Uuzaji wa viwanja Butiama hautendi haki, eti ukiwa na Viwanja Vinne unaambiwa uiachie Serikali kimoja

Nyakijooga

JF-Expert Member
Dec 9, 2018
276
473
Mimi nafanya kazi Butiama katika Chuo Kikuu cha Mwalimu Julius Nyerere, wakati wa kuajiriwa, Watumishi wengi tulinunua maeneo karibu na eneo ambalo Serikali ilitazamia kujenga chuo.

Bahati nzuri tukawa tumeenda masomoni lakini tuliporudi miaka mitano baadaye tukakuta maeneo yetu yamepimwa bila sisi kushirikishwa. Tukaanzisha mchakato wa kufuatilia ili kujua imekuwaje yamepimwa na kwa jina gani bila sisi kuhusishwa.

Tulipofuatilia suala hilo kwa Afisa Mipango Mji, alitueleza kuwa upimaji ulifanyika kwa kushirikisha watu, wengi wao walikuwa Wanakijiji ingawa sisi hatukujulishwa kwa namna yoyote, hata kwa njia ya simu.

Baada ya kuchunguza, tulibaini walitaka kutumia uelewa mdogo wa Wanakijiji hao ili kurahisisha mchakato kwa maslahi wanayoyajua wao.

Tulimlalamikia Afisa Mipango kuhusu kutoshirikishwa, tukashauri mchakato huo ubatilishwe na sisi pia tuzingatiwe. Ndipo akataka tukubaliane kuwa, baada ya upimaji, tungekuwa na mgao wa Asilimia 60 kwa 40 ambapo kama eneo lilikuwa na heka 3 au 4 ambalo viwanja 10 vilipatikana, Serikali ingechukua vinne na sisi sita.

Hata hivyo, tulipinga kwa kuwa hatukushirikishwa kwenye mchakato wa awali.

Afisa Mipango aliendelea kuleta ubabe na kutueleza kuwa makubaliano yalikuwa yamepita. Akaamua kuendelea na uuzaji viwanja vilivyopimwa kwa madai kwamba walitupa nafasi ya kuchagua, ila hatukutokea.

Baada ya hapo, walitoa tangazo la kuuza viwanja katika Kitongoji cha Ikorokomyio, eneo ambalo chuo kipya kinajengwa, na sisi tuliona tangazo hilo siku moja kabla ya kuuza viwanja.

Tulipomuuliza kwa nini tangazo lilichelewa, alijibu kuwa lilichelewa kwa sababu ya matatizo ya mtandao, jambo ambalo hatukuliridhia.

Hivi sasa, watu wameanza kununua viwanja hivyo, ikiwemo na maeneo ambayo ni mali yetu, hata sisi ambao hatujakubali mchakato huo.

Unaenda pale unaonesha viwanja vyako, lakini kuna wengine ambao ndani ya vile sita pia kuna vingine vimechukuliwa tena, na hivyo kusababisha mtafaruku mzito uliojaa ubabe usio na maana.

Kitu kingine ni kwamba mtu mwenye kiwanja kimoja hachangii gharama nyingine, yeye analipia tu gharama za upimaji, ambazo si zile zinazofahamika na Serikali yaani Tsh. 130,000/-; badala yake, unapigiwa hesabu ya Tsh. 300 kwa kila mita ya mraba.

Mwenye viwanja viwili hana shida, lakini ukiwa na vitatu hadi vinne unalazimika kuachia kimoja na ukiwa na vitano unaachia viwili kwa Serikali. Hii ni sawa kweli?

Tulipendekeza kwamba, kwa kuwa hatukukubaliana na mchakato wa kwanza, tupatiwe nafasi ya kulipia tu gharama za upimaji kwa viwanja vyote sita.

Hata hivyo, waliendelea kushikilia kuwa haiwezekani kwa sababu viwanja hivyo vinachukuliwa kwa ajili ya huduma kama maji, umeme na barabara.

