Mnyanyembe wa Mboka
JF-Expert Member
- Feb 10, 2017
- 2,347
- 3,033
Salam kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
KAZI IENDELEE !!!
Ama baada ya salam waswahili wanasema Muungwa akivuliwa nguo huchutama ... !!! UVCCM chutameni kwanza na muinamishe vichwa chini
Nawasihi msiwe kama M/Kiti wenu mtazidi kujidhalilisha kwa unafiki usio na uelekeo, tafuteni uelekeo kwanza ndio muendelee na mapambio yenu huku mkijua mnapambia nini kuelekea wapi tofauti na tulipotoka
Sote tunafahamu kuwa kuna hali ya mkanganyiko imewakuta kuhusu nani asifiwe na nani akandiwe kulingana na propaganda zinazolenga mafanikio ya itikadi na mitazamo ya kiutawala. Na kama kusifiwa au kukandiwa basi iwe ni kwa lipi kati ya SSH na JPM.
Hii ni kwa sababu ipo wazi mbele ya jamii ya watanzania wote bila kujali chama, dini au itikadi, na imeonekana wazi dhahiri shahiri kuwa utawala wa JPM ni sawa na HASI(-) wakati utawala wa Mama unaonekana kuwa ni CHANYA(+)
Kwa hiyo kumsifia Magu ni kumponda Mama na kumsifia Mama ni kumponda Magu. Kwa kufupi Mama kachora mstari kati yake na Magu hivyo basi ni watanzania tu kuamua upande mmoja kati ya upi wa kusifia na upi wa kukandia na kamwe haiwezekani usifie pande zote utakua ni mnafiki wa kiwango cha lami
Ndg. Zangu UVCCM ni wazi kabisa kwa hali ilivyo haiwezekani kusifia wote na kufanya hivyo ni sawa na kutaka kuchanganya Maji na Mafuta yachanganyike ili upate solution moja
Hapa la msingi kila mmoja kwa wakati wake ajifanye kama Kigwangala tu tujue moja au kama alivyofanya Jafo na barakoa yake siku ya kumuaga Magu kitendo bila kuchelewa kabla jogoo halijawika watu wakaigeuka Nyungu
Ukisikia kupotezwa ndio huku lazima uchague moja kuramba matapishi na kukubali kuitwa mnafiki au kukaza na misimamo ya kijiwejiwe.
Kazi mnayo!!!
KAZI IENDELEE !!!
Ama baada ya salam waswahili wanasema Muungwa akivuliwa nguo huchutama ... !!! UVCCM chutameni kwanza na muinamishe vichwa chini
Nawasihi msiwe kama M/Kiti wenu mtazidi kujidhalilisha kwa unafiki usio na uelekeo, tafuteni uelekeo kwanza ndio muendelee na mapambio yenu huku mkijua mnapambia nini kuelekea wapi tofauti na tulipotoka
Sote tunafahamu kuwa kuna hali ya mkanganyiko imewakuta kuhusu nani asifiwe na nani akandiwe kulingana na propaganda zinazolenga mafanikio ya itikadi na mitazamo ya kiutawala. Na kama kusifiwa au kukandiwa basi iwe ni kwa lipi kati ya SSH na JPM.
Hii ni kwa sababu ipo wazi mbele ya jamii ya watanzania wote bila kujali chama, dini au itikadi, na imeonekana wazi dhahiri shahiri kuwa utawala wa JPM ni sawa na HASI(-) wakati utawala wa Mama unaonekana kuwa ni CHANYA(+)
Kwa hiyo kumsifia Magu ni kumponda Mama na kumsifia Mama ni kumponda Magu. Kwa kufupi Mama kachora mstari kati yake na Magu hivyo basi ni watanzania tu kuamua upande mmoja kati ya upi wa kusifia na upi wa kukandia na kamwe haiwezekani usifie pande zote utakua ni mnafiki wa kiwango cha lami
Ndg. Zangu UVCCM ni wazi kabisa kwa hali ilivyo haiwezekani kusifia wote na kufanya hivyo ni sawa na kutaka kuchanganya Maji na Mafuta yachanganyike ili upate solution moja
Hapa la msingi kila mmoja kwa wakati wake ajifanye kama Kigwangala tu tujue moja au kama alivyofanya Jafo na barakoa yake siku ya kumuaga Magu kitendo bila kuchelewa kabla jogoo halijawika watu wakaigeuka Nyungu
Ukisikia kupotezwa ndio huku lazima uchague moja kuramba matapishi na kukubali kuitwa mnafiki au kukaza na misimamo ya kijiwejiwe.
Kazi mnayo!!!