STEIN
JF-Expert Member
- Aug 29, 2010
- 1,770
- 553
Ndugu zangu wanaJF,
Nimetafakari sana kauli za hivi karibuni za hawa wanaojiita watoto wa JK, Makamba, Sumae, Mzindakaya, Lowasa, Msekwa etc. wakiongozwa na redio na TV ya propaganda kama Clouds FM/TV chini ya wanapropaganda kama kina Kibonde wanayo jeuri ya kuwakomboa wanachuo?????
Nashangaa sana kutokana na wazazi wa hawa vijana wanaojiita UVCCM ndio walioshikilia mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu kwa kuamini tutawaongoza wajanja wachache kwa ridhaa ya wajinga wengi, matajiri wachache kwa ridhaa ya masikini wengi.
Eti leo vijana wao wanakuja na kusema wana dhamira ya kweli ya kutetea wanavyuo, hini propagandi iliyopita kiasi maana haingii akilini kuona Ridhiwani anaandamana ili baba yake aivunje bodi ya mikopo nasema haiwezekani hawa mafisadi wachanga wanakuja na agenda ya siri nyuma ya pazia.
Agenda hiyo ni ya kuendelea kuwapumbaza hawa vijana wa vyuo vikuu wasiendelee kudai haki zao za msingi. Kama kweli wanaona hawa vijana wananyanyaswa na wazee wao basi wawataje hadharani kuwa ndio wanaoihujumu bodi ya mikopo.
Na katika hili hawa vijana wamepewa hela za kuwapumbaza vijana ili tu wawe washabiki huku wakiendelea kunyanyasika.
Nasema mtu ambaye CCM anaona bodi inawanyanyasa vijana ajiuzulu mara moja kwani bodi hiyo imeundwa na kuongozwa na makada wa CCM.
Nawashauri wanavyuo waendelee kudai haki zao kupitia serikali zao za wanafunzi na si UVCCM maana wataendelea kuwa mtaji wa CCM na mafisadi hadi lini?
Majuzi tu walikuwa wanasema CDM ndio inapandikiza migomo vyuoni, wiki mbili badae wanasema eti bodi ndio inayasababisha haya, hivi hawa UVCCM na CCM yao wanafikiri sisi tunasau kama wao wanvyosahau mara kwa mara? Hii haikubaliki kamwe.
Naomba tupaze sauti zetu kupitia JF ya kuwaelimisha na kupinga hujuma yeyote dhidi ya wanavyuo.
Mungu ibariki TZ na wau wake.
Nimetafakari sana kauli za hivi karibuni za hawa wanaojiita watoto wa JK, Makamba, Sumae, Mzindakaya, Lowasa, Msekwa etc. wakiongozwa na redio na TV ya propaganda kama Clouds FM/TV chini ya wanapropaganda kama kina Kibonde wanayo jeuri ya kuwakomboa wanachuo?????
Nashangaa sana kutokana na wazazi wa hawa vijana wanaojiita UVCCM ndio walioshikilia mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu kwa kuamini tutawaongoza wajanja wachache kwa ridhaa ya wajinga wengi, matajiri wachache kwa ridhaa ya masikini wengi.
Eti leo vijana wao wanakuja na kusema wana dhamira ya kweli ya kutetea wanavyuo, hini propagandi iliyopita kiasi maana haingii akilini kuona Ridhiwani anaandamana ili baba yake aivunje bodi ya mikopo nasema haiwezekani hawa mafisadi wachanga wanakuja na agenda ya siri nyuma ya pazia.
Agenda hiyo ni ya kuendelea kuwapumbaza hawa vijana wa vyuo vikuu wasiendelee kudai haki zao za msingi. Kama kweli wanaona hawa vijana wananyanyaswa na wazee wao basi wawataje hadharani kuwa ndio wanaoihujumu bodi ya mikopo.
Na katika hili hawa vijana wamepewa hela za kuwapumbaza vijana ili tu wawe washabiki huku wakiendelea kunyanyasika.
Nasema mtu ambaye CCM anaona bodi inawanyanyasa vijana ajiuzulu mara moja kwani bodi hiyo imeundwa na kuongozwa na makada wa CCM.
Nawashauri wanavyuo waendelee kudai haki zao kupitia serikali zao za wanafunzi na si UVCCM maana wataendelea kuwa mtaji wa CCM na mafisadi hadi lini?
Majuzi tu walikuwa wanasema CDM ndio inapandikiza migomo vyuoni, wiki mbili badae wanasema eti bodi ndio inayasababisha haya, hivi hawa UVCCM na CCM yao wanafikiri sisi tunasau kama wao wanvyosahau mara kwa mara? Hii haikubaliki kamwe.
Naomba tupaze sauti zetu kupitia JF ya kuwaelimisha na kupinga hujuma yeyote dhidi ya wanavyuo.
Mungu ibariki TZ na wau wake.