Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 301
HOFU ya kung'oana madarakani imegubika mkutano wa baraza kuu la ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) unaofanyika kesho, huku mwenyekiti wake, Hamad Yusuph Masauni, ambaye anadaiwa kuwa alighushi umri, akibeza tuhuma hizo kuwa ni za kipuuzi.
Masauni alichaguliwa kushika wadhifa huo Desemba, 2008 katika uchaguzi uliokuwa umejaa utata na kusababisha mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete kuamua mgombea atoke Zanzibar. Awali wagombea walikuwa Hussein Bashe na Benno Malisa kutoka Bara.
UVCCM leo inafanya mkutano wa kamati ya utekelezaji pamoja na semina wakati kesho kutakuwa na mkutano wa baraza kuu, ambao pia utahudhuriwa na Kikwete. Vikao vyote vinafanyika mjini Iringa.
Hofu ya kung'oana ilionekana dhahiri jana wakati zaidi ya wajumbe 60 kutoka Zanzibar walipokuwa wakiondoka jijini Dar es salaam kuelekea Iringa, wakiimba nyimbo za kumsifu Masauni na kubeza wanaofanya mipango ya kumuengua.
Hata hivyo, vyanzo vingine vya habari vilifafanua kwamba tayari baadhi ya wajumbe kutoka Zanzibar wameandaa maazimio ambayo yanalenga kumng'oa mmoja wa vigogo wa UVCCM kutoka visiwani humo.
Kwa mujibu wa maazimio hayo, wajumbe hao wanataka kigogo huyo aachie ngazi kutokana na kushindwa kusimamia umoja wa vijana visiwani humo na kusababisha shughuli mbalimbali kuzorota.
Awali, habari zilizosambazwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari zilidai kuwa Masauni ameghushi umri wake na hivyo anatakiwa ajiuzulu.
Waraka unaosambazwa unadai kuwa kuna cheti kinachoonyesha kuwa alizaliwa Oktoba 3, 1973 wakati fomu zake za kuomba hati mpya ya kusafiria zinaonyesha alizaliwa Oktoba 3,1979. Lakini Masauni alionekana kutotetereshwa na tuhuma hizo.
"Sijaona huo waraka, lakini naamini ni tuhuma za uongo; zinalenga kunipunguzia kasi yangu ya utendaji katika usimamizi wa rasilimali za umoja, maadili na uwajibikaji," alisema Masauni alipohojiwa na Mwananchi kuhusu waraka huo.
"Labda kuna watu walifikiri wangeweza kuniburuza katika nafasi yangu, lakini sitaacha kusimamia rasilimali za umoja wetu; umoja na mshikamano miongoni mwa vijana na uwajibikaji."
Kiongozi huyo mkuu wa UVCCM alitamba kwamba umoja huo ni imara na ataendelea kusimamia vema matumizi bora ya rasilimali za chama, maadili na uwajibikaji bila kujali watu wanaotaka kumpunguza kasi.
Lakini alipoulizwa kuhusu umri wake halisi, Masauni hakutaka kuwa bayana. "Nilikupa nafasi hiyo ya kuzungumza (na mimi) kwa kifupi kwa sababu ya heshima.
Hapa nipo na watu wengine katika gari nitakuwa nawasumbua. Hizo tuhuma nazisikia tu sijaziona ila naamini hazina msingi," alijibu.
Ingawa hakufafanua tuhuma hizo, Masauni aligusia mchakato wa kumpata mwenyekiti wa jumuiya hiyo, akisema kuwa ulifuata taratibu zote na hivyo tuhuma zinazoibuliwa sasa zina lengo la kuvunjia heshima vikao vya umoja na chama.
"Nilichaguliwa kwa vikao halali, kabla ya hapo watu waliangalia rekodi zetu. Waliangalia mambo ya uadilifu na yote ya msingi... katika mambo yote haya vikao vya chama na hata vyombo vya usalama vilishiriki, sasa sijui watu wanachosema," alilalamika.
Mkuu huyo wa jumuiya hiyo kongwe alisema lengo lake kuu ni kuunganisha vijana, kuleta umoja na kuwajengea uwezo wa kimaendeleo. "Kamwe sitakubali kuona vijana wanagawanyika; lengo ni kuona wanakuwa kitu kimoja, amani, mshikamano na utulivu. Haya ni malengo yangu makuu katika uongozi wa UVCCM," alisisitiza.
Masauni anatarajiwa kumaliza muda wake wa kikatiba ifikapo 2012. Alipoulizwa kama chama chake kimepokea tuhuma hizo dhidi ya Masauni, katibu mkuu wa CCM, Yusuph Makamba alijibu:, "Hilo ni jambo dogo tu haliwezi kumega UVCCM wala kusumbua chama.
"Kama ni tuhuma zitachunguzwa tu na kubainika ukweli au uongo wake... huwezi kusema zinaweza kumega umoja, hilo ni jambo dogo tu mbona!" alibeza Makamba.
Makamba aliongeza:"Kwa sababu tuhuma hizo nimezisikia na kuziona kama ambavyo naamini na wewe (mwandishi) umeziona, jambo la msingi ni kusubiri vikao vya UVCCM vikae na kuleta ukweli."
Aliweka bayana kwamba UVCCM ni taasisi huru ambayo ina vikao vyake vya maamuzi ambavyo ni pamoja na baraza kuu na kamati ya utekelezaji.
