Uuuuuuwi! - I don't even want to try this one..

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
2008-03-07 16:27:01
Na Valery Kiyungu, Kunduchi

Shule ya Msingi Ununio iliyoko katika Kata ya Kunduchi Jijini imepokea msaada wa madawati mapya 148 yaliyo na thamani ya zaidi ya shilingi milioni 264.

Msaada huo uliotolewa na Bw.Peter Jensen, unalenga kupunguza tatizo la uhaba wa madawati hali inayowafanya wanafunzi wengine kukaa chini.

Akipokea msaada huo Bw. Carin Ungele kwa niaba ya Afisa Elimu Manispaa ya Kinondoni, amesema msaada huo utapunguza tatizo la upungufu wa madawati shuleni hapo.

``Manispaa ya Kinondoni imefarijika na misaada ya mara kwa mara ambayo hutolewa na Bw. Jensen hususan katika shule hii ya Ununio,`` akasema Bw. Ungele.

Kwa upande wake, Bw. Jensen amesema aliguswa na tatizo hilo na hivyo kuamua kuwapunguzia kero ya muda mrefu wanafunzi hao.

Aidha ameahidi kuendelea kutoa msaada wa samani shuleni hapo utakaowalenga walimu na wanafunzi ili kuboresha kiwango cha elimu.

``Nitaendelea kuisaidia shule hii kwa kuendelea kutoa misaada mingine zaidi ili kuboresha kiwango cha elimu shuleni hapo,`` akasema Bw. Jensen.


Akizungumza na Alasiri muda mfupi baadae Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Bw. Rubega Rubega amesema kabla ya kupewa msaada huo idadi kubwa ya wanafunzi walikuwa wakikaa chini.

Hii ni mara ya tatu kwa Bwana Jensen kusaidia shule hiyo ya Ununio yenye wanafunzi 737, ambapo katika mwaka 2003, alitoa msaada wa madawati 20, yenyeb uwezo wa kukaliwa na wanafunzi 100, meza 13, kwa ajili ya walimu, na viti 15, pia kwa matumizi ya walimu wa shule hiyo.
 
Yaani ina maana dawati moja ni Tsh - 1,571,428.57 (Shilingi milioni moja laki tano na usheee!!!)???????????????????

Halafu hili tatizo la ya madawati ina maana limeshakuwa sugu na kukosa kabisa ufumbuzi wa kudumu?????????
 
Yaani ina maana dawati moja ni Tsh - 1,571,428.57 (Shilingi milioni moja laki tano na usheee!!!)???????????????????

Halafu hili tatizo la ya madawati ina maana limeshakuwa sugu na kukosa kabisa ufumbuzi wa kudumu?????????

Ina maana hayo madawati yametengenezwa kwa dhahabu, almasi na platinum? Kwa mtaji huu, ufisadi nje nje!

./mwana wa haki!
 
Changa la macho hilo!!!

Madawati hata yangetengenezwa kwa mninga bei labda ni robo ya hiyo tu kwa estimate za juu!!!
 
Yaani ina maana dawati moja ni Tsh - 1,571,428.57 (Shilingi milioni moja laki tano na usheee!!!)???????????????????

Halafu hili tatizo la ya madawati ina maana limeshakuwa sugu na kukosa kabisa ufumbuzi wa kudumu?????????

Waandishi wetu wa habari ni vituko inawezekana kabisa gharama halisi ni shilingi milioni 26.4 kukosa umakini akashindwa kutofautisha na 264 Milioni washika kalamu wetu hawako makini kabisa akikuhoji hakikisha unaona alicho kiandika maana ni wazuri sana kumisinform, walio wengi makini wapo wachache
 
Alitoa msaada wa madawati 20, yenye uwezo wa kukaliwa na wanafunzi 100, meza 13, kwa ajili ya walimu, na viti 15, pia kwa matumizi ya walimu wa shule hiyo.

Kwa hesabu hizi ina maana dawati moja linakaliwa na watu watano mhh!!!!!!!! (Au ndio maana linauzwa 1.57m)sina uhakika na dimensions za hayo madawati an anyway!!!! Na haya mapya kama yana same capacity ina maana tatizo la madawati sasa kwisha shuleni hapo!!!!!!!!!!
 
Hapo tatizo ni uandishi haiingii akilini dawati li cost more than 1.5m never ever!
 
Mwandishi asihukumiwe kwanza ila afafanue tu...!

Akishindwa awe kundi la walewale...!

Kazi kwelikweli...!
 
Kuna mawili hapa!

