UVCCM yakoleza kasi ya ushindi wa CCM Monduli

MASIGA

Senior Member
Aug 29, 2015
130
281
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi wameendelea kuongeza kasi ya ushindi wa CCM katika Jimbo la Monduli kwa kukutana na kuwajengea hamasa vijana kutoka makundi mbalimbali kama vile wajasiriamali, wafanyabiashara wa ndizi, wachonga vinyago, madereva bodaboda na bajaji, wanamichezo na wananchi wa rika zote katika jamii kwa kuwataka kumchagua Ndugu Julius Kalanga siku ya Jumapili tarehe 16/09/2018 kwa tiketi ya CCM kuwa mbunge wa Monduli.

UVCCM imewafahamisha vijana na wananchi wengine kuwa Ndugu Julius Kalanga ana uwezo wa kuwawakilisha vizuri bungeni na anatoka katika chama kimoja na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli ambacho ndicho kinachoongoza serikali hivyo ni rahisi kushirikiana na serikali katika kuzitatua kero za wananchi wa Monduli.

Aidha UVCCM imewahakikishia wanawake, wazee na wasichana kuwa hakuna wa kuwabugudhi au kuwatisha wasijitokeze kupiga kura kwani wamejipanga vizuri kuhakikisha chama viongozi na wanachama wao wapo salama wakati wote wa kampeni na baada ya kampeni hivyo wajitokeze kwa wingi siku ya kupiga kura na wamchague Ndugu Julius Kalanga kuwa Mbunge wa Monduli.

Timu ya kampeni ya UVCCM inaundwa na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Ndugu Musa Mwakitinya, Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha na Mjumbe wa kamati ya utekelezaji UVCCM Taifa Ndugu Saitoti Zelothe, Mjumbe wa Baraza Kuu na Mjumbe wa kamati ya utekelezaji UVCCM Taifa Ndugu Joanfaith Kataraiya, Mhe Edwin Sanda Mbunge wa Kondoa Mjini, Mhe Gudluck Mlinga mbunge wa Ulanga Mashariki na Mhe Mariam Ditopile Mbunge viti maalum kundi la vijana akitokea UVCCM.

Ratiba ya kampeni inaendelea....

#JuliusKalangaTenaMonduli #KaziInaendelea
IMG-20180912-WA0399.jpg
IMG-20180912-WA0398.jpg
IMG-20180912-WA0395.jpg
IMG-20180912-WA0393.jpg
IMG_20180912_180848.jpg
IMG_20180912_182839.jpg
IMG_20180912_182637.jpg
IMG_20180912_174632.jpg
IMG_20180912_161112.jpg
IMG_20180912_162330.jpg
IMG_20180912_174611.jpg
 
Chama kilichoko madarakani huwa hakina haja kubwa ya kujieleza saaana tutaleta hiki, tutafanya vile bali kuwaonyesha kwa kidole yale yanayofanyika.
CCM mbona ahadi tuu na mpo madarakani? Nguvu kubwa inatumika kama vile ndio mnapata usajili?
 
Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Taifa Ndugu Tabia Maulid Mwita amekutana na kundi vijana la manyangulo na makorianga wapatao 319 ambao ndio linalotegemewa kama jeshi la ulinzi kwa kabila la wamaasai. Amewaomba wahakikishe mgombea ubunge wa CCM Ndugu Julius Kalanga anapata kura nyingi za ushindi kwa wao kumpigia kura na kumuombea kura kwa wengine.

Amewaeleza wao ni kundi tegemeo kwenye jamii yao wahakikishe wanapata mbunge atakayesikiliza na kuziwasilisha kero zao serikalini kwa utatuzi ambaye si mwingine ila ni Ndugu Julius Kalanga wa CCM ambaye chama chake kinaongoza serikali na kina Rais wa Nchi ambaye ni Dkt John Pombe Magufuli.

Ndugu Tabia amesema mpaka sasa hakuna wa kuizuia CCM kushinda katika Jimbo la Monduli kwani wananchi wameshajua *"Upinzani hauna desturi ya kutatua kero za wananchi maana wanaamini kwa kufanya hivyo watakosa hoja za kuikosoa serikali iliyopo madarakani ndio maana huwakataza wabunge wake kutoshirikiana na serikali. Kwa kuwa wananchi wa Monduli wanataka maendeleo ni vyema mkamchagua Ndugu Kalanga ili akashirikiane na serikali kwa urahisi kuwaletea maendeleo."*

Vijana hawa wa Kata ya Makuyuni Jimbo la Monduli walimhakikishia Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa kuwa wamejipanga vizuri kuhakikisha wazee, kina mama, na kina dada wanajitokeza kupiga kura kwa amani na utulivu bila kutishwa na yeyote.

