Uwezekano wa kuenea kwa salafi jihadi nchini Tanzania

ALLAH ana raha sana kubiganiwa na wanadamu aliyewaumba mwenyewe
images.jpg
 
Ndio

Mifano
Alshababu wanapigwa vita na wanapigana vita na majeshi ya KDF, AMISON

Islamic state(syria) wanapigana vita na Majeshi ya Syria , russia, USA
Hakuna gaidi anayepigana vita acha uongo

Magaidi ni watu waoga wenye silaha, wao huwa wanavizia, yaani wanajificha au wanaenda mahala kwa siri na kulipua

Hiyo ni tabia ya watu waoga. Hawajawai kupigana head to head straight away na majeshi aidha ya Marekani, Israel. Au kwingineko.

Ni sawa na mtu akuvizie barabarani kisha akupige ngumi au nondo na kukimbia kisha aje kujisifu kuwa :

'' Mmepigana akakupiga'' huu ni Umbea mkubwa.

Ingieni ulingoni mpigane ukimpiga una haki ya kujisifu.
 
Hakuna gaidi anayepigana vita acha uongo

Magaidi ni watu waoga wenye silaha, wao huwa wanavizia, yaani wanajificha au wanaenda mahala kwa siri na kulipua

Hiyo ni tabia ya watu waoga. Hawajawai kupigana head to head straight away na majeshi aidha ya Marekani, Israel. Au kwingineko.

Ni sawa na mtu akuvizie barabarani kisha akupige ngumi au nondo na kukimbia kisha aje kujisifu kuwa :

'' Mmepigana akakupiga'' huu ni Umbea mkubwa.

Ingieni ulingoni mpigane ukimpiga una haki ya kujisifu.
Inaonekana hujui maana ya "Mbinu za kivita" kajifunze hilo kwanza then urudi.
 
Da'awa au elimu za Kisalafi zinapingana na masuala yote ya kigaidi na elimu yetu inatutaka kuwatii viongozi wa dola. Hata kama sio Waislamu. Da'awa yetu sio ya kiuanaharakati na tunapinga mambo ya maandamano na mfano wake. Nakukaribisha ktk vikao vyetu vya kusoma dini hapa Dodoma ukae chini usome dini kiusahihi na hapo ndipo utapata utambuzi juu ya akheeda yetu. Lakini pia kwa sasa kuna Majalis za kielimu ya Kisalafi ktk maeneo mengi nchini. Aidha kuna tovuti na live channels zinazorusha darsa na mihadhara yetu. Yote haya yanafanyika bila uficho wowote. Hakuna mahali popote utakuta tukijinasibu na hizo vurugu ulizozitaja. Katika Misikiti na Madrassa zetu utakutana na vitabu tu. Humo hautakutana na majambia wala visu wala bendera wala madufu. Tunaisoma dini kwa juhudi huku tukichakarika vilivyo ktk kutafuta riziki halali. Nasaha yangu kwako ni kumcha Allah, simamia haki na fanya uadilifu ktk maneno na matendo yako. Aidha kabla haujarudi tena hapa, wewe kama mchambuzi, fuatilia yale tunayoyasoma (ukihitaji links nitakupatia) uenda utafaidika na kupata utambuzi mpana zaidi juu ya Da'awa ya Kisafi.
Atembelee www.firqatunnajia.com
 
Inaonekana hujui maana ya "Mbinu za kivita" kajifunze hilo kwanza then urudi.
Hakuna katika uislamu mbinu ya kukimbia.

Kama kweli wale ni wapiganaji wa kiislamu basi wasikimbie wabaki pale pale kama kweli wana lengo la kupiganiandini ya Allah.

Wale ni watu fulani fulani tu ambao ni wajinga wa dini na funia yao wasiokuwa na uelewa.

Ukiwaangalia utaona kama akili zao ziko tofauti na sisi watu wa kawaida.
 
