kufikiri.

Tumeona hata maprofesa wetu uwezo wao wa kufikiri hushuka pale wanapojiunga na CCM, hii inasababishwa na ubinafsi, wanaweka akili zao pembeni ili watimize malengo yao, kujaza matumbo yao.

Hapo utaona uwezo wa watu kufikiri (ubinafsi) unaathiri maendeleo ya nchi husika (Tanzania) kwasababu ya ukosefu wa demokrasia kwenye chaguzi zetu (tunme ya CCM inawabeba).

Dawa ya hili tatizo ni Katiba Mpya, iwaweke huru wasomi wetu kutumia maarifa yao kuendeleza nchi bila hofu ya kutumbuliwa na Rais asipopendezwa na utendaji wao.
 
Je, Uwezo wa mtu kufikiri na kutenda, unaendana na nchi aliyopo?

Kuna mambo ukiyatafakari saana, unaweza kuona kwamba, uhusiano kati ya mtu uwezo wake wa kufikiri na kutenda kunatokana na nchi aliyopo,kuna nchi zina watu wasomi, ambapo mambo yao huendeshwa kitaalamu na kiuweledi wa kutosha, lakini zipo nchi ambazo nazo zinawasomi wa level ileile, lakini kwa jinsi zinavyoendesha mambo yake utadhani hao waliosoma, ni sawa na jamii ya wasiosoma tu na kwamba hawana msaada, msaada wao ni kudhibiti kila anayehoji uwezo wao wa taaluma zao! hii ni mbaya sana

Changamoto nyingine ni kwamba, Zipo nchi ambazo zinajivunia mabadiriko makubwa yanayotokana na matunda ya watu wake kwa kazi nzuri wafanyazo wasomi wake na kunufaisha zaidi watu woke, tofauti kabisa na ilivyo kwa baadhi ya nchi ambazo wasomi wake hawana msaada kabisa kwa watu wao, kazi yao na sifa yao kubwa, hujivunia kwa kujiongezea mishahara tena nyongeza hiyo ya mishahara, haitokani wa weledi na matunda bora ya kazi zao maofisini, ni kuwachangisha tu wananchi na kisha wao kujiongezea mishahara na kupangiana safari mbalimbali nje ya nchi zao na kujlipa posho kubwa kubwa, wakati huohuo nchi utakuta inautajiri mkubwa wa rasilimali asili, Cha kushangaza zaidi, hata wale ambao hawana elimu kubwa kwenye nchi hizo zenye msaada wa wasomi wake, uelewa wao katika mambo mbalimbali juu ya kinachoendelea katika nchi zao, unaweza kudhani elimu zao ndogo, ndiyo uwezo wa watu wenye elimu kubwa kwenye taifa lingine.

Nchi, za watu kama hao, kila jambo hupimwa kwa kutumia vigezo vya leo na miaka mingi ijayo, ikilinganishwa na baadhi ya nchi zenye watu wenye uwezo mdogo wa kufikiri na kutenda, ambapo watu wake hupima mambo yake kwa kutumia vigezo vya leo na kesho tu! elimu ya namna hii hauwezi ukasema imemkomboa mwananchi na kiongozi huyo

katika nchi watu wake ambapo fikra zao na utendaji kazi ulio chini mno, raia wake ni kama kuku broiler, mchinjanji huchukua kuku mmoja baada ya mwingine na hakuna anayepiga kelele, wote ni kimya wakiwa wamepanga foleni zamu kwa zamu

Nchi kama hizo, maendeleo kwao ni magumu saana na hata yakipatikana ni ya maumivu makubwa kwa makundi makubwa ya watu, huku kundi dogo likibadirisha vitu vya anasa kila uchwao na kundi hili kuishi kama liko peponi

Shida zinazotukabiri hasa katika nchi zetu hizi ni uhasama mkubwa uliomo katika vyama na katika suala zima la siasa!

Hatujawahi kabisa kukubali uwezo binafsi wa mtu na tukajivunia watu hao ndani ya chama hata nje ya chama, hiki ndicho kinachotafuna mataifa yenye watu aina hizi, Kwenye mataifa yenye watu wanaokubali uwezo wa mmojammoja, watu wenye uwezo mkubwa hutunzwa kama mboni ya jicho kwa ajili ya mambo ya nchi zao, tofauti na nchi hizi zingine ambapo mwenye uwezo mkubwa anaweza kutafuutwa ikiwezekana apotezwe! Jamani haya mambo yapo mjuwe!

Kwa mantiki hiyo, mataifa yenye watu kama hao, wasiokubali uwezo wa watu wao, huishi kwa mashindano na kwa makundi makundi ya kisiasa ili kusaka madaraka pasina kujali uwezo wao wa kushughurikia kero za wananchi

Na kwa kuwa nchi kama hizo, wananchi wake kulingana na nchi waliopo, huwa kama kuku broiler, muda ukifika wa uchaguzi huletewa pumba tena ili mchinjaji akiwa anachinja, wengine wakiendelea kudonoa pumba mdogomdogo wakisubiri maumivu yao

Je, ni kweli sasa, kuna tofauti ya kufikiri na kutenda kulingana na nchi uliyopo?

Mwingine anaweza kusema, Wa Africa ndivyo tulivyo, lakini kuna waafrica ambao wako nje ya bala la Africa wakifanya mambo makubwa sana, tunayo mifano mingi kwa watu wenye ngozi nyeusi waliowahi kufanya mambo makubwa na yakawa historical mpaka leo!
Ni ukoloni tu, kunakuiga kizuri na kuiga kibaya
 
Hii mada yako umechanganya vitu vingi sana.

Maendeleo, uwezo wa watu kufikiri na nchi aliyopo, demokrasia, nk

Sijui kwanini umezunguka kote huko, kama issue ni maendeleo, au matumizi mabovu ya mali ya umma, tatizo haliletwi na nchi aliyopo au uwezo wa kufikiri.

Tumeona hata maprofesa wetu uwezo wao wa kufikiri hushuka pale wanapojiunga na CCM, hii inasababishwa na ubinafsi, wanaweka akili zao pembeni ili watimize malengo yao, kujaza matumbo yao.

Hapo utaona uwezo wa watu kufikiri (ubinafsi) unaathiri maendeleo ya nchi husika (Tanzania) kwasababu ya ukosefu wa demokrasia kwenye chaguzi zetu (tunme ya CCM inawabeba).

Dawa ya hili tatizo ni Katiba Mpya, iwaweke huru wasomi wetu kutumia maarifa yao kuendeleza nchi bila hofu ya kutumbuliwa na Rais asipopendezwa na utendaji wao.
Barikiwa sana mkuu

umeongelea masuala ya katiba kwamba, huwenda ndio iliyofunga uwezo wa wasomi wetu kiasi cha kuwa watumwa wa maarifa yao kwa watawala, naweza kukuelewa kwa kiasi na kubakia na maswali tena, Kipindi cha utawala uliopita, karibu wasomi wetu wengi walikuwa wakiimba wimbo wa nyungu na kuzibeza kabisa chanjo cha korona, lakini leo wale wale tena wanaimba wimbo wa chanjo na kubeza nyungu, hili nalo ni la kikatiba?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom