mwanamichakato
JF-Expert Member
- Mar 20, 2015
- 887
- 705
Ufaransa (France) inapokea watalii si chini ya milioni 80 kila mwaka toka kote duniani. Paris ikiwa kitovu cha kupokea watalii husika. Lakini pamoja na wingi huo wa watalii, Ufaransa haina vivutio vya utalii kwa wingi kama ilivyo Tanzania, Kenya ama Afrika ya Kusini.
Msingi mkubwa wa watalii wengi kutembelea Paris (Ufaransa) ni hospitality, huduma nafuu za mahotel, ukarimu wa wageni na makumbusho mbalimbali katika nchi. Lakini wengi wa watalii hurudi kutembelea tena na tena.
Hapa kwetu tuna vivutio vya kila aina kuanzia mbuga, hifadhi, milima, maporomoko, mapango, fukwe na mengineyo, lakini idadi ya watalii inakuwa kidogo kila mwaka. Na pia kuna jitihada kubwa za Mh Rais Samia Suluhu Hassan kupitia Royal Tour.
Tunakwama wapi? Na nini kifanyike?
Elimu ya kina itolewe kwa wananchi wadau wa utalii kwa kuanza na taxi drivers, hotel operators, viongozi wa viwanja vya ndege, mamlaka za uhifadhi, maafisa uhamiaji, wadau wa afya, wakazi jirani na maeneo ya vivutio na mijini.
Makundi haya yaelimishwe kuhusu uhalisia na saikolojia ya watalii wengi wanaokuja, kwamba si wote ni matajiri, hivyo kasumba ya kuwapiga bei na kuwakomoa ni sawa na uhujumu taifa/uchumi.
Kwa mfano, taxi drivers wa airport zetu za kimataifa wamekuwa wakichaji wageni kati ya dola 35 mpaka 80 kwa safari ya kilomita 10 mpaka 15. Sidhani kama ina afya, huku pia baadhi ya wenye hotel wakichaji zaidi watalii au wageni katika mazingira ambayo wangeweza kuweka gharama za chini, hivyo kuchochea utalii zaidi.
Kwa kuwa sekta ya utalii inaweza liingizia taifa mabilioni ya fedha kila mwaka, hivyo kupunguza utegemezi katika mikopo na misaada, hakuna budi kufanya uwekezaji katika ulinzi wa wageni. Jeshi letu la polisi liwe na kitengo maalumu cha kulinda watalii ili kuongeza usalama wao, kitu ambacho ni chachu kuu ya mipango ya watalii kutembelea au kututembelea mataifa fulani (mataifa yenye usalama mdogo yana nafasi ndogo sana kupata watalii) ukilinganisha na yenye usalama mkubwa.
Vitendo vya watalii kuporwa, kufanyiwa vitendo vya ulaghai na kudhalilishwa havipaswi kutetewa hata kidogo, hivyo vinapaswa kuwa sawa na uhujumu taifa/uchumi.
Ikumbukwe wawekezaji wengi katika nchi zinazoendelea, wengi wao huvutiwa kuwekeza baada ya kuridhishwa na mazingira wakiwa watalii. Hivyo, upo uwezekano mkubwa wa kuunganisha utalii na uwekezaji na kupanua wigo wa mapato kiuchumi na maendeleo ya nchi.
Serikali iruhusu uwekezaji wa vivutio vya kisasa katika fukwe zetu, visiwa vyetu, mapango yetu na milima yetu. Tumethubutu, tumejaribu, tunaweza.
Vyombo vya habari ndani na nje vinapaswa kuwa na vipindi maalumu vinavyohusiana na kuhamasisha utalii wa ndani, kwa mfano, katika mainstream media zote pamoja na media za kidigitali.
Vyombo vya usafiri (Anga, ardhini, nchi kavu) navyo vihusike kuwa na maudhui yaliyoandaliwa maalumu kuhusu utalii.
Utalii ni zaidi ya madini, utalii ni zaidi ya mafuta na gesi. Tunaweza kuendesha taifa letu kwa mapato ya utalii.
Msingi mkubwa wa watalii wengi kutembelea Paris (Ufaransa) ni hospitality, huduma nafuu za mahotel, ukarimu wa wageni na makumbusho mbalimbali katika nchi. Lakini wengi wa watalii hurudi kutembelea tena na tena.
Hapa kwetu tuna vivutio vya kila aina kuanzia mbuga, hifadhi, milima, maporomoko, mapango, fukwe na mengineyo, lakini idadi ya watalii inakuwa kidogo kila mwaka. Na pia kuna jitihada kubwa za Mh Rais Samia Suluhu Hassan kupitia Royal Tour.
Tunakwama wapi? Na nini kifanyike?
Elimu ya kina itolewe kwa wananchi wadau wa utalii kwa kuanza na taxi drivers, hotel operators, viongozi wa viwanja vya ndege, mamlaka za uhifadhi, maafisa uhamiaji, wadau wa afya, wakazi jirani na maeneo ya vivutio na mijini.
Makundi haya yaelimishwe kuhusu uhalisia na saikolojia ya watalii wengi wanaokuja, kwamba si wote ni matajiri, hivyo kasumba ya kuwapiga bei na kuwakomoa ni sawa na uhujumu taifa/uchumi.
Kwa mfano, taxi drivers wa airport zetu za kimataifa wamekuwa wakichaji wageni kati ya dola 35 mpaka 80 kwa safari ya kilomita 10 mpaka 15. Sidhani kama ina afya, huku pia baadhi ya wenye hotel wakichaji zaidi watalii au wageni katika mazingira ambayo wangeweza kuweka gharama za chini, hivyo kuchochea utalii zaidi.
Kwa kuwa sekta ya utalii inaweza liingizia taifa mabilioni ya fedha kila mwaka, hivyo kupunguza utegemezi katika mikopo na misaada, hakuna budi kufanya uwekezaji katika ulinzi wa wageni. Jeshi letu la polisi liwe na kitengo maalumu cha kulinda watalii ili kuongeza usalama wao, kitu ambacho ni chachu kuu ya mipango ya watalii kutembelea au kututembelea mataifa fulani (mataifa yenye usalama mdogo yana nafasi ndogo sana kupata watalii) ukilinganisha na yenye usalama mkubwa.
Vitendo vya watalii kuporwa, kufanyiwa vitendo vya ulaghai na kudhalilishwa havipaswi kutetewa hata kidogo, hivyo vinapaswa kuwa sawa na uhujumu taifa/uchumi.
Ikumbukwe wawekezaji wengi katika nchi zinazoendelea, wengi wao huvutiwa kuwekeza baada ya kuridhishwa na mazingira wakiwa watalii. Hivyo, upo uwezekano mkubwa wa kuunganisha utalii na uwekezaji na kupanua wigo wa mapato kiuchumi na maendeleo ya nchi.
Serikali iruhusu uwekezaji wa vivutio vya kisasa katika fukwe zetu, visiwa vyetu, mapango yetu na milima yetu. Tumethubutu, tumejaribu, tunaweza.
Vyombo vya habari ndani na nje vinapaswa kuwa na vipindi maalumu vinavyohusiana na kuhamasisha utalii wa ndani, kwa mfano, katika mainstream media zote pamoja na media za kidigitali.
Vyombo vya usafiri (Anga, ardhini, nchi kavu) navyo vihusike kuwa na maudhui yaliyoandaliwa maalumu kuhusu utalii.
Utalii ni zaidi ya madini, utalii ni zaidi ya mafuta na gesi. Tunaweza kuendesha taifa letu kwa mapato ya utalii.