Athari za Salafi -Jihad kuenea katika nchi yetu ya Tanzania, Kwanza ningependa kuchukua nafasi hii kumshukuru MwenyeziMungu mwingi wa Rehma na mwenye Kurehemu, Kabla ya hili janga la Corona tunalopitia hivi sasa mwanzoni mwa mwaka 2019 kulikua kuna matukio mbalimbali ya Ugaidi yaliyokua yanajitokeza katika pande mbalimbali za Africa. Ukiachana na nchi kama Mali, Burkina Faso na Libya ambazo zipo mbali kidogo na ukanda huu wa Africa Mashariki , kuna nchi katika upande wa Afrika Mashariki ambazo zina chembechembe za Ugaidi.

Inajulikana kua Tanzania ilikua moja ya nchi ambazo zilitoa au “kurecruit” wanamgambo wa Al Shabab kule Somalia. Mikoa iliyoongoza kutoa wanamgambo wengi ni Tanga, Mwanza na Dar es Salaam. Katika kipindi kile tulishuhudia kijana wa Kitanzania akihusishwa na mashambulizi ya Garissa. Kijana mstaarab alieyetoka katika familia ya kitajiri ya MBERESERO. Naam nipende kushukuru jeshi la Polisi kipindi kile wakishirikiana na Intelligency kupambana na janga lile sanasana ningependa kumshukuru DCI wa kipindi kile CP Diwani Athumani.

Ukiachana na hayo, mwanzoni mwa mwaka 2020 kuna matukio mengi ya Kigaidi yalikua yanatokea saana katika ukanda wa Afrika ya mashariki pamoja na Kusini , specifically nchini Msumbiji (Mozambique) pamoja na Kenya. Hii inatokana na uwepo wa makundi ya Waislam wenye Itikadi kali za Salafi.

Hii inaleta picha mpaka kule Africa ya Kati ambapo mpaka saiv bado kuna kavuguvugu ka udini kanatawala baina ya “Seleka” na “Anti Balaqa”. Makundi ya Salafi yaliyopo Mozambique yanafanya harakat zake karibia na mpaka wa nch iyetu ya Tanzania na hivo bas kuhatarisha usalama wa Raia kwa ujumla. Hofu yangu kubwa ni kuona baadhi ya Vijana wa Kiislamu kushawishika kuingia katika makundi hayo ya kigaidi kama ilivyotokea miaka iliyopita kule Somalia.

Hivyo bas vyombo vyetu vya ulinzi na Usalama vinapaswa kuzingatia hayo mambo yasijurudie tena. Bado tunahitaj nguvu kazi katika Taifa letu na hivyo bas VIjana wakiiIslam tusishwawishike katika kuyaendea hayo mambo. Mikoa iliyo hatarini zaidi ni ile iliyopo kusini ikiwemo LIndi na Mtwara na ni mikoa ambayo Idadi ya wakazi wengi wao ni waislam .

Na kwa jinsi Serikali ilivyofocus kwenye suala la Corona unawapa muda zaidi kujipanga na kuandaa mikakati madhubuti. Sitoshangaa baada ya kuisha kwa Janga la Corona, janga la Ugaidi kuchkua nafas kama vyombo vyetu vya Ulinzi na Usalama havitatilia mkazo dalili hizi.

ABDULKARIM MZEE

Mwanadiplomasia na Mchambuzi wa Masuala ya Ugaidi katika bara la Afrika


rucotz98@gmail.com
Uko sahihi kuhusu hawa magaidi na namna ulivyoeleza.

Lakini shida ni moja tu,umewapachika magaidi jina la USALAFI.

Hapa ni sawa umewazungumzia magaidi lakini pia umewachafua masalafi kwa kuwatia katika huo ugaidi.

Hii maana yake mtu akisikia mtaani salafi salafi atajua ni wale wale hii inapelekea kuongeza kuwachongea kwa jamii kwa mambo hata ambayo hawanayo.

Nasikitika kuwa uliyeandika haya ni muislamu safi,na nina imani pengine unatofautiana nao mitazamo ama hujawajua vizuri masalafy ni akina nani.

