Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,480
- 9,241
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ameionya serikali ya Syria kwamba italipa gharama kubwa kutokana na mashambulizi yake dhidi ya majeshi ya Uturuki katika eneo la kaskazini mashariki mwa Syria.
Wanajeshi watano wa Uturuki waliuawa katika mji wa Idlib unaodhibitiwa na upinzani siku ya Jumatatu wiki hii wakati majeshi ya Syria yakiendelea kusonga mbele katika eneo la mapigano.
Wanajeshi wa Uturuki walifyatua makombora kadhaa ili kujibu mashambulizi hayo, lakini Rais Erdogan amesema wataendelea na mashambulizi ya kujihami.