Uturuki yajiondoa kwenye Mkataba wa Kimataifa kuwalinda Wanawake, unachochea talaka na ushoga

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,133
10,843
Serikali ya raisi Tayep Erdogan imejiondoa rasmi kwenye mkataba wa kimataifa unaotaka kuwalinda wanawake dhidi wa matendo ya udhalilishwaji. Hatua hiyo imetajwa kuwa ni ushindi mkubwa wa viongozi wahafidhina wa chama cha AK kinachoongozwa na Rais huyo wakishutumu mkataba huo kama kichocheo cha talaka nyingi nchini humo na pia kuhamasisha ndoa za jinsia moja baina ya wanawake na wanawake.

Kwa mujibu ya wahafidhina hao wa AK nchi hiyo ina sheria nyingi katika wizara tofauti ambazo zinatosha kuwalinda wanawake na jamii nyengine dhidi ya udhalilishwaji.Pamoja na sheria hizo mahakama nazo zimetengeneza kifaa cha kielektronik cha kuwafuatilia wakosaji sugu wanaowadhalilisha wanawake.

Chama cha upinzani cha CHP tangu ulipoanza uvumi wa nchi hiyo kujitoa kimekuwa kikiwahamasisha wanachama wake kuandamana kupinga uamuzi huo kwa madai kuwa kujitoa kwa nchi hiyo kutoka mkataba wa kuwalinda wanawake kutaongeza vitendo vya kudhalilishwa kwa wanawake pamoja na mauwaji dhidi yao.

2020-11-25T173131Z_1408322603_RC2HAK9BSNSC_RTRMADP_3_WOMEN-ANTIVIOLENCE-TURKEY.jpg
 
Katika nchi zinazojitambua, Turkey..si wanafiki


🇦🇷🇦🇷🇦🇷
Ni kweli kabisa. Nchi yenyewe ni ndogo kuliko Tanzania na idadi ya watu wake wanakaribiana na Tanzania.Inafurahisha inapochukua maamuzi haimuangalii mtu usoni dhidi ya maslahi yake. Wamewahi kuvimbishiana na Marekani na Urusi mara kadhaa.
 
Ni kweli kabisa. Nchi yenyewe ni ndogo kuliko Tanzania na idadi ya watu wake wanakaribiana na Tanzania.Inafurahisha inapochukua maamuzi haimuangalii mtu usoni dhidi ya maslahi yake. Wamewahi kuvimbishiana na Marekani na Urusi mara kadhaa.

Mungu amjaalie afya njema na umri mrefu Raisi wao Erdogan. Namkubali sana huyu mwanaume.


🇦🇷🇦🇷🇦🇷
 
Ni kweli kabisa. Nchi yenyewe ni ndogo kuliko Tanzania na idadi ya watu wake wanakaribiana na Tanzania.Inafurahisha inapochukua maamuzi haimuangalii mtu usoni dhidi ya maslahi yake. Wamewahi kuvimbishiana na Marekani na Urusi mara kadhaa.
Mkuu si kweli Uturuki ni kubwa kijogirafia kuliko Tanzania na wala hazina uwiano wowote wa watu ,maana watanzania tupo million 60 Wakati Uturuki ina raia karibia million 85.
 
Mkuu si kweli Uturuki ni kubwa kijogirafia kuliko Tanzania na wala hazina uwiano wowote wa watu ,maana watanzania tupo million 60 Wakati Uturuki ina raia karibia million 85.
Ndivyo nilivyosema.Uturuki ni ndogo kieneo kuliko Tanzania. Na idadi ya watu 85milioni inakaribiana na watanzania milioni 60 wakati kasi ya watanzania kuongezeka ni kubwa kuliko ya Uturuki.
Vyengine vilivyozidi ni Tanzania kuwa na rasilimali nyingi kuliko Uturuki isipokuwa yenyewe ipo eneo nyeti la Kijiografia baina ya Ulaya na Asia hivyo inaizidi Tanzania kifursa za kibiashara na ukuwaji wa viwanda.
 
Ndivyo nilivyosema.Uturuki ni ndogo kieneo kuliko Tanzania. Na idadi ya watu 85milioni inakaribiana na watanzania milioni 60 wakati kasi ya watanzania kuongezeka ni kubwa kuliko ya Uturuki.
Vyengine vilivyozidi ni Tanzania kuwa na rasilimali nyingi kuliko Uturuki isipokuwa yenyewe ipo eneo nyeti la Kijiografia baina ya Ulaya na Asia hivyo inaizidi Tanzania kifursa za kibiashara na ukuwaji wa viwanda.
Mkuu angalia ramani ya dunia vizuri Uturuki ni kubwa kieneo kuliko Tz .
Kwenye suala la watu nakubaliana na wewe Tz tuna zaliana kwa kasi sana.
Kwenye rasilimali nakubaliana na ww Tz ina ina rasilimali kuliko Uturuki,ila linapo kuja kwenye suala la kiuchumi kati ya Uturuki na Tz ni mbingu na aridhi maana Uturuki ni taifa lenye nguvu kiuchumi duniani.
 
Mkuu angalia ramani ya dunia vizuri Uturuki ni kubwa kieneo kuliko Tz .
Kwenye suala la watu nakubaliana na wewe Tz tuna zaliana kwa kasi sana.
Kwenye rasilimali nakubaliana na ww Tz ina ina rasilimali kuliko Uturuki,ila linapo kuja kwenye suala la kiuchumi kati ya Uturuki na Tz ni mbingu na aridhi maana Uturuki ni taifa lenye nguvu kiuchumi duniani.

Turkey
Total783,356 km2 (302,455 sq mi) (36th)

Tanzania
Total947,303 km2 (365,756 sq mi) (31st)

Nikweli kiongozi, Ami yuko sahihi..turkey ni ndogo kidogo kwa tanzania.
 
Back
Top Bottom