johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,891
- 141,824
Hapo ndipo UVCCM ilipofikia imekuwa kama taasisi ya watafuta vyeo wanaotumia mbinu mbadala mbali na elimu. Ninaikumbuka UVCCM ile enzi za akina Sendeka na baadaye Nchimbi na Uhalula kabla Nape naye hajaingia na cheche zake, vijana walishindana kifikra na si " kujipendekeza". Taabu ilianzia pale wazee walipoivamia taasisi na kujiita wadhamini na makamanda wa vijana na kuanza kuitumia jumuiya kama ngazi ya kujipatia madaraka ya " juu" na hapa ndipo vijana walipolewa kabisa. Niwashauri tu UVCCM ambao mko uchaguzini kwa sasa, JITAMBUENI na muikomboe jumuiya yenu ambayo kwa sasa ni kama imetekwanyara na watu fulani fulani ulojo, kuweni makini. Nawatakia uchaguzi mwema!!