Mtendaji huyo mkuu wa chama alisema vikao hivyo vya maamuzi vinaweza kulifanyia kazi suala hilo na kupata ufumbuzi wake wa kina bila chama kuingilia kati.
Masauni alichaguliwa kushika wadhifa huo Desemba, 2008 katika uchaguzi uliokuwa umejaa utata na kusababisha mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete kuamua mgombea atoke Zanzibar. Awali wagombea walikuwa Hussein Bashe na Benno Malisa kutoka Bara.
UVCCM leo inafanya mkutano wa kamati ya utekelezaji pamoja na semina wakati kesho kutakuwa na mkutano wa baraza kuu, ambao pia utahudhuriwa na Kikwete. Vikao vyote vinafanyika mjini Iringa.
Hofu ya kung'oana ilionekana dhahiri jana wakati zaidi ya wajumbe 60 kutoka Zanzibar walipokuwa wakiondoka jijini Dar es salaam kuelekea Iringa, wakiimba nyimbo za kumsifu Masauni na kubeza wanaofanya mipango ya kumuengua.
Hata hivyo, vyanzo vingine vya habari vilifafanua kwamba tayari baadhi ya wajumbe kutoka Zanzibar wameandaa maazimio ambayo yanalenga kumng'oa mmoja wa vigogo wa UVCCM kutoka visiwani humo.
Kwa mujibu wa maazimio hayo, wajumbe hao wanataka kigogo huyo aachie ngazi kutokana na kushindwa kusimamia umoja wa vijana visiwani humo na kusababisha shughuli mbalimbali kuzorota.
Awali, habari zilizosambazwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari zilidai kuwa Masauni ameghushi umri wake na hivyo anatakiwa ajiuzulu.
Waraka unaosambazwa unadai kuwa kuna cheti kinachoonyesha kuwa alizaliwa Oktoba 3, 1973 wakati fomu zake za kuomba hati mpya ya kusafiria zinaonyesha alizaliwa Oktoba 3,1979. Lakini Masauni alionekana kutotetereshwa na tuhuma hizo.
"Sijaona huo waraka, lakini naamini ni tuhuma za uongo; zinalenga kunipunguzia kasi yangu ya utendaji katika usimamizi wa rasilimali za umoja, maadili na uwajibikaji," alisema Masauni alipohojiwa na Mwananchi kuhusu waraka huo.
"Labda kuna watu walifikiri wangeweza kuniburuza katika nafasi yangu, lakini sitaacha kusimamia rasilimali za umoja wetu; umoja na mshikamano miongoni mwa vijana na uwajibikaji."
Kiongozi huyo mkuu wa UVCCM alitamba kwamba umoja huo ni imara na ataendelea kusimamia vema matumizi bora ya rasilimali za chama, maadili na uwajibikaji bila kujali watu wanaotaka kumpunguza kasi.
Lakini alipoulizwa kuhusu umri wake halisi, Masauni hakutaka kuwa bayana. "Nilikupa nafasi hiyo ya kuzungumza (na mimi) kwa kifupi kwa sababu ya heshima.
Hapa nipo na watu wengine katika gari nitakuwa nawasumbua. Hizo tuhuma nazisikia tu sijaziona ila naamini hazina msingi," alijibu.
Ingawa hakufafanua tuhuma hizo, Masauni aligusia mchakato wa kumpata mwenyekiti wa jumuiya hiyo, akisema kuwa ulifuata taratibu zote na hivyo tuhuma zinazoibuliwa sasa zina lengo la kuvunjia heshima vikao vya umoja na chama.
"Nilichaguliwa kwa vikao halali, kabla ya hapo watu waliangalia rekodi zetu. Waliangalia mambo ya uadilifu na yote ya msingi... katika mambo yote haya vikao vya chama na hata vyombo vya usalama vilishiriki, sasa sijui watu wanachosema," alilalamika.
Mkuu huyo wa jumuiya hiyo kongwe alisema lengo lake kuu ni kuunganisha vijana, kuleta umoja na kuwajengea uwezo wa kimaendeleo. "Kamwe sitakubali kuona vijana wanagawanyika; lengo ni kuona wanakuwa kitu kimoja, amani, mshikamano na utulivu. Haya ni malengo yangu makuu katika uongozi wa UVCCM," alisisitiza.
Masauni anatarajiwa kumaliza muda wake wa kikatiba ifikapo 2012. Alipoulizwa kama chama chake kimepokea tuhuma hizo dhidi ya Masauni, katibu mkuu wa CCM, Yusuph Makamba alijibu:, "Hilo ni jambo dogo tu haliwezi kumega UVCCM wala kusumbua chama.
"Kama ni tuhuma zitachunguzwa tu na kubainika ukweli au uongo wake... huwezi kusema zinaweza kumega umoja, hilo ni jambo dogo tu mbona!" alibeza Makamba.
Makamba aliongeza:"Kwa sababu tuhuma hizo nimezisikia na kuziona kama ambavyo naamini na wewe (mwandishi) umeziona, jambo la msingi ni kusubiri vikao vya UVCCM vikae na kuleta ukweli."
Aliweka bayana kwamba UVCCM ni taasisi huru ambayo ina vikao vyake vya maamuzi ambavyo ni pamoja na baraza kuu na kamati ya utekelezaji.
Mtendaji huyo mkuu wa chama alisema vikao hivyo vya maamuzi vinaweza kulifanyia kazi suala hilo na kupata ufumbuzi wake wa kina bila chama kuingilia kati.