Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 46,985
- 144,312
Tunashauri uongozi wa Manispaa ya Dodoma kutafakari upya muda walioutoa kwa wananchi waliojitokeza kununua viwanja katika Manispaa hiyo ambapo wanatakiwa kukamilisha malipo yote ndani ya siku 30 tangu tarehe ya kukabidhiwa invoice.
Kwanza bei ya viwanja kwa mita ya mraba kiasi fulani iko juu kwa kiasi fulani kwani bei ya chini kwa square meter moja ni sh 3,000, bei ya kati ni sh 6,000 kwa mita moja ya mraba na bei ya juu ni shilingi 8,000 kwa mita moja ya mraba na hizi bei ni kwa viwanja ambavyo ni kwa ajili ya makazi tu na tukumbuke hii ni bei ya serikali na si ya mtu binafsi.
Bei kwa viwanja vya makazi na biashara ndio ziko juu zaidi kwa mita moja ya mraba ambayo bei ya chini ni kama shilingi 5,000kwa mita ya mraba, bei ya kati shilingi 7,500 na bei ya juu ikiwa ni shilingi 8,500 kwa mita moja ya mraba.
Bei kwa ajili ya viwanja vya kufanyia biashara tu ndio inafika mpaka shilingi 10,000 kwa mita ya mraba na hivi viwanja viko katika eneo la Mtumba eneo liliko katika barabara kuu ya Dodoma to Dar-es-Salaam.
Maeneo mengine ambayo viwanja bado havijaanza kuuzwa ni Nala, Michese na Iyumbu ambako kote bei zinafanana.
Ukweli ni kwamba licha ya kila mtu kutakiwa kuchagua kiwanja chenye ukubwa na bei atakayoimudu lakini muda huo wa siku 30 uliotolewa ni mfupi mno kwa wananchi wengi wa kawaida kumudu.
Kwa mfano kiwanja cha ukubwa wa mita za mraba 700 kwa bei ya shilingi 3,000 kwa mita moja ya mraba thamani yake ni shilingi 2,100,000 ambayo inapaswa kulipwa ndani ya siku 30 tu na ukishindwa unanyang'anywa tena hawalazimiki kukupa taarifa kulingana na maelezo yaliyoko katika invoice.
Kweli wapo watu wenye fedha zao ambao hela kama hiyo ni ndogo sana kwao ila kwa wananchi wa kawaida wenye majukumu mengi ya kifamilia kulipa hela hiyo ndani ya siku 30 ni changamoto unless viwanja hivi vimelenga watu wenye vipato vikubwa kwani hata kwa watumishi wa umma hapo ni lazima wengi watafute mkopo ndio waweze kulipa ndani ya hizo siku 30 zilizotolewa.
Mimi ningewashauri watoe walau miezi miwili mpaka mitatu ya kukamilisha malipo na mtu akishindwa ndio anyang'anywe kiwanja ila tofauti na hapo sitashangaa wananchi wengi wakaja kushindwa kukamilisha malipo haya ndani ya muda uliopangwa licha ya wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye ununuzi wa hivyo viwanja.
Wakati wa CDA walikuwa wanatoa muda wa kutosha kwa watu kulipia kidogokidogo tofauti na leo hii sasa sjui kwasababu Dodoma imekuwa makao makuu ya serikali watu ndio hatuelewi!!
Ile dhana kwamba awamu hii ni wanyonge basi tuitekeleze kwa vitendo na sio kwa maneno tu ya majukwaani.
Anyway, labda wanapima upepo kwanza wakiona hali ni tofauti huenda wakaongeza muda.
Kwanza bei ya viwanja kwa mita ya mraba kiasi fulani iko juu kwa kiasi fulani kwani bei ya chini kwa square meter moja ni sh 3,000, bei ya kati ni sh 6,000 kwa mita moja ya mraba na bei ya juu ni shilingi 8,000 kwa mita moja ya mraba na hizi bei ni kwa viwanja ambavyo ni kwa ajili ya makazi tu na tukumbuke hii ni bei ya serikali na si ya mtu binafsi.
Bei kwa viwanja vya makazi na biashara ndio ziko juu zaidi kwa mita moja ya mraba ambayo bei ya chini ni kama shilingi 5,000kwa mita ya mraba, bei ya kati shilingi 7,500 na bei ya juu ikiwa ni shilingi 8,500 kwa mita moja ya mraba.
Bei kwa ajili ya viwanja vya kufanyia biashara tu ndio inafika mpaka shilingi 10,000 kwa mita ya mraba na hivi viwanja viko katika eneo la Mtumba eneo liliko katika barabara kuu ya Dodoma to Dar-es-Salaam.
Maeneo mengine ambayo viwanja bado havijaanza kuuzwa ni Nala, Michese na Iyumbu ambako kote bei zinafanana.
Ukweli ni kwamba licha ya kila mtu kutakiwa kuchagua kiwanja chenye ukubwa na bei atakayoimudu lakini muda huo wa siku 30 uliotolewa ni mfupi mno kwa wananchi wengi wa kawaida kumudu.
Kwa mfano kiwanja cha ukubwa wa mita za mraba 700 kwa bei ya shilingi 3,000 kwa mita moja ya mraba thamani yake ni shilingi 2,100,000 ambayo inapaswa kulipwa ndani ya siku 30 tu na ukishindwa unanyang'anywa tena hawalazimiki kukupa taarifa kulingana na maelezo yaliyoko katika invoice.
Kweli wapo watu wenye fedha zao ambao hela kama hiyo ni ndogo sana kwao ila kwa wananchi wa kawaida wenye majukumu mengi ya kifamilia kulipa hela hiyo ndani ya siku 30 ni changamoto unless viwanja hivi vimelenga watu wenye vipato vikubwa kwani hata kwa watumishi wa umma hapo ni lazima wengi watafute mkopo ndio waweze kulipa ndani ya hizo siku 30 zilizotolewa.
Mimi ningewashauri watoe walau miezi miwili mpaka mitatu ya kukamilisha malipo na mtu akishindwa ndio anyang'anywe kiwanja ila tofauti na hapo sitashangaa wananchi wengi wakaja kushindwa kukamilisha malipo haya ndani ya muda uliopangwa licha ya wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye ununuzi wa hivyo viwanja.
Wakati wa CDA walikuwa wanatoa muda wa kutosha kwa watu kulipia kidogokidogo tofauti na leo hii sasa sjui kwasababu Dodoma imekuwa makao makuu ya serikali watu ndio hatuelewi!!
Ile dhana kwamba awamu hii ni wanyonge basi tuitekeleze kwa vitendo na sio kwa maneno tu ya majukwaani.
Anyway, labda wanapima upepo kwanza wakiona hali ni tofauti huenda wakaongeza muda.