Tukauliza kwa misingi gani, wakati utaratibu wa huduma hizo unaeleweka ikiwa sio kazi yao? Ni ya mamlaka nyingine, bado kukawa na ugumu.
 
Pateni wakili, aelewe sawasawa shida yenu. Mufungue kesi mahakamani. Mkilalamika tu bila kuchukua hatua ya kisheria itakula kwenu.
 
kesi ya ardhi haianzii mahakamani
mahakama pekee utakayoenda ni mahakama kuu

sehemu ya kwanza ni baraza la kata ikishindikana (nako ni usuluhishi sio uamuzi) unaenda Baraza la ardhi na nyumba la wilaya (huku ndio kuna umauzu na sio usuluhishi) usiporidhika na maamuzi unakata rufaa (Mahakama kuu)
Nendeni mahakamani mkuu
 
Mahakamani mnalipwa vizuri sana...kuna watu wamelipwa Mwanza baada ya jiji kuwavunjia ukuta
 
Mimi nafanya kazi Butiama katika Chuo Kikuu cha Mwalimu Julius Nyerere, wakati wa kuajiriwa, Watumishi wengi tulinunua maeneo karibu na eneo ambalo Serikali ilitazamia kujenga chuo.

Bahati nzuri tukawa tumeenda masomoni lakini tuliporudi miaka mitano baadaye tukakuta maeneo yetu yamepimwa bila sisi kushirikishwa. Tukaanzisha mchakato wa kufuatilia ili kujua imekuwaje yamepimwa na kwa jina gani bila sisi kuhusishwa.

Tulipofuatilia suala hilo kwa Afisa Mipango Mji, alitueleza kuwa upimaji ulifanyika kwa kushirikisha watu, wengi wao walikuwa Wanakijiji ingawa sisi hatukujulishwa kwa namna yoyote, hata kwa njia ya simu.

Baada ya kuchunguza, tulibaini walitaka kutumia uelewa mdogo wa Wanakijiji hao ili kurahisisha mchakato kwa maslahi wanayoyajua wao.

Tulimlalamikia Afisa Mipango kuhusu kutoshirikishwa, tukashauri mchakato huo ubatilishwe na sisi pia tuzingatiwe. Ndipo akataka tukubaliane kuwa, baada ya upimaji, tungekuwa na mgao wa Asilimia 60 kwa 40 ambapo kama eneo lilikuwa na heka 3 au 4 ambalo viwanja 10 vilipatikana, Serikali ingechukua vinne na sisi sita.

Hata hivyo, tulipinga kwa kuwa hatukushirikishwa kwenye mchakato wa awali.

Afisa Mipango aliendelea kuleta ubabe na kutueleza kuwa makubaliano yalikuwa yamepita. Akaamua kuendelea na uuzaji viwanja vilivyopimwa kwa madai kwamba walitupa nafasi ya kuchagua, ila hatukutokea.

Baada ya hapo, walitoa tangazo la kuuza viwanja katika Kitongoji cha Ikorokomyio, eneo ambalo chuo kipya kinajengwa, na sisi tuliona tangazo hilo siku moja kabla ya kuuza viwanja.

Tulipomuuliza kwa nini tangazo lilichelewa, alijibu kuwa lilichelewa kwa sababu ya matatizo ya mtandao, jambo ambalo hatukuliridhia.

Hivi sasa, watu wameanza kununua viwanja hivyo, ikiwemo na maeneo ambayo ni mali yetu, hata sisi ambao hatujakubali mchakato huo.

Unaenda pale unaonesha viwanja vyako, lakini kuna wengine ambao ndani ya vile sita pia kuna vingine vimechukuliwa tena, na hivyo kusababisha mtafaruku mzito uliojaa ubabe usio na maana.

Kitu kingine ni kwamba mtu mwenye kiwanja kimoja hachangii gharama nyingine, yeye analipia tu gharama za upimaji, ambazo si zile zinazofahamika na Serikali yaani Tsh. 130,000/-; badala yake, unapigiwa hesabu ya Tsh. 300 kwa kila mita ya mraba.