Licha ya matatizo waliyokuwa nayo masalafy katika ufahamu wa mambo ya kisheria ya kifiqhi lakini katika jambo kubwa ambalo wanalipiga vita hawa jamaa ni UGAIDI.

Leo hakuna shekhe yeyote wa bakwata ambae kasimama kuwasema watu wa uamsho kipindi kile,au kuwasema magaidi wa somalia na kenya akina aboud rogo,HAKUNA SHEKHE WA BAKWATA WALA HAWA MASHEIK MAARUFU AKINA OTHMAN MAALIM NA WENGINEO.

Waliosimama kidete ni hawa masalafy akina kassim mafuta,akina hussein sembe na wengineo Allah awalipe,hawa wanajulikana ni katika watu wanaoitangaza daawa ya salaf.

Sasa Sioni kama ulifanya tafiti vizuri kusema kuwa hawa wanaodai jihadi ati nao ni masalafi.

Hili ni tatizo kwa waisla.u,matokeo yake wakiona watu wamevaa kanzu fupi na ndevu nyingi wanajua ndo wale wale matokeo yake pengine wakakamatwa wale ambao sio na wale ndio wako wanaendeleza ugaidi,hii inatokana na eatu kama nyie ambao hamufanyi tafiti yakinifu kabla ya kuzungummza
 
Mbona huwa mnaharibu lugha ama mimi ndo sifahamu lugha ya kiswahili.

Unamaanisha Rehma ni Rehema au
Nini maana ya Rehma?

Kiswahili kimetohoa asilimia 49 ya maneno kutoka lugha ya Kiarabu.

"Rehma" ni miongoni mwa hayo maneno.

"Rehema" ni neno la Kiswahili lililotokana na neno "rehma" la Kiarabu.

Zingatia, mtoa mada ni Muislamu, yawezekana ndiyo maana akaandika "rehma"
 
Hakuna katika uislamu mbinu ya kukimbia.

Kama kweli wale ni wapiganaji wa kiislamu basi wasikimbie wabaki pale pale kama kweli wana lengo la kupiganiandini ya Allah.
Sasa kwanini mtume alikimbia mecca akakimbilia medina??
Vita Ya Uhud ilikuwaje?
unapata faida gani kupotosha makusudi?
 
Kisha katika bonde la Ela bwana akawatia mikononi mwake Daudi akawachinja watu elfu elfu.

Ukisoma kitabu cha Samwi, waamuzi, wafalme utajiuliza hivi kweli hili ni neno la Mungu au nasoma kitabi kilichoandikwa na shatani?
Maana kimejaa unyama na uharifu mkubwa dhidi ya binadamu tena uliobarikiwa na Mungu mwenyewe.

Astaghafirulah!!!
 
Sasa kwanini mtume alikimbia mecca akakimbilia medina??
Kuondoka kwa Mtume makka ni kwa sababu ya kuwa yeye alifanyiwa mipango ya kuuwawa na vitimbi vingi wakati wa kulingania kwake dini.

Hilo liko wazi,na ni kwa sababu watu waliupiga vita uislamu na kuwauwa na kuwatesa wale waliokubali uislamu wa Muhammad.

Hapa tanzania waislamu wanafanya harakati zao za kidini na wanatangaza dini kwa ihuru kuliko ule uhuru wa makka enzi za Mtume.


Vita Ya Uhud ilikuwaje?
unapata faida gani kupotosha makusudi?
Hakuna vita ambayo mtume alivizia watu mtaani wanafanya mambo yao akaanza kuchinja.

Hakuna vita hiyo.

Vita zote za Mtume ni wale maadui hawa waislamu wanapigana ana kwa ana na sio kwamba walikuwa wanavizia watu mitaani majumbani wanawauwa.

Nafahamu kuwa unajivika gamba la uislamu ili tu uuchafue na sio uutetee😅,ili watu waone kuwa wewe ni muislamu na una misimamo ya kigaidi,kumbe wewe mwenyewe ni mtu saaafi wa dini nyingine hahhhahha.
 
Kuondoka kwa Mtume makka ni kwa sababu ya kuwa yeye alifanyiwa mipango ya kuuwawa na vitimbi vingi wakati wa kulingania kwake dini.

