Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Mechi kali ya Patashika ya ligi kuu Tanzania bara kupigwa leo February 11, 2020 kwenye Uwanja wa Jamhuri mkoani Morogoro, ambapo Wakata Miwa, Wana Tamu Tamu, Mtibwa Sugar wanamkabili Mfalme wa Nyika, Mnyama Mkali, Simba SC.
Mechi kali ya hamsha hamsha yenye kusisimua pamoja na burudani ndani ya uwanja kwa muda wote wa dakika 90 za mchezo, hivyo timu hizi zinakutana ikiwa kila moja kuwa na kumbukumbu ya kupoteza michezo yao iliyopita ambapo Simba walipoteza dhidi ya JKT Tanzania 1-0 huku Mtibwa Sugar wakilala kwa Lipuli FC bakora 1-0.
Kocha wa Simba, Sven Vanderbroeck amesema, amejiandaa kikamilifu pamoja na kufanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza kwa vitendo uwanjani ili kuepuka makosa yaliyopita hivyo iwe hali ya uwanja, mvua au waamuzi wa mchezo haipaswi kuwa sababu, ni ushindi pekee tunawahitaji na wana kazi ya kuhakikisha hilo.
Kocha Zuberi Katwila amesema mchezo unategemewa kuwa mgumu na wa ushindani na kwa upande wao matokeo mabaya yaliyopita kwa mechi tatu mfululizo hayana nafasi ya kuwafanya wasiibuke na ushindi dhidi ya Simba SC.
Kumbuka mchezo kuanzia saa 10: 00 jioni, Usikose Ukaambiwa.
••••Ghazwat•••••Kulitaka Mwana Kulipewa Mwana
UPDATE
Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba imeendelea kujikita kileleni baada ya kuichapa Mtibwa Sugar kwa mabao 3-0 kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.
Katika mchezo huo Simba ilipata mabao yake kupitia nahodha John Bocco, beki Mohamed Hussein na kiungo Hassan Dilunga.
Ushindi huo unaifanya Simba kufikisha pointi 53, kifuatiwa na Azam (44) Yanga (37) kabla ya mechi yake dhidi ya Mbao na Namungo ikiwa ya nne na pointi 36
Mechi kali ya hamsha hamsha yenye kusisimua pamoja na burudani ndani ya uwanja kwa muda wote wa dakika 90 za mchezo, hivyo timu hizi zinakutana ikiwa kila moja kuwa na kumbukumbu ya kupoteza michezo yao iliyopita ambapo Simba walipoteza dhidi ya JKT Tanzania 1-0 huku Mtibwa Sugar wakilala kwa Lipuli FC bakora 1-0.
Kocha wa Simba, Sven Vanderbroeck amesema, amejiandaa kikamilifu pamoja na kufanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza kwa vitendo uwanjani ili kuepuka makosa yaliyopita hivyo iwe hali ya uwanja, mvua au waamuzi wa mchezo haipaswi kuwa sababu, ni ushindi pekee tunawahitaji na wana kazi ya kuhakikisha hilo.
Kocha Zuberi Katwila amesema mchezo unategemewa kuwa mgumu na wa ushindani na kwa upande wao matokeo mabaya yaliyopita kwa mechi tatu mfululizo hayana nafasi ya kuwafanya wasiibuke na ushindi dhidi ya Simba SC.
Kumbuka mchezo kuanzia saa 10: 00 jioni, Usikose Ukaambiwa.
••••Ghazwat•••••Kulitaka Mwana Kulipewa Mwana
UPDATE
Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba imeendelea kujikita kileleni baada ya kuichapa Mtibwa Sugar kwa mabao 3-0 kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro.
Katika mchezo huo Simba ilipata mabao yake kupitia nahodha John Bocco, beki Mohamed Hussein na kiungo Hassan Dilunga.
Ushindi huo unaifanya Simba kufikisha pointi 53, kifuatiwa na Azam (44) Yanga (37) kabla ya mechi yake dhidi ya Mbao na Namungo ikiwa ya nne na pointi 36