UVCCM: Usalama wa taifa haumsaidii rais, unavuruga nchi kwa maslahi yake

Mbu Sugu,

TISS ndio walioandika barua kwa Waziri Mkuu Lowasa 2007, wakisisitiza "Hoja ya Dr Slaa isiruhusiwe kuingia ukumbini kwa kuwa Serikali haitakuwa na majibu". Kama utakumbuka hoja hiyo ilihusu Uwizi Mkubwa Benki Kuu(BOT na Hazina. Pia katika Taarifa ya Ernst and Young
kampuni inayomilikiwa na vigogo wa TISS ilikuwa moja ya makampuni yaliyojinufaisha na EPA, na JK hadi leo amepata kigugumizi kufikisha Kampuni hiyo mahakamani(Rejea Taarifa ya Ernst and Young).

Kama ushauri wa TISS kwa Waziri Mkuu (Naamini wasingeliweza kumshauri Waziri Mkuu bila kibali au angalau kumjulisha Rais, sasa ulitegemea nini. Watu wanaoitwa Usalama wa Taifa wanageuka kuwa "wahujumu" wa Rasilimali za Taifa! Ni kweli tumshukuru mtu kwa mema aliyofanya, na labda siyo wote pia wameoza, lakini nyumba isiposafishwa kwa uchafu mdogo kwenye kona hatimaye nyumba nzima itanuka na ndiko tulikofika leo.

Hoja yako ni ya kinadharia wakati ushahidi wa maandishi dhidi yao unaonyesha tofauti. Usalama wa Taifa ungelikuwepo, Kampuni iliyowasha umeme (Mwanza) kwa siku mbili 2007 isingeliendelea kulipwa mabilioni ya fedha za walipa kodi wa Tanzania hadi leo, takriban miaka mitatu baadaye. Nadhani malalamiko ya wanajamvi yanaeleweka. Si vema kutetea nadharia isiyo na mshiko mbele ya "documentary evidence".

Ni upungufu wa weredi kama tutaendelea kufikiri kwamba kila jambo zuri au baya nchini limefanywa na majasusi na si vyombo vingine pia. Kwa maana kwamba kama TISS watalaumiwa kwa kila jambo baya linalotokea nchini basi pia wapewe sifa kwa mambo yote mazuri yanayotokea nchini. Ni muhimu tukajifunza mipaka ya uwajibikaji katika mifumo wa kisiasa na kiutendaji ili kutenda haki kwa kila chombo ndani ya mfumo wa serikali.
 
wana JF, mi nafikiri tujitahidi kutumia lugha nzuri tunapomkosoa Mhe. Rais, tabia ya kupenda kumuita mkwere ni dalili ya ukabila, kwa sababu kama anakosea katika kutimiza majukumu yake au kama ana udhaifu ni wake binafsi si kwa sababu ya kabila lake. mimi si mkwere lakini sisi vijana tukendelea na tabia ya kumsema mtu kabila lake akikosea, tunaweka mazingira mabaya ambayo mtu atakuwa anachaguliwa kwa kabila lake

Mbona Pinda anajiita mtoto wa mkulima?....au hilo unaliongeleaje?
 
Hata mimi hawa TISS siwaelewi kwa kweli....ngoja tumsubiri MMKJJ kama ulivyompoint out.
 
Hawana mpango wote hawa (UVCCM); sisi wengine tumevunja mwiko wote wa kuzungumzia taasisi hii na kutaka watu wawajibishwe kwa miaka minne na kuleta reform ya kweli kwenye chombo hicho wao wako wapi? Kama wanaamini TISS ina matatizo si wana wabunge wengi kwanini wasilobby kuleta mabadiliko ya sheria ili TISS ifanyiwe mabadiliko ya kweli.

Kwa kuanzia wanaweza kupitia Ilani ya Chadema kuhusu usalama wa taifa kwani ndio ilani pekee katika uchaguzi mkuu uliopiita iliyokuwa na ajenda ya kufanyia mabadiliko TISS.
 
@Saigoni, mwache Nduka aongee anavyotaka. Ni kama anajaribu kuharibu discussion ya mada husika.
Tuendelee kujadili nafasi ya TISS katika kumsaidia rais ufanisi wa majukumu yake.
 
Kweli Rais tunaye! Yeye kila mtu hamsaidii-anahitaji msaada gani huyu? Nimeshasikia baraza la mawaziri halimsaidii, sekretariati ya chama haimsaidii-anahitaji msaada wa aina gani? Huu si ukilaza wake tu? UVCCM mwambieni Kikwete ukweli - urais na usharobaro mbalimbali. Siku nyingine akisikia kuna nafasi ys urais akae mbali.
 
Hawana mpango wote hawa (UVCCM);



Kwa kuanzia wanaweza kupitia Ilani ya Chadema kuhusu usalama wa taifa kwani ndio ilani pekee katika uchaguzi mkuu uliopiita iliyokuwa na ajenda ya kufanyia mabadiliko TISS.

BLUE..hata chizi alitegemea hii kutoka kwa mwanakijiji mkombozi wa wa tanzania anayepigania uhuru kutoka nje ya nchi.

RED.. Kwa bahati nzuri watanzania walio wengi hawakupenda hayo mabadiliko, ndio maana hawakuinunua ilani ya CDM.
 
Kweli Rais tunaye! Yeye kila mtu hamsaidii-anahitaji msaada gani huyu? Nimeshasikia baraza la mawaziri halimsaidii, sekretariati ya chama haimsaidii-anahitaji msaada wa aina gani? Huu si ukilaza wake tu? UVCCM mwambieni Kikwete ukweli - urais na usharobaro mbalimbali. Siku nyingine akisikia kuna nafasi ys urais akae mbali.
umajua yeye hajiwezi but nadhani kuchagua washauri wazuri napo inahitaji akili ya ziada!
 
BLUE..hata chizi alitegemea hii kutoka kwa mwanakijiji mkombozi wa wa tanzania anayepigania uhuru kutoka nje ya nchi.
RED.. Kwa bahati nzuri watanzania walio wengi hawakupenda hayo mabadiliko, ndio maana hawakuinunua ilani ya CDM.

Hapo kwenye RED kama unamshangaa Mwanakijiji basi inabidi umshangae na Dalai Lama. hivi naomba kuuliza kwani sifa kuu ya kuwa mwanaCCM ni lazima uwe zuzu na kaswende ya ubongo?
 


Hapo kwenye RED kama unamshangaa Mwanakijiji basi inabidi umshangae na Dalai Lama. hivi naomba kuuliza kwani sifa kuu ya kuwa mwanaCCM ni lazima uwe zuzu na kaswende ya ubongo?


Hakuna sehemu nimeshangaa, lakini pia nashukuru leo umetoa mfano unamfaa Mwanakijiji maana naye ni kama Dalai Lama kiongozi wa kidini wa huko Tibet maana na yeye humu ndani ni kama kiongozi wa dini ya kichadema. Hayo ya kaswende ya ubongo labda uwaulize wana CCM, mimi ni mwanachama wa CDM ambaye sikipendi chama changu.(labda niulize mambo ya makasino, na mahawara za watu( shy rose)
 


Hapo kwenye RED kama unamshangaa Mwanakijiji basi inabidi umshangae na Dalai Lama. hivi naomba kuuliza kwani sifa kuu ya kuwa mwanaCCM ni lazima uwe zuzu na kaswende ya ubongo?

mkuuu umefikilia kama mimi ndani ya ccm wachache sana wenye akili ya kawaida ya kufikiri wengi wao mazuzu tuuu!
 
Kwa bahati nzuri watanzania walio wengi hawakupenda hayo mabadiliko, ndio maana hawakuinunua ilani ya CDM.

watanzania waliyapenda sana hayo mabadiliko ndio maana walichagua chadema. Hao TISS ambao UVCCM wanawalalamikia leo wakazikachakachua kura zao wakishirikiana na NEC. Ndio maana NEC hadi leo hawasemi "mshindi" alipata kura ngapi! Fungua website yao uangalie election results. Ni aibu hadi leo miezi mi5 baada ya uchaguzi hakuna final result. Angalia mshindi wa Arumeru magharibi na aliyeapishwa!
 
watanzania waliyapenda sana hayo mabadiliko ndio maana walichagua chadema. Hao TISS ambao UVCCM wanawalalamikia leo wakazikachakachua kura zao wakishirikiana na NEC. Ndio maana NEC hadi leo hawasemi "mshindi" alipata kura ngapi! Fungua website yao uangalie election results. Ni aibu hadi leo miezi mi5 baada ya uchaguzi hakuna final result. Angalia mshindi wa Arumeru magharibi na aliyeapishwa!


