bitimkongwe
JF-Expert Member
- Oct 21, 2009
- 7,347
- 6,738
Nonsense! wanao uwezo wa kumchagulia mtanzania uraia hata kama hana asili ya kiafrika?
Hivi Rostam ndo fisadi pekee Tanzania nzima? Maana kila kitu Rostam Rostam....
Ni wakati wa kujikomba sasa tusishangae! Kama bosi wake wa juu kapata kigugumizi na kutowa siku90 yeye atafanya nini? Hata hivyo Domo jumba ya maneno...........!Mjumbe wa UVCCM mkoa wa Kilimanjaro Paul Makonda ameomba serikali imnyang'anye Rostam uraia na kumfukuza nchini
Source radio one news
Vijana wa CCM ni wapuuzi kweli kweli, na hiyo inaonyesha jinsi uongozi wa CCM ulivyo kwani akina Nchimbi na Makala walianzia huko huko vijana. Wanataka Rostam anyang'anywe uraia na kufukuza nchi ili aende wapi ilihali yeye ni raia wa Tanzania na mbunge wa Igunga?.
Mjumbe wa UVCCM mkoa wa Kilimanjaro Paul Makonda ameomba serikali imnyang'anye Rostam uraia na kumfukuza nchini
Source radio one news
eti Umoja wa vijana wa CCM....pppfff!! Hivi kweli hao ni vijana kiumri...mbona kila nikiona kwenye mikusanyiko yao mi naona ni vizee na njemba zilizokomaa, na nyingine mpaka inatoka oili utosini!!!
Jamani mmeona taarifa ya ITV jinsi UVCCM walivoongea live kuhusu Rostam Aziz kuondoka haraka sana hapa nchini? Mwalionaje hilo ni unafiki au wanamaanisha? Au ndo JF imewachallenge to that extent?
Nani aliyekuambia kuwa RA ni raia mwenzako? Hivi unajua kwanini baadhi ya viongozi wetu hawataki sheria ya kuwa na uraia wa nchi mbili ipitishwe? Sasa ni mojawapo ni RA na ndio maana amekuwa mstari wa mbele kupigania dual citizenship.RA si mwenzetu!!!!!!!!!!
Mnataka Mungu aibariki Tanzania mara ngapi?Kidogokidogo hujaza kibaba,kila ufisadi utakaofanywa na viongozi wetu utakuwa ukiisongesha nchi nyuma kwa maana ya uchumi wake na hapo ni sawa na mtoto anaejumlisha 2+2=I halafu tiki kubwa akidhani anasonga mbele kumbe kila siku anazidi kuwa mjinga.Baba Mungu ibariki Tanzania