Hilo liko wazi,na ni kwa sababu watu waliupiga vita uislamu na kuwauwa na kuwatesa wale waliokubali uislamu wa Muhammad.

Hapa tanzania waislamu wanafanya harakati zao za kidini na wanatangaza dini kwa ihuru kuliko ule uhuru wa makka enzi za Mtume.



Hakuna vita ambayo mtume alivizia watu mtaani wanafanya mambo yao akaanza kuchinja.

Hakuna vita hiyo.

Vita zote za Mtume ni wale maadui hawa waislamu wanapigana ana kwa ana na sio kwamba walikuwa wanavizia watu mitaani majumbani wanawauwa.

Nafahamu kuwa unajivika gamba la uislamu ili tu uuchafue na sio uutetee😅,ili watu waone kuwa wewe ni muislamu na una misimamo ya kigaidi,kumbe wewe mwenyewe ni mtu saaafi wa dini nyingine hahhhahha.
Hujamuelewa jamaa..hapo wewe ulisema kwenye uislam hakuna kukimbia jamaa akasema kuwa muhamad mwenyewe alikimbia mecca, sasa wewe tena unamjibu kwa kusema muhammad hajawahi kuvizia watu..Hata hiyo vita ya uhud waislam walipigwa wakakimbia.
Jibu 1 thing at a time
 
Hujamuelewa jamaa..hapo wewe ulisema kwenye uislam hakuna kukimbia jamaa akasema kuwa muhamad mwenyewe alikimbia mecca, sasa wewe tena unamjibu kwa kusema muhammad hajawahi kuvizia watu..Hata hiyo vita ya uhud waislam walipigwa wakakimbia.
Jibu 1 thing at a time
Kinacholinganishwa sio kukimbia,kinacholinganishwa ni kwa nini walikimbia.

Kuhusu kukimbia mbona mifano Mingi tu,ila kwa nini walikimbia hapo ndo ishu ilipo.

Kukimbia katika uislamu kupo lakini je kukimbia nini ?

Uislamu haujaruhusu mtu kukimbia vitani yaani kukimbia katika jihadi.

Alshabaab wanasema vile wanavyouwa wako jihaad,sasa kama wako jihaad kwa nini wanakimbia ?

Wale waislamu waliokimbia vitani kuna aya zilishuka zikawakemea jambo hilo kwamba ni dhambi kubwa.sasa kukimbia kwao haihalalishi jambo hilo.

Mtume alikimbia sio kwamba alikuwa vitani,alikuwa kwenye maisha yake ya kawaida.
 
Kinacholinganishwa sio kukimbia,kinacholinganishwa ni kwa nini walikimbia.

Kuhusu kukimbia mbona mifano Mingi tu,ila kwa nini walikimbia hapo ndo ishu ilipo.

Kukimbia katika uislamu kupo lakini je kukimbia nini ?

Uislamu haujaruhusu mtu kukimbia vitani yaani kukimbia katika jihadi.

Alshabaab wanasema vile wanavyouwa wako jihaad,sasa kama wako jihaad kwa nini wanakimbia ?

Wale waislamu waliokimbia vitani kuna aya zilishuka zikawakemea jambo hilo kwamba ni dhambi kubwa.sasa kukimbia kwao haihalalishi jambo hilo.

Mtume alikimbia sio kwamba alikuwa vitani,alikuwa kwenye maisha yake ya kawaida.
mjomba ile vita ya uhud walipigwa waislam wote ikiwemo muhammad ikabidi warudi medina.....Kuretreat katika vita ni jambo la kawaida na sio kweli kwamba muhammad alishinda vita vyote au makalifa walishinda vita vyote
 
mjomba ile vita ya uhud walipigwa waislam wote ikiwemo muhammad ikabidi warudi medina.....Kuretreat katika vita ni jambo la kawaida na sio kweli kwamba muhammad alishinda vita vyote au makalifa walishinda vita vyote
Sawa.
 
Back
Top Bottom