Tutor B
JF-Expert Member
- Jun 11, 2011
- 9,025
- 6,554
Kama ni uvumilivu, kweli watanzania tumekuwawavumilivu sana. Serikali yetu imekuwa haiwajali wananchi wake na sasa watanzania tufumbuke macho tuweze kuona mbali tulikotoka, tujitazame tuipo na tuangalie kwa makini wapi tunakokwenda.
Mtukio ni mengi lakini binafsi naishangaa serikali na jeshi la polisi. Hivi kwa matukio ya hivi karibuni yanayohusisha siasa, mbona jeshi la polisi limekuwa na kasumba ya kuahidi kuyafanyia uchunguzi lakini hakuna hata moja lililotolewa majibu ya kueleweka? Labda mwana JF yawezekana wewe umeishapata majibu ya matukio yafuatayo:-
Mtukio ni mengi lakini binafsi naishangaa serikali na jeshi la polisi. Hivi kwa matukio ya hivi karibuni yanayohusisha siasa, mbona jeshi la polisi limekuwa na kasumba ya kuahidi kuyafanyia uchunguzi lakini hakuna hata moja lililotolewa majibu ya kueleweka? Labda mwana JF yawezekana wewe umeishapata majibu ya matukio yafuatayo:-
- Kutekwa kwa dr. Ulimboka
- Kuteswa kwa Kibanda,
- Kuuawa kwa Fr.Mushi Zanzibar,
- Kuuawa kwa Mwandishi wa habari Iringa,
- Uchomwaji wa makanisa,
- Bomu la Kanisani Arusha,
- Bomu la kwenye mkutano wa CDM arusha,