mwengeso
JF-Expert Member
- Nov 27, 2014
- 9,219
- 6,650
Katika hotuba yake kwenye Bunge leo Alhamisi 22/04/2021, Rais Mama Samia, kuhusu uwekezaji, amesema Tutarudisha imani ya Wawekezaji na kutoa vivutio kwa Wawekezaji, tunalalamikiwa sana, kumekuwa na mchakato mrefu Watu wanapotaka kuwekeza Tanzania, Serikali ya Awamu ya Sita tunakwenda kukomesha hili na Uwekezaji utakwenda kwa haraka.
Hakika ni ahadi nzuri kwa wawekezaji waaminifu na wasio. Lakini ameacha maswali ya msingi bila majibu, km:
√ Je, wimbi linaloendelea nchini la kuwanyanyasa wawekezaji wa ndani wadogo wadogo, kwa jina la "Machinga" Rais anawahakikishia nini?
√ Nafasi yao katika uchumi wa nchi yao ni ipi?
√ Vitambulisho vyao vina nguvu tena, au ndio mwisho wake?
Hakika ni ahadi nzuri kwa wawekezaji waaminifu na wasio. Lakini ameacha maswali ya msingi bila majibu, km:
√ Je, wimbi linaloendelea nchini la kuwanyanyasa wawekezaji wa ndani wadogo wadogo, kwa jina la "Machinga" Rais anawahakikishia nini?
√ Nafasi yao katika uchumi wa nchi yao ni ipi?
√ Vitambulisho vyao vina nguvu tena, au ndio mwisho wake?