SYENDEKE
Senior Member
- Jul 18, 2011
- 169
- 26
wandugu niko kwenye sherehe za mwenge kwa sasa mwenge wa uhuru umelala mkoa wa iringa wilaya ya mafinga viwanja vya mashujaa karibu na ofisi za ccm wilaya sasa kuna waraka umetoka kwa wafanyakazi wote wa halmashauri ni lazima kuwepo na kukeshe kwenye sherehe za mwenge halafu kuna attendance ya mahudhulio kwa wafanyakazi kila baada ya masaa 5 hadi asubuhi na mwajili(Mkurugenzi) amechimba bonge la mkwala kwa yule atakaye kiuka agizo hilo inawezekana kupewa barua ya onyo kali au kusimamishwa kazi kabisa sasa hapa nina mama mmoja kiukweli ni umri umekwenda sana anasema mwanangu usione hivi naogopa kufukuzwa kazi huyu mtu hana masihala kabisa ngoje nivumilie bwana hao ndo wakubwa hata kama sijapenda kuwa hapa. KUNA HAJA GANI YA MWENGE KAMA KUNA UTUMWA KIASI HIKI. HUUU NDO MWENGE WA UHURU