Kwanza ni msaada mwingine tena wa madawati. Je wazazi, halmashauri ya wilaya na utawala wa shule na hata wizara mama wako wapi? Jukumu la kuhakikisha kuwa Shule zina vitendea kazi kama madawati, meza, viti, vitabu ni la nani? Je bado tutaendelea kusubiri misaada ili kujikimu?

Pili, uwiano wa dawati kwa wanafunzi. Ikiwa dawati moja lakaa wanafunzi watano, je darasa lina wanafunzi wangapi? je ni nafasi gani hawa wanafunzi wanayo kuweza kuwa makini kusoma ikiwa kuna msongamano wa namna hiyo?

Kwa kumalizia, naomba nimchokoze Mwanakijiji, "je hivi ndivyo tulivyo"?
 
Kwa hesabu hizi ina maana dawati moja linakaliwa na watu watano mhh!!!!!!!! (Au ndio maana linauzwa 1.57m)sina uhakika na dimensions za hayo madawati an anyway!!!! Na haya mapya kama yana same capacity ina maana tatizo la madawati sasa kwisha shuleni hapo!!!!!!!!!!

Kwani ni gazeti gani vile?

Gazeti ni Alasiri.
Nadhani ni tatizo la kiuandishi tu.
 
Kuna mawili hapa!

Kwanza ni msaada mwingine tena wa madawati. Je wazazi, halmashauri ya wilaya na utawala wa shule na hata wizara mama wako wapi? Jukumu la kuhakikisha kuwa Shule zina vitendea kazi kama madawati, meza, viti, vitabu ni la nani? Je bado tutaendelea kusubiri misaada ili kujikimu?

Pili, uwiano wa dawati kwa wanafunzi. Ikiwa dawati moja lakaa wanafunzi watano, je darasa lina wanafunzi wangapi? je ni nafasi gani hawa wanafunzi wanayo kuweza kuwa makini kusoma ikiwa kuna msongamano wa namna hiyo?

Kwa kumalizia, naomba nimchokoze Mwanakijiji, "je hivi ndivyo tulivyo"?


Ndivyo tulivyo wengi wetu..... samahani, mwanakijiji angekujibu vinginevyo na maneno mengi kushinda kamusi ya Kichina :)

Misumeno tunayo, magogo ya mbao tunayo, kufua vyuma na kutengeneza misumari tunaweza... kuranda mbao tunaweza, eti tunasubiria msaada wa madawati utafikiri madawati hayo yanatengenezwa kwa alloy kutoka planet mafikiriko... si hivyo tu, jioni yake tunakwenda kwenye kibaraza na kunywa gahawa na kumung'unywa visheti na malumbano lukuki huku tukimpongeza Mzungu kwa kutukomboa kwa madawati! :(
 
Ndivyo tulivyo wengi wetu..... samahani, mwanakijiji angekujibu vinginevyo na maneno mengi kushinda kamusi ya Kichina :)

Misumeno tunayo, magogo ya mbao tunayo, kufua vyuma na kutengeneza misumari tunaweza... kuranda mbao tunaweza, eti tunasubiria msaada wa madawati utafikiri madawati hayo yanatengenezwa kwa alloy kutoka planet mafikiriko... si hivyo tu, jioni yake tunakwenda kwenye kibaraza na kunywa gahawa na kumung'unywa visheti na malumbano lukuki huku tukimpongeza Mzungu kwa kutukomboa kwa madawati! :(

Hahahahaaaaa...Mwanakijiji can be very long winded at times....
 
This is ridiculous!! Poor journalism maybe a reason for such numbers. Si unajua waandishi wa kibongo, uvivu mwingi wakati mwingine anauliza watu waliokuwepo na wao pengine spika mbaya na makelele kibao. or could it be the editor's fault or probably pronunciation za kijerumani??

Nasema hivi kwa sababu I cannot fathom such misuse of money! Pliiizz tell me there is some other reason behind such numbers.
 
unaona hii inathibitisha sivyo tulivyo kama tungekuwa ndivyo tulivyo tungepuuzia na kukubali kuwa dawati moja lina kost milioni 1 na upuuzi na linaweza kukaliwa na watu wa tano!

ila wapo watu wanaokubali "ndivyo tulivyo" na huishi hivyo mimi kwa hao simo.
 
This is ridiculous!! Poor journalism maybe a reason for such numbers. Si unajua waandishi wa kibongo, uvivu mwingi wakati mwingine anauliza watu waliokuwepo na wao pengine spika mbaya na makelele kibao. or could it be the editor's fault or probably pronunciation za kijerumani??

Nasema hivi kwa sababu I cannot fathom such misuse of money! Pliiizz tell me there is some other reason behind such numbers.

You can't fathom such misuse of money...? Have you been living under a rock somewhere? In case you forgot...this is Tanzania. Nothing surprises me.
 
Back
Top Bottom