Pia vijana wamemuhakikishia Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Ndugu Tabia Kuwa kauli yao ni moja tu *"Wanampa Magufuli Kalanga ili kazi iendelee"*

Kabla ya mkutano wake makamu mwenyekiti alishiriki amsha amsha ya kijiwe kwa kijiwe kumuombea kura Ndugu Kalanga akiwa ameambatana na Mjumbe wa Halmashauri Kuu CCM Taifa Ndugu Musa Mwakitinya, Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha na Mjumbe wa Kamati ya utekelezaji UVCCM Taifa Ndugu Saitoti Zelothe, Mjumbe wa Baraza Kuu UVCCM Taifa na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji UVCCM Taifa Ndugu Joanfaith Kataraia, Mjumbe wa Baraza Kuu UVCCM Taifa kutoka Mkoa wa Arusha Ndugu Lulu Mwacha na Ndugu Ramadhan Mlao kutoka Pwani.

Wengine ni Mhe Gudluck Mlinga Mbunge wa Ulanga Mashariki, Mhe Mariam Ditopile Mbunge Viti maalum kundi la Vijana na Katibu wa CCM Wilaya ya Longido Ndugu Juma Simba Gadafi.


Ratiba ya kampeni inaendelea...

#KaziInaendelea
#JuliusKalangaTenaMonduli
IMG_20180913_175004.jpg
IMG_20180913_162942.jpg
IMG_20180913_175022.jpg
IMG_20180913_162806.jpg
 
Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Taifa Ndugu Tabia Maulid Mwita amekutana na kundi vijana la manyangulo na makorianga wapatao 319 ambao ndio linalotegemewa kama jeshi la ulinzi kwa kabila la wamaasai. Amewaomba wahakikishe mgombea ubunge wa CCM Ndugu Julius Kalanga anapata kura nyingi za ushindi kwa wao kumpigia kura na kumuombea kura kwa wengine.

Amewaeleza wao ni kundi tegemeo kwenye jamii yao wahakikishe wanapata mbunge atakayesikiliza na kuziwasilisha kero zao serikalini kwa utatuzi ambaye si mwingine ila ni Ndugu Julius Kalanga wa CCM ambaye chama chake kinaongoza serikali na kina Rais wa Nchi ambaye ni Dkt John Pombe Magufuli.

Ndugu Tabia amesema mpaka sasa hakuna wa kuizuia CCM kushinda katika Jimbo la Monduli kwani wananchi wameshajua *"Upinzani hauna desturi ya kutatua kero za wananchi maana wanaamini kwa kufanya hivyo watakosa hoja za kuikosoa serikali iliyopo madarakani ndio maana huwakataza wabunge wake kutoshirikiana na serikali. Kwa kuwa wananchi wa Monduli wanataka maendeleo ni vyema mkamchagua Ndugu Kalanga ili akashirikiane na serikali kwa urahisi kuwaletea maendeleo."*

Vijana hawa wa Kata ya Makuyuni Jimbo la Monduli walimhakikishia Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa kuwa wamejipanga vizuri kuhakikisha wazee, kina mama, na kina dada wanajitokeza kupiga kura kwa amani na utulivu bila kutishwa na yeyote.

Pia vijana wamemuhakikishia Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Ndugu Tabia Kuwa kauli yao ni moja tu *"Wanampa Magufuli Kalanga ili kazi iendelee"*

Kabla ya mkutano wake makamu mwenyekiti alishiriki amsha amsha ya kijiwe kwa kijiwe kumuombea kura Ndugu Kalanga akiwa ameambatana na Mjumbe wa Halmashauri Kuu CCM Taifa Ndugu Musa Mwakitinya, Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha na Mjumbe wa Kamati ya utekelezaji UVCCM Taifa Ndugu Saitoti Zelothe, Mjumbe wa Baraza Kuu UVCCM Taifa na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji UVCCM Taifa Ndugu Joanfaith Kataraia, Mjumbe wa Baraza Kuu UVCCM Taifa kutoka Mkoa wa Arusha Ndugu Lulu Mwacha na Ndugu Ramadhan Mlao kutoka Pwani.

Wengine ni Mhe Gudluck Mlinga Mbunge wa Ulanga Mashariki, Mhe Mariam Ditopile Mbunge Viti maalum kundi la Vijana na Katibu wa CCM Wilaya ya Longido Ndugu Juma Simba Gadafi.


