Azizi J Hamad
JF-Expert Member
- Sep 20, 2020
- 442
- 230
Aliyekukopa korosho ni nani? Maana ninavyofahamu sehemu sahihi ya kuuza ni kupitia vyama vya ushirika.Baba sisi wengine ni Wakullma tumekopwa korosho zetu mpaka Leo hatujalipwa tuchape Kazi gani?
Wengine ni Wasomi walikua wanafanya Kazi kwenye makampuni Sasa hivi yamefiliisika atachapa kazi gani
Wafanyakazi hakuna ongezeko la mishahara
Ninyi wengine mpo kwenye systems
Waswahili wanasema mwenye shibe hamjui mwenye njaa
Watanzania sio wavivu wala watu wa kulalamika miaka yote tulikua Tunaishi vizuri mpaka huyu alivyo chukua nchi
Kwa Sasa tupo kama burundi
Kweli tulikua tunawashangaa warundi
Sasa hivi Tanzania mbaya Sana kodi ni nyingi kuliko kipato
Mama mja mzito kodi
Maiti haupewi mpaka ulipe kodi yaani we acha tu
Ndio maana hata nchi jirani haziji kununua mazao kwa sababu ya kodi
Narudia Tena watanzania sio wavivu ila Kazi hakuna makampuni yamehama
Viwanda vimefungwa kwa sababu kodi kodi kodi ya kuumiza wafanya biashara
Tunasoma ili tuwe na uwezo wa kujiongeza, kufilisika kwa kampuni sio sababu ya kumfanya mtu ashindwe kuchapa kazi, narudia tena ukiona mtu analalamika sana kipindi hiki cha Magufuli ujue alikuwa anaishi kwa ujanja ujanja kipindi cha nyuma na kipindi hiki sio cha ujanja ujanja tena.
Mazoea yana tabu, ulizoea kuishi bila kufanya kazi na unakula vizuri kutokana na uwepo wa soko jeusi (black market) ambapo kulikuwa na fedha haramu nyingi mitaani, sasa hayo mazoea hayapo tena kila mtu anakula kutokana na jitihada zake.
Mama mjamzito kodi huu ni uongo
Maiti kodi huu ni uongo. Hivi mgonjwa anaumwa na anaendelea kutibiwa huku analipa taratibu, ikitokea akapona atalipa deni lake, ila akifa mnataka asilipe deni umeona wapi hayo mambo? Inabidi alipie deni lake alilopatiwa matibabu wakati wa uhai wake, ili fedha ikatumike kumlipa daktari ili aweze kutibia wagonjwa wengine.
Na mimi nakazia tena ukiona mtu, kampuni, kiwanda au nchi inapata shida kujiendesha, kufanya biashara au kununua bidhaa hapa Tanzania sasa hivi, ujue kampuni hiyo ilikuwa inateleza kiujanja ujanja hapa Tanzania. Tanzania hakuna ujanja ujanja tena, ujanja ujanja sasa basi.
Chagua CCM, Chagua Magufuli.