Uwezo mdogo wa kufikiri wa madiwani wa Ilala na Meya Jerry Silaa

Bobby

JF-Expert Member
Jan 10, 2008
2,182
1,890
Nia yangu ni kuhoji matumizi yasiyo na tija ya Halmashauri ya Ilala. Kama uko Dar utakuwa umeyaona mabango ambayo yamegharimiwa na Halmshauri ya Ilala yakiwa na ujumbe wa kumpongeza mwenyeketi, makamu mwenyekiti na viongozi wengine wa chama kwa kuchaguliwa tena.

Kwangu mimi hili ni moja ya matumizi ya kijinga na yasiyo na kichwa wala miguu yanayofanywa na Halamshauri zetu.

Meya Jerry Silaa na madiwani wake wanaonekana bado wanaishi kwenye zama za chama kimoja. Unatumiaje kodi za wanachadema, wanaNCCR, wanaTLP, wanaUDP na hata wengine wasio na vyama kumpongeza mwenyekiti wa CCM?

Hivi inakuwaje hatuna pesa za kununua dawa kwa ajili ya hospitali ya Amana na zahanati ya Mnazimmoja lakini tuna pesa kwa ajili ya mabango ya kumpongeza mwenyekiti kwa kuchaguliwa kitu ambacho kila mtu alikitarajia? Meya Silaa kwanini unatumia pesa zetu kwa ajili ya political mileage?

Kwa style hii ya uongozi tulionao then ndoto za maendeleo zinapaswa kufutwa vichwani mwetu.
 
Nami nakuunga mkono kamanda BOBY nimeajaribu kupita maeneo mengi ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilala iko hoi sana kwenye miundo mbinu ya Barabara hasa maeneo ya pembezoni kama kule Ukonga,Kitunda,Kivule ukilinganisha na Wilaya kama ya Kinondoni miundo mbinu inajengwa sana .Kwa mapato Ilala inaongoza kukupata mapato mengi kutokana na majengo,matangazo na masoko.Ubunifu katika Manispaa hii ni duni kama siyo michwa mingi chini ya ndg Jerry mayor kijana lakini hana vision za maendeleo
 
Last edited by a moderator:
Pamoja na hayo, mimi pia huwa nasikitishwa na mabango yenye picha za meya mwenyewe Jerry Slaa kwa kujitukuza badala ya mamilioni ya pesa hizo ambazo ni nyingi katika kusambaza mabango hayo kuzitumia katika maendeleo ya wananchi wa Ilala na DSM kwa ujumla.
 
Nia yangu ni kuhoji matumizi yasiyo na tija ya Halmashauri ya Ilala. Kama uko Dar utakuwa umeyaona mabango ambayo yamegharimiwa na Halmshauri ya Ilala yakiwa na ujumbe wa kumpongeza mwenyeketi, makamu mwenyekiti na viongozi wengine wa chama kwa kuchaguliwa tena. Kwangu mimi hili ni moja ya matumizi ya kijinga na yasiyo na kichwa wala miguu yanayofanywa na Halamshauri zetu. Meya Jerry Silaa na madiwani wake wanaonekana bado wanaishi kwenye zama za chama kimoja. Unatumiaje kodi za wanachadema, wanaNCCR, wanaTLP, wanaUDP na hata wengine wasio na vyama kumpongeza mwenyekiti wa CCM? Hivi inakuwaje hatuna pesa za kununua dawa kwa ajili ya hospitali ya Amana na zahanati ya Mnazimmoja lakini tuna pesa kwa ajili ya mabango ya kumpongeza mwenyekiti kwa kuchaguliwa kitu ambacho kila mtu alikitarajia? Meya Silaa kwanini unatumia pesa zetu kwa ajili ya political mileage? Kwa style hii ya uongozi tulionao then ndoto za maendeleo zinapaswa kufutwa vichwani mwetu.
Siungi mkono but sina uhakika kama wanatumia fedha za Halmashauri na siyo za CCM......Lakini kwa tabia za akina NAPE kuwalazimisha wafanyakazi wa serikali kuhudhuria ziara za CCM lolote linaweza kutokea
 
Pamoja na hayo, mimi pia huwa nasikitishwa na mabango yenye picha za meya mwenyewe Jerry Slaa kwa kujitukuza badala ya mamilioni ya pesa hizo ambazo ni nyingi katika kusambaza mabango hayo kuzitumia katika maendeleo ya wananchi wa Ilala na DSM kwa ujumla.

Katalina thanks personally sikutaka kufika huku ila inaboa sana kwa kweli hivi madiwani wa Ilala hawana uwezo au ndio wamenunuliwa na Meya wao? Kuna bango moja lipo karibu na Azam mtaa wa Mkwepu ni kichefuchefu kweli mpaka unajiuliza haya mabango yanatolewa bure?