Mwenye viwanja viwili hana shida, lakini ukiwa na vitatu hadi vinne unalazimika kuachia kimoja na ukiwa na vitano unaachia viwili kwa Serikali. Hii ni sawa kweli?

Tulipendekeza kwamba, kwa kuwa hatukukubaliana na mchakato wa kwanza, tupatiwe nafasi ya kulipia tu gharama za upimaji kwa viwanja vyote sita.

Hata hivyo, waliendelea kushikilia kuwa haiwezekani kwa sababu viwanja hivyo vinachukuliwa kwa ajili ya huduma kama maji, umeme na barabara.

Tukauliza kwa misingi gani, wakati utaratibu wa huduma hizo unaeleweka ikiwa sio kazi yao? Ni ya mamlaka nyingine, bado kukawa na ugumu.
Poleni sana
 
kesi ya ardhi haianzii mahakamani
mahakama pekee utakayoenda ni mahakama kuu

sehemu ya kwanza ni baraza la kata ikishindikana (nako ni usuluhishi sio uamuzi) unaenda Baraza la ardhi na nyumba la wilaya (huku ndio kuna umauzu na sio usuluhishi) usiporidhika na maamuzi unakata rufaa (Mahakama kuu)
Asante mkùu kwa ufafanuzi
 
Madhali ukiwa na wake watano serikali haichukui yeyote sioni tatizo
 
kesi ya ardhi haianzii mahakamani
mahakama pekee utakayoenda ni mahakama kuu

sehemu ya kwanza ni baraza la kata ikishindikana (nako ni usuluhishi sio uamuzi) unaenda Baraza la ardhi na nyumba la wilaya (huku ndio kuna umauzu na sio usuluhishi) usiporidhika na maamuzi unakata rufaa (Mahakama kuu)
Juzi waziri alisema, kama kuna mgogoro wa aina yoyote wa ardhi, na unaona giza apigiwe simu na yeye atatuma wawakilishi wake, watasikiliza na kutoa suluhu, amegundua viongozi wa halmashauri wengi wanashiriki kutengeneza migogoro ili wanufaike na rushwa za nenda rudi.

Hivyo waathirika wamtafute waziri au naibu wake, Pinda wamshirikishe wamsikilizie atasemaje. Uchaguzi ukikaribia huwa kuna gas inawasukuma sana hawa watu ,na huu ndio muda wenyewe wautumie kwa faida yao.
 
kesi ya ardhi haianzii mahakamani
mahakama pekee utakayoenda ni mahakama kuu

sehemu ya kwanza ni baraza la kata ikishindikana (nako ni usuluhishi sio uamuzi) unaenda Baraza la ardhi na nyumba la wilaya (huku ndio kuna umauzu na sio usuluhishi) usiporidhika na maamuzi unakata rufaa (Mahakama kuu)
Kwa kuwa hii kesi ni dhidi ya serikali ya mtaa na pia mkurugenzi wa upimaji na ramani na mkurugenzi wa mipango miji basi attorney general atahusika.
Kwa asilimia kubwa sana, hii kesi inaenda moja kwa moja High Court. Ni government proceeding kwa hiyo wapate msaada wa kisheria kutoka kwa wakili.
Maoni yangu, demand notice ikaribishe settlement kabla ya tishio ili kama kuna uwezekano wizara/halmashauri iruhusu mwenye ardhi achague kampuni binafsi ya upimaji kwa bei huru. Ingawa kuna uwezekano ukarudi palepale yaani ukapewa compensation ndogo, wakachukua eneo kubwa zaidi.
Kuepuka hilo, jenga angala nyumba ndogo au mabanda ya mbuzi na uwe na mbuzi au mifugo ambayo inapata lishe kwenye ardhi hiyo ili uongeze value, au tumia njia yeyote ya kuongeza thamani ardhi yako ili wakitathmini waone siyo rahisi ku-compensate.
 
Back
Top Bottom