Uturuki yajitolea kusaidia mazungumzo ya Ukraine na Urusi

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,458
Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki amemwambia mwenzake Volodymir Zelensk wa Ukraine kwamba taifa lake lipo tayari kutoa kila usaidizi katika mchakato wa majadiliano kati ya Urusi na Ukraine.

Ofisi ya Rais ya Uturuki imesema ahadi hiyo imetolewa wakati wa mazungumzo kwa njia ya simu baina ya viongozi hao.

Erdogan amesema uokozi wa majeruhi na raia katika Mji wa Mariupol lazima uhakikishwe. Katika mazungumzo hayo kiongozi huyo wa Uturuki aliongeza kwa kusema taifa lake linajiweka katika dhamana ya msingi wa usimamizi mzuri wa suala hilo.

Ukraine imekuwa katika jitihada ya kusaka hakikisho la kiusalama kutoka kwa mataifa mbalimbali wakati wa mazungumzo.

Source: DW
 
Huyu si ndo amefunga mlango wa bahari nyeusi meli za Urusi haziingii wala hazitoki na ametangaza kufunga anga lake kwa miezi mitatu kumkomoa Urusi?

Hii leo anatoa usaidizi wa amani.
Yawezekana sielewi lolote.
 
Huyu si ndo amefunga mlango wa bahari nyeusi meli za Urusi haziingii wala hazitoki na ametangaza kufunga anga lake kwa miezi mitatu kumkomoa Urusi?

Hii leo anatoa usaidizi wa amani.
Yawezekana sielewi lolote.
Mkumbuke waturuki ni Wagalatia wale
 
Anajisumbua bure.
Madai ya urusi kwa Ukraine hayatekelezeki.
Njia ni moja tu urusi ashindwe kivita au Ukraine ashindwe kivita.
 
Turkey wana nia ya kweli ya kumaliza hii vita. NATO, USA na UK wanataka iendelee ili watest silaha zao dhidi ya silaha za Mrusi
 
Back
Top Bottom