Hata kama ni bure basi tuweke jumbe zenye kumake sense japo kidogo basi maana ni aibu pia kuweka jumbe za ajabu ajabu kwenye mabango jamani resources tulizonazo ni kidogo sana kuzichezea kiasi hiki ni kijitafutia laana bure.
 
Siungi mkono but sina uhakika kama wanatumia fedha za Halmashauri na siyo za CCM......Lakini kwa tabia za akina NAPE kuwalazimisha wafanyakazi wa serikali kuhudhuria ziara za CCM lolote linaweza kutokea

Chief Lugina, fedha zinazotumika kwenye haya mabango ni za Halmashauri ya Ilala meaning ni kodi yangu na yako, uhakika kwenye hili asilimia mia kwa mia.
 
Nia yangu ni kuhoji matumizi yasiyo na tija ya Halmashauri ya Ilala. Kama uko Dar utakuwa umeyaona mabango ambayo yamegharimiwa na Halmshauri ya Ilala yakiwa na ujumbe wa kumpongeza mwenyeketi, makamu mwenyekiti na viongozi wengine wa chama kwa kuchaguliwa tena.

Kwangu mimi hili ni moja ya matumizi ya kijinga na yasiyo na kichwa wala miguu yanayofanywa na Halamshauri zetu.

Meya Jerry Silaa na madiwani wake wanaonekana bado wanaishi kwenye zama za chama kimoja. Unatumiaje kodi za wanachadema, wanaNCCR, wanaTLP, wanaUDP na hata wengine wasio na vyama kumpongeza mwenyekiti wa CCM?

Hivi inakuwaje hatuna pesa za kununua dawa kwa ajili ya hospitali ya Amana na zahanati ya Mnazimmoja lakini tuna pesa kwa ajili ya mabango ya kumpongeza mwenyekiti kwa kuchaguliwa kitu ambacho kila mtu alikitarajia? Meya Silaa kwanini unatumia pesa zetu kwa ajili ya political mileage?

Kwa style hii ya uongozi tulionao then ndoto za maendeleo zinapaswa kufutwa vichwani mwetu.

- Kwa tuhuma nzito kama hizi ulitakuwa kuwa na uhakika kuwa hela zilizotumika ni za Jiji na ni za wananchi kitu ambacho knowing Jerry as I do will never do that, nasema never not Jerry!

- Mkuu nenda Ofisi za jiji uulize na upewe dataz za wapi hela za mabango unayoyasema zimetoka, kuliko kuzusha mambo bila facts!!

Es!
 
Katalina thanks personally sikutaka kufika huku ila inaboa sana kwa kweli hivi madiwani wa Ilala hawana uwezo au ndio wamenunuliwa na Meya wao? Kuna bango moja lipo karibu na Azam mtaa wa Mkwepu ni kichefuchefu kweli mpaka unajiuliza haya mabango yanatolewa bure? Hata kama ni bure basi tuweke jumbe zenye kumake sense japo kidogo basi maana ni aibu pia kuweka jumbe za ajabu ajabu kwenye mabango jamani resources tulizonazo ni kidogo sana kuzichezea kiasi hiki ni kijitafutia laana bure.

Siku nimeliona hilo bango lenye picha yake nikachoka kabisa nikasema huyu ni meya akiwa Rais, si ndio picha yake itaonekana nchi nzima. Leo nimepita wameliondoa.
 
- Kwa tuhuma nzito kama hizi ulitakuwa kuwa na uhakika kuwa hela zilizotumika ni za Jiji na ni za wananchi kitu ambacho knowing Jerry as I do will never do that, nasema never not Jerry!

- Mkuu nenda Ofisi za jiji uulize na upewe dataz za wapi hela za mabango unayoyasema zimetoka, kuliko kuzusha mambo bila facts!!

Es!

Mkuu ES I thought hili liko wazi sana hasa kama ungekuwa umefuatilia vizuri mjadala. Its ok kumfahamu huyo meya ila uhakika ni kwamba MABANGO YASIYO NA TIJA NINAYOYAZUNGUMZIA HAPA MALIPO YAKE NI PESA ZA MANISPAA YA ILALA period. Tena kwa kuwa unamfahamu in person mwambie aache kutumia pesa zetu kwa manufaa binafsi ya kisiasa au vinginevyo.
 
Mkuu ES I thought hili liko wazi sana hasa kama ungekuwa umefuatilia vizuri mjadala. Its ok kumfahamu huyo meya ili uhakika ni kwamba MABANGO YASIYO NA TIJA NINAYOYAZUNGUMZIA HAPA MALIPO YAKE NI PESA ZA MANSPAA YA ILALA period.


- Bro I know Jerry on a very close range, ninaweza kuweka any bet kama unataka kwamba Jerry hawezi kutumia hela za Kodi ya wananchi kwa mabango, tatizo ni kwamba mnaandika sana umbeya na majungu halafu mnataka kulazimisha kwamba ni ukweli, how could you say this is the truth kama kweli unamjua Jerry?

