isajorsergio
Platinum Member
- Apr 22, 2018
- 4,125
- 6,250
Maelfu ya wahamiaji kutoka Syria wameanza kumiminika katika mipaka ya nchi za Ulaya wakitokea Turkey. Greece ndio nchi iliyoshuhudia wahamiaji wengi zaidi katika mipaka yake, aidha na raia/wahamiaji kutoka nchi za Pakistan, Iraq, Lebanon na Yemen nao wameunga mkono juhudi.
Turkey ilifungua mipaka yake mapema leo na kuruhusu wahamiaji wanaohitaji kungia Ulaya kupita, kisha jioni ya leo Turkey imetoa magari ya kutosha na yenye standard za kimataifa kusafirisha wahamiaji wasiokuwa na usafiri wakufika mipakani. Hali hii inashuhudiwa katika mji mkuu jijini Instanbul pamoja na majiji na miji mingine pamoja na utoaji wa magari pia zimetolewa boti za kuwawezesha wahamiaji kuingia Ulaya bila bugdha.
Brand new Marcedes-Benz ya mwaka 2019 ikivusha wahamiaji kuingia ulaya
Haya yanatokea baada ya Turkey kupoteza wanajeshi wake mjini Idlib, Syria. Wakati hayo yakiendelea Pakistan imesimama na Turkey na kusema wapo bega kwa bega kupambana na watu hatari wanaoichafua dunia nchi nyingine ni Albania, Uzbekistan, Somalia na Kazakhstan. Muda mfupi baada ya kusemwa hayo - Hilal Kaplan ambaye anayefanya kazi katika kitengo cha rais Erdogan kupitia mtandao wa Tweeter "Twira" aliandika "Let Europe burn too" akiwa na maana "Acha Ulaya iungue pia".
Wakati hayo yakiendelea runinga mbalimbali zimerusha matangazo ya moja kwa moja "Mubashara" zikionesha namna wahamiaji wanavyoingia Turkey na kutoka wenda Ulaya.
Mtandao wa mawasiliano unaomilikiwa na serikali ya Turkey Turçe Telekom umeifungia / limit access mitandao ya Twitter, Facebook, Instagram and Messenger. Ikumbukwe Turkey ndio taifa linalooongoza kwa kuwa na watumiaji na utumiaji wa mtandao wa Twetter.
Ikumbukwe mapema leo Erdogan amenukuliwa akisema "Uthubutu ni jadi yetu na sihitaji kuonesha namna gani nilivyo, lakini subiri"
Turkey ilifungua mipaka yake mapema leo na kuruhusu wahamiaji wanaohitaji kungia Ulaya kupita, kisha jioni ya leo Turkey imetoa magari ya kutosha na yenye standard za kimataifa kusafirisha wahamiaji wasiokuwa na usafiri wakufika mipakani. Hali hii inashuhudiwa katika mji mkuu jijini Instanbul pamoja na majiji na miji mingine pamoja na utoaji wa magari pia zimetolewa boti za kuwawezesha wahamiaji kuingia Ulaya bila bugdha.
Brand new Marcedes-Benz ya mwaka 2019 ikivusha wahamiaji kuingia ulaya
Haya yanatokea baada ya Turkey kupoteza wanajeshi wake mjini Idlib, Syria. Wakati hayo yakiendelea Pakistan imesimama na Turkey na kusema wapo bega kwa bega kupambana na watu hatari wanaoichafua dunia nchi nyingine ni Albania, Uzbekistan, Somalia na Kazakhstan. Muda mfupi baada ya kusemwa hayo - Hilal Kaplan ambaye anayefanya kazi katika kitengo cha rais Erdogan kupitia mtandao wa Tweeter "Twira" aliandika "Let Europe burn too" akiwa na maana "Acha Ulaya iungue pia".
Wakati hayo yakiendelea runinga mbalimbali zimerusha matangazo ya moja kwa moja "Mubashara" zikionesha namna wahamiaji wanavyoingia Turkey na kutoka wenda Ulaya.
Mtandao wa mawasiliano unaomilikiwa na serikali ya Turkey Turçe Telekom umeifungia / limit access mitandao ya Twitter, Facebook, Instagram and Messenger. Ikumbukwe Turkey ndio taifa linalooongoza kwa kuwa na watumiaji na utumiaji wa mtandao wa Twetter.
Ikumbukwe mapema leo Erdogan amenukuliwa akisema "Uthubutu ni jadi yetu na sihitaji kuonesha namna gani nilivyo, lakini subiri"