Sasa na ninyi mkachukua hatua gani? au rather Dr Slaa ulifanya nini baada ya kushinda urais lakini akaapishwa JK?
 
hawa hawana chochote wananatapatapa tu.....of course wanataka kuonesha picha ya kwamba TISS hawako kwa ajili yao but in fact TISS are doing all for them.....wasitutie changa la macho hawa alah!
 
Wachawi ni wao wenyewe na waangalie sana maana ndio wanajimaliza hivyo, siku hao TUSI sorry TISS watakapoamua kuweka mambo mengine hadharani itakua aibu! Ona jeshi Yemen limejiunga na Wananchi, kuna uwezekano mkubwa hao TISS nao wamejiunga na sisi wanyonge! Thanx TISS
 
Alijisemea mjomba....ukiona paka kakubali kulala chali, omba ruhusa kazini!!!! kwanini na yeye asifanye vivyo hivyo au akina "adella" bado wana mfariji???? asanteni TISS kwa kumui-ignore bosi wenu na kuwatumikia wananchi, si naskia hataki ushauri wenu? anataka ushauri wa my wife wake na wanawe tu!!! so its okay with TISS
 
Hawa jamaa Kama wanalalamika katika Majukwaa ya Habari kama Wapinzani Mbona hawana tofauti na Kikwete sasa! Wao nani atawasaidia maana rais wanataka asaidiwe na TISS. Wapo ruling part wanatakiwa kufanya reform siyo kulalamika.

Kwani hiyo TISS mbona ipo hivyo hivyo tokea enzi, kilicha badilika ni Uongozi wa juu, au wana manaa kuwa Rais aliteuwa DG Bomu! Kama maoni yao ndio hayo kwanini wasipereke kwa rais azimio la kumbadilisha na mawazo yao kama Chama Tawala na Kumuomba Rais kumbadilisha DG bila kujali Dini yake ili kuleta ufanisi wanaodhani wao unakosekana.

Je wanadhani Rais hatakiwi kuchanganya na zake kama alivyoshauri wakati wa malalamiko ya wafanyakazi! Kama ikiwa hashauriki ndani ya system ya Serikali wanadhani system itafanya nini?

Tuliwai kuambiwa kuwa kuna marais wakishauriwa wanaelewa ila wakienda nyumbani kulala na wake zao kesho wanarudi wamebadilika na wamesahau ule ushauri wa Serikali, Je kama yeye ni wa aina hiyo inakuwaje?

Kama Leaks zinasema yeye ndie aliyekataza RA hasikamatwe kuhusu Ufisadi, UVCCM wanataka TISS wafanyeje wamuuwe ili tuchague Rais mwingine! au wanataka wamsaidie vipi? Yeye ndio anafunguo za nguvu ya dola, kama kawafungia chumbani watafanyanini hao waliofungiwa? Kwani wao wanataka kujifanya hawajui kuwa ikulu imejaa waganga wakinyeji! na wanaposhambulia TISS kisiasa wana maana gani? wanataka kutwambia TISS wao wanaifahamu kama chombo cha kiasiasa! au ujumbe wao kwa jamii ni upi? kuwa kuna makubaliano walifanya na RO kuwa akiteuliwa angesaidia sasa wanaona muda unaenda bila kutimiza ahadi ya cheo chake!

UVCCCM bado hawajui lolote, wanalalama bila majibu ya maswali muhimu.
 
wana JF, mi nafikiri tujitahidi kutumia lugha nzuri tunapomkosoa Mhe. Rais, tabia ya kupenda kumuita mkwere ni dalili ya ukabila, kwa sababu kama anakosea katika kutimiza majukumu yake au kama ana udhaifu ni wake binafsi si kwa sababu ya kabila lake. mimi si mkwere lakini sisi vijana tukendelea na tabia ya kumsema mtu kabila lake akikosea, tunaweka mazingira mabaya ambayo mtu atakuwa anachaguliwa kwa kabila lake

Kwa status yake, yeye ni mkwere namba moja, no big deal kumuadress hivyo!! Mambo ya ukabila unataka kuyaleta wewe!!! Duh!
 
Back
Top Bottom