Ndugu zangu wapendwa, nimekuwa na mawazo tofauti kuhusu serikali kuendelea kuwatunza viongozi wetu Raisi na Waziri mkuu pale wanapoondoka madarakani.Kwa mujibu wa sheria wanatakiwa kutunzwa hadi mungu anapo wachukua (wanapo fariki) dunia,mimi naona kwa sasa utaratibu huu ubadilishwe wawe wanatunzwa kwa miaka mitano tu, baada ya kuondoka madarakani. baada ya hapo waendelee na maisha yao kama watanzania wengine.Hii itasaidia kuipunguzia mzigo serikali yetu (wananchi) kuwatunza hawa waheshimiwa, kwani baada ya kustaafu naona wanafanya shughuli ambazo zina waingizia kipato.
Naomba mawazo yenu.
Naomba mawazo yenu.