- This is absolutely not him, nenda Mnispaa au watumie email najua Jerry mwenyewe atakijubu hela za hayo mabango zinakotoka na kama anahusika, wacheni kuchafua majina ya watu bure!!

Es!
 
Mimi ni mmoja wa watu ambaye nilikua namuona Jerry kama kijana kweli mwenye mawazo yakijana. lakini kwa uupuzi ule aliofanya nimemumfananisha na Napy Nnaue. Hata kama hatuna ushahidi wakua altumia hela za halimashauli ila uwezekani ni mkubwa mno kwasbb ya nembo ya halmashauli. Go Jery. your time has expired.
 
Nami nakuunga mkono kamanda BOBY nimeajaribu kupita maeneo mengi ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilala iko hoi sana kwenye miundo mbinu ya Barabara hasa maeneo ya pembezoni kama kule Ukonga,Kitunda,Kivule ukilinganisha na Wilaya kama ya Kinondoni miundo mbinu inajengwa sana .Kwa mapato Ilala inaongoza kukupata mapato mengi kutokana na majengo,matangazo na masoko.Ubunifu katika Manispaa hii ni duni kama siyo michwa mingi chini ya ndg Jerry mayor kijana lakini hana vision za maendeleo

kwa hali ilivyo sasa hivi ni vigumu sana kutenganisha serikali na chama cha mapinduzi,shughuli za kichama zinagharimu rasilimali zetu ata tusiokuwa wafuasi wa chama chochote,huu ni upofu na ulevi wa hali ya juu kabisa wa chama dola
 
Last edited by a moderator:
- Kwa tuhuma nzito kama hizi ulitakuwa kuwa na uhakika kuwa hela zilizotumika ni za Jiji na ni za wananchi kitu ambacho knowing Jerry as I do will never do that, nasema never not Jerry!

- Mkuu nenda Ofisi za jiji uulize na upewe dataz za wapi hela za mabango unayoyasema zimetoka, kuliko kuzusha mambo bila facts!!

Es!
wewe umeshasahau unatumia ID gani.......unahisi kama unatumia ile ya willy......

sio lazima uwe na degree ya police na investigation toka nyuu yoki kujua kama mabango yale ni upuuzi mkubwa.....so called viongozi wanapenda sana pongezi.......li bango kubwaaa kama lile sio chini ya milioni 5 pale eti kupongezana....upuuzi mkubwa...
 
kama kuna uthibitisho kuwa pesa ya almashauri ndio ilitumika hilo ni tatizo ila kama walitumia karuzuku kao ka chama haina shida.......
 
wewe umeshasahau unatumia ID gani.......unahisi kama unatumia ile ya willy......

sio lazima uwe na degree ya police na investigation toka nyuu yoki kujua kama mabango yale ni upuuzi mkubwa.....so called viongozi wanapenda sana pongezi.......li bango kubwaaa kama lile sio chini ya milioni 5 pale eti kupongezana....upuuzi mkubwa...

- Vipi umemamliza kuiba picha za Masta wa bongo kwenye starehe zao na kwenda kuwauzia magazeti ya udaku? Mwanaume mzima ndiyo kazi inayokuweka mjini na kuomba omba bia watu kwenye mastarehe! pole sana wala sina muda wa kujadili nonsense na mtu kama wewwe!!

Es!
 
kama kuna uthibitisho kuwa pesa ya almashauri ndio ilitumika hilo ni tatizo ila kama walitumia karuzuku kao ka chama haina shida.......

Asigwa, pesa zilizotumika kwenye haya mabango ni za Manispaa ya Kinondoni hakuna shaka kwenye hili nadhani tuzungumze mengine but sio hili. Hofu yangu ni kwamba uccm ndilo tatizo kubwa la Ilala, kwa kuwa madiwani wote na wabunge ni wa ccm so wanajiona kama kamati fulani ya chama na kusahau kuwa pesa tulizowabidhi ni za watanzania (in this case wanailala) bila kujali itikadai zao za chama. Sijaona mabango yakipuuzi kama haya Temeke na Kinondoni.

Jerry Slaa kwa taarifa yako unawaharibia vijana wengine kupata nafasi kwani wote tutaonekana ni wapuuzi na wenye mawazo ya kizee, yakibinafsi na yaliyopitwa na wakati kama haya unayofanya wewe. Unapaswa kuwaangalia kwanza wanailala waliokuheshimu na kukupa nafasi hii kabla ya kuangalia maslahi yako kisiasa na ya chama chako. I used to think wewe ni mtanzania kwanza kabla ya kuwa mwanaccm but nimeprove kwamba I was completely wrong.
 
Back
Top Bottom