Albert Msando
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 1,019
- 171
UVCCM Arusha kesho wameandaa sherehe ya kumpongeza 'Meya' kwa kuchaguliwa kwake. Sishangai kwa 'vijana taifa la kesho' kufanya sherehe ya kumpongeza Meya wakati tuna msiba kwa sababu hayo ndio waliyojifunza na matunda ya CCM!!
Kuna mahali mtu unafika unaamua kumuachia Mungu kwa sababu ukifikiria sana unaweza kutenda dhambi kutokana na hasira na kichefuchefu unachokipata kwa kufikiria jambo fulani. Utashi uliotumika kuandaa sherehe hiyo wanaujua waandaji. Inawezekana waliandaa kabla ya mauaji ya raia lakini bado walikuwa na uwezo wa kuahirisha na kujumuika na waombolezaji wengine hata kama wasipokuja NMC! Kama wanadhani raia wale walijitakia kifo basi Mungu awahukumu marehemu hao, ila kama marehemu wetu wamekufa kutokana na kuchoshwa na dhuluma, uonevu, manyanyaso na ukandamizaji wa viongozi basi Mungu awahukumu UVCCM! Mungu wetu ni Mungu wa HAKI na atatuhukumu wote kwa HAKI!
Nawatakia UVCCM Arusha sherehe njema kesho, wale, wanywe na kufurahi pamoja na nafsi zao. Sisi wengine tunaendelea kuomboleza na tutashiriki kuwasindikiza wananchi wenzetu katika pumziko lao la milele! Amen.
Kuna mahali mtu unafika unaamua kumuachia Mungu kwa sababu ukifikiria sana unaweza kutenda dhambi kutokana na hasira na kichefuchefu unachokipata kwa kufikiria jambo fulani. Utashi uliotumika kuandaa sherehe hiyo wanaujua waandaji. Inawezekana waliandaa kabla ya mauaji ya raia lakini bado walikuwa na uwezo wa kuahirisha na kujumuika na waombolezaji wengine hata kama wasipokuja NMC! Kama wanadhani raia wale walijitakia kifo basi Mungu awahukumu marehemu hao, ila kama marehemu wetu wamekufa kutokana na kuchoshwa na dhuluma, uonevu, manyanyaso na ukandamizaji wa viongozi basi Mungu awahukumu UVCCM! Mungu wetu ni Mungu wa HAKI na atatuhukumu wote kwa HAKI!
Nawatakia UVCCM Arusha sherehe njema kesho, wale, wanywe na kufurahi pamoja na nafsi zao. Sisi wengine tunaendelea kuomboleza na tutashiriki kuwasindikiza wananchi wenzetu katika pumziko lao la milele! Amen.