Uwaziri siyo jinsia; haiwezekani kisa Jinsia tuwe na Mawaziri wabovu. Ili tusonge mbele tunataka viongozi makini bila kujali dini wala jinsia

dmkali

JF-Expert Member
Nov 17, 2014
11,252
21,345
Nazidi kuwasihi Watanzania wenzangu! Hoja zingine za kipuuzi tuziepuke!

Ajenda ya 50 kwa 50 Pasipo uwezo binafsi haina maana!

Inchi inahitaji maendeleo, Tunaelekea kwenye kasi ya kufanya kazi usiku na mchana

Wanaume wenye uwezo mkubwa wapo wengi mlitaka waachwe ili wakateuliwe wanawake kisa wapaka poda

Baadhi za hoja ukizitafakali ni za kipuuzi sana!

MMESAHAU KWAMBA MAENDELEO YASIPOFIKIWA LAWAMA ZOTE MNAMPA RAIS!

RAIS NI KAMA KOCHA WA TIMU! MSIMPANGIE TIMU! maana mwisho wa siku timu ikifungwa MTAMFURUSHA!
 
Kweli kabisaa
Baadhi ya watu wanafikilisha sana! Nimeshangaa sana kuona Tundu lisu kakurupuka kujadili Jinsia Ili wateuliwe wabovu Azunguke inchi nzima kunanga utendaji mbovu wa RAIS!

Siipendi CCM Lakini baadhi mambo tusipokuwa makini wapinzani tunajipinga wenyewe!

Tumwache Rais afanye ili baadae ndipo tumlaum vizuri
 
Haya mambo yanatutesa sana, kwenye baraza la mawaziri tunataka uwiano wa kidini, kwenye timu ya taifa uwiano wa kidini, kwenye ajira uwiano wa kidini, kwanamna hii hatuwezi fika popote.
 
Haya mambo yanatutesa sana, kwenye baraza la mawaziri tunataka uhuwiano wa kidini, kwenye timu ya taifa uhuwiano wa kidini, kwenye ajira uhuwiano wa kidini, kwanama hii hatuwezi fika popote.
Mkuu umesema vema kabisa. Na ni kweli tupu. Wakati mwingine usitumie neno "UHUWIANO" maana sio kiswahili.. tumia Uhusiano au Uwiano hayo ndio maneno sahihi ya kiswahili sanifu. Nikutakie Asubuhi Njema Mkuu.
 
Haya mambo yanatutesa sana, kwenye baraza la mawaziri tunataka uhuwiano wa kidini, kwenye timu ya taifa uhuwiano wa kidini, kwenye ajira uhuwiano wa kidini, kwanama hii hatuwezi fika popote.
Simba na Yanga uwiano wa kidini

Ni mawazo ya kijinga kweli
 
Ccm mnajipiga dole wenyewe alafu mnanusa, juzi hapa mlisimamisha visimi kuwa chadema inanyanyasa wanawake leo hii mnadai wanawake hawana sifa ya kuingia baraza la mawaziri
 
Kwa hiyo mleta mada unataka kusema wanawake, waislamu na watu kutoka Kaskazini wengi hawana uwezo wa kutosha ndio maana wamekosa nafasi katika baraza jipya!

Okay, sasa tujadili hili.
-Nini mantiki ya serikali ya CCM kuanzisha agenda ya 50/50 kijinsia miaka kadhaa iliyopita wakati mantiki haipo? Kwanini hiyo sera isifutwe kabisa?

-Kwanini haya mambo ya ubaguzi(jinsia, dini, kanda) yanajionyesha wazi wazi sasa na sio hapo kabla? Hivi Wanawake, watu wa kaskazini na waislamu uwezo wao kiutendaji umeshuka ghafla kipindi cha Magufuli tu mpaka wasipate teuzi?
 
Ccm mnajipiga dole wenyewe alafu mnanusa, juzi hapa mlisimamisha visimi kuwa chadema inanyanyasa wanawake leo hii mnadai wanawake hawana sifa ya kuingia baraza la mawaziri
Kwani wakipewa uwaziri ndio manyanyaso yanakoma!?
 
Ndugai aliposema cdm kuna mfumo dume mbona hukuanzisha uzi?
 
Nazidi kuwasihi watanzania wenzangu! Hoja zingine za kipuuzi tuziepuke!

Ajenda ya 50 kwa 50 Pasipo uwezo binafsi haina maana!

Inchi inahitaji maendeleo, Tunaelekea kwenye kasi ya kufanya kazi usiku na mchana!

Wanaume wenye uwezo mkubwa wapo wengi mlitaka waachwe ili wakateuliwe wanawake kisa wapaka poda!

Baadhi za hoja ukizitafakali ni za kipuuzi sana!

MMESAHAU KWAMB MAENDELEO YASIPOFIKIWA LAWAMA ZOTE MNAMPA RAIS!

RAIS NI KAMA KOCHA WA TIMU! MSIMPANGIE TIMU! maana mwisho wa siku timu ikifungwa MTAMFURUSHA!

Najua mtakuja na hoja hovyo hovyo kutetea ujinga uliofanyika. Hakuna wanawake kwenye bunge hili wenye uwezo!? Hiyo hujajibu. Hakuna waislamu hata kumi wenye uwezo kuwa mawaziri? Hakuna wazanzibari hata watano kuwa mawaziri?!
BARAZA LA KISUKUMA HILI?!
 
Kwani wanawake wenye uwezo hawapo?Kwa nini hawapo katika baraza la Mawaziri?
Walioonekana ni hao kina mwalimu! Sasa kama wapo wengine panga Safu yako hapa!
Rais anapoteuwa! Haiishi kuangalia vyeti pekee Bali pia uthubutu, ujasiri, availability kwa maana mda wote hata usiku wa manane, Usiri, na Mlengo wa kisiasa!
 
Walioonekana ni hao kina mwalimu! Sasa kama wapo wengine panga Safu yako hapa!
Rais anapoteuwa! Haiishi kuangalia vyeti pekee Bali pia uthubutu, ujasiri, availability kwa maana mda wote hata usiku wa manane, Usiri, na Mlengo wa kisiasa!
Kwani Tanzania hakuna wanawake wenye sifa hizi ulizozitaja za uthubutu, ujasiri, availability,Usiri, na Mlengo wa kisiasa?
 
Najua mtakuja na hoja hovyo hovyo kutetea ujinga uliofanyika. Hakuna wanawake kwenye bunge hili wenye uwezo!? Hiyo hujajibu. Hakuna waislamu hata kumi wenye uwezo kuwa mawaziri? Hakuna wazanzibari hata watano kuwa mawaziri?!
BARAZA LA KISUKUMA HILI?!
Mwisho wa siku kocha hupanga timu kutokana na wachezaji wanaomuelewa haraka!
ULITAKA AMTEUWE NANI MWENYE UWEZO EBU WEKA LIST YAKO HAPA!
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom