Kipangaspecial
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 19,408
- 25,926
Mwisho wa siku kinageuzwa kuwa mradi wa ccmMkoa wa Geita umeanza maandalizi ya ujenzi wa uwanja wa kisasa wa mpira wa miguu utakaokuwa na uwezo wa kubeba mashabiki 15,000 kwa wakati mmoja.
Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel amesema uwanja huo utajengwa na SUMA JKT kwa awamu kutegemea vyanzo vya mapato ya ndani unatarajiwa kuchukua miaka minne kukamilika.
“Uwepo wa uwanja utasaidia kuvutia wawekezaji na pia kukuza vipaji vya vijana wa mkoa wa Geita lakini pia kukuza sekta ya michezo mkoa wa Geita,” amesema Mhandisi Gabriel.
Uwanja huo utakapokamilika unatajwa kuwa chachu ya kupata timu shiriki kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara.
View attachment 1546965