Ratiba ya kampeni inaendelea...

#KaziInaendelea
#JuliusKalangaTenaMonduliView attachment 865539View attachment 865541View attachment 865542View attachment 865543
Duuh wamasai wamekula kijani , kweli ccm ni balaaaaaa
 
Chadema wanapoteza tu muda
Jimbo la Monduli ni la familia ya Sokoine Lowasa Ana laana ya Marehemu Sokoine.Alipora Jimbo analifanya lake Na familia yake Bila kupata ridhaa ya familia ya Sokoine.Moja ya sababu kubwa ya yeye Lowasa kushindwa uraisi ni dharau kwa sokoine Na familia yake
 
Jimbo la Monduli ni la familia ya Sokoine Lowasa Ana laana ya Marehemu Sokoine.Alipora Jimbo analifanya lake Na familia yake Bila kupata ridhaa ya familia ya Sokoine.Moja ya sababu kubwa ya yeye Lowasa kushindwa uraisi ni dharau kwa sokoine Na familia yake
Haya maelezo ya familia ya sokoine kukabidhiwa jimbo la monduli ww umeyapata wap? kwenye makabidhiano wakina nani ndio walikuwa mashahidi?
 
Haya maelezo ya familia ya sokoine kukabidhiwa jimbo la monduli ww umeyapata wap? kwenye makabidhiano wakina nani ndio walikuwa mashahidi?
Sokoine hakuwa fisadi kama Lowasa alikuwa Waziri mkuu asiyepokea mshahara Lowasa tapeli fisadi kipindi kile akajifanya clean.Mzee sokoine akamuaminia kumbe kibaka mwizi toka akisoma chuo kikuu UDSM alikuwa Na kesi za kuibia wanafunzi wenzie mabwenini.Hasidi haachi asili.Anayebisha aende UDSM aangalie kama Lowasa hana kesi za kuibia wanachuo wenzie miaka hiyo akisoma.
 
Sokoine hakuwa fisadi kama Lowasa alikuwa Waziri mkuu asiyepokea mshahara Lowasa tapeli fisadi kipindi kile akajifanya clean.Mzee sokoine akamuaminia kumbe kibaka mwezi toka akisoma chuo kukuu UDSM alikuwa Na kesi za kuibia wanafunzi wenzie mabwenini.Hasidi haachi asili.Anayebisha aende UDSM aangalie kama Lowasa hana kesi za kuibia wanachuo wenzie miaka hiyo akisoma.
Hayo maelezo yako hayaonyeshi wapi jimbo la monduli walikabidhiwa familia ya sokoine, zaidi Naona unamshambulia lowassa , mimi siko interested na kashfa za watu kwasababu hata mimi nina kashfa zangu
 
Hayo maelezo yako hayaonyeshi wapi jimbo la monduli walikabidhiwa familia ya sokoine, zaidi Naona unamshambulia lowassa , mimi siko interested na kashfa za watu kwasababu hata mimi nina kashfa zangu
Utajijua Lowasa hana adabu kwa familia ya sokoine tapeli alimyenyekea sana akiwa hai kumbe it was false conman humility Rangi zake halisi alizionyesha 2015. Sasa majibu atayapata uchaguzi wa mbunge Monduli.Ataijua laana ya Marehemu sokoine Alichokisema 2015 kwa dharau wakati Namelok sokoine akipogombea ubunge kupitia CCM bado kipo kwenye mafaili ya familia ya Sokoine
 
Utajijua Lowasa hana adabu kwa familia ya sokoine tapeli alimyenyekea sana akiwa hai kumbe it was false conman humility Rangi zake halisi alizionyesha 2015. Sasa majibu atayapata uchaguzi wa mbunge Monduli.Ataijua laana ya Marehemu sokoine Alichokisema 2015 kwa dharau wakati Namelok sokoine akipogombea ubunge kupitia CCM bado kipo kwenye mafaili ya familia ya Sokoine
Duuh hapa hakuna cha kukusaidia , ila maelezo yako yanaonyesha unatatizo na lowassa (hilo nawaachia wenyewe), mimi nilitaka kujua tu kuwa jimbo la monduli ni kweli kakabidhiwa sokoine na familia yake? hivyo the basi kwasababu umeshindwa kuthibitisha mimi nitachukulia maneno yako kama uzushi tu
 
Hakuna ushindi tena kwa upinzani awamu hii. Ni kupoteza muda na pesa tu. Kichaa kapewa rungu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom