Utumishi ya Kapteni Mkuchika wa awamu ya tano hii imekuwa mbaya na kisiasa zaidi

Tila-lila2

JF-Expert Member
Oct 20, 2019
653
1,058
Ukweli niliamua kuacha kazi mwishoni mwa Mwaka 2016 na nikaamua kurudi kijijini na nyumbani kwetu Idukilo Shinyanga na kuanza kazi zangu za biashara. Kilichonifanya niache kazi ni kutokana na tu na maamuzi ya kibabe ya watu wenye mamlaka kuamua kibabe kuhusu mambo ya mtumishi wa umma hata kama hajapenda.

Kwa kifupi nilihamishwa kibabe kutoka mkoa ambao tayari nilishawekeza na kutokana na mshahara mdogo wa utumishi wa umma basi kipato changu cha ziada kikawa kinanifanya niishi vizuri.

Hilo likawakera binadamu wenzangu wakanisema vibaya na kuniundia majungu tu hadi nikahamishwa kupelekwa Dar es Salaam

Dar es Salaam yao ikanishinda - pamoja na kushawishiwa sana kwamba mambo yataniendea vizuri nikaona siwezi kumudu nikaacha kazi na kwa umri wangu ulivyo nisingeweza kustaafu kwa hiari.

Naambiwa eti vihela vyangu vya pensheni nisubiri nifikishe miaka 55 - na sasa nimebakiza miaka minne sasa kuifikia hiyo 55 - Mwenyezi Mungu anijalie nisife angalau nivipate hivyo vihela.

Pamoja na kutokuwa kwenye ajira kwa kweli kadri siku zinavyoenda naona watumishi wenzangu waliobaki bado wanaendelea kunyanyasika sana. Kuna mambo kadhaa ambayo yamejitokeza katika awamu hii ambayo yanaonekana kama kuboresha utumishi lakini kumbe yanakandamiza zaidi, nimeorodhesha kwa mtiririko ufuatao:

1. Kwa sasa hivi watumishi wa umma hawafikiriwi kabisa kwenye mambo ya uhamisho - mtu anaomba uhamisho lkn hajibiwi na utumishi wapo kimya tu. Yule ambaye hajaomba uhamisho anahamishwa kibabe - tena anahamishwa bila hata kupewa stahili zake za kiutumishi anaambia atalipwa malimbikizo.

2. Watumishi wengi wameandikiwa barua za kupandishwa vyeo lakini mabadiliko kwenye mishahara yao hayafanyiki. Kinachofanyika sasa ni kuziandika barua hizo kwa tarehe ya mbele ili wasidai malimbikizo - mwenyewe mpaka ninaacha kazi mwishoni wa 2016 sikuwa nimerekebishiwa mshahara pamoja na kuwa nilishapata barua ya kupandishwa cheo kwa miezi zaidi ya 8 nyuma. Nasimuliwa na wenzangu tangu niondoke wamebadilishiwa barua za kupandishwa vyeo mara kibao ili kuzuia wasidai malimbikizo.

3. Hata watumishi ambao wanakaimu nao wanakaimishwa zaidi hata ya miaka miwili bila kulipwa stahiki zao na wanapotolewa kwenye nafasi za kukaimu hawana tena nafasi ya kudai maslahi waliyokaimia.

4. Kwa sasa hata Sheria ya Utumishi inadaiwa imebadilishwa na Katibu Mkuu wa utumishi anaweza kukuhamisha popote pale, kukupunguza cheo au hata kukupandisha tu cheo hata kama hustahili na hawezi kufanywa chochote.

5. Wanasiasa kama kina Mkuchika kwa sasa wanawachukia watumishi wa umma - kumekuwa na mpambano ambao upo indirect, wanasiasa hawaongelei kabisa maslahi ya wafanyakazi katika mtazamo chanya. Juzi Mkuchika kaongelea kuhusu kucheleweshwa kwa mafao ya wastaafu lakini hakuongelea kabisa kuhusu wafanyakazi ambao bado wapo kazini na wana madai kibao.

Hakuongelea kuhusu nyongeza za mishahara, hakuongelea kuhusu manyanyaso ya uhamisho wa kibabe, hakuongelea kuhusu ajira mpya na za wazi ambazo hawataki kuziziba, hakuongelea kuhusu, kuthibitisha wale ambao wanapandishwa vyeo, hakuongelea kuhusu malimbikizo ya madai mbalimbali ya watumishi km malipo ya uhamisho, nyongeza za mishahara, nyongeza za pensheni, nk.

Kwa ujumla wanasiasa na viongozi wa vyama vya wafanyakazi wamekuwa kitu kimoja. Wanawanyanyasa na kuwanyonya watumishi wa umma. Watumishi wa Umma wanawafanyia wanasiasa kazi zao, wanawalipa viongozi wa vyama vya wafanyakazi ada zinazowajaza matumbo yao lakini wanasiasa na viongozi wa vyama vya wafanyakazi wamenyamaza kimywa. Hii sio haki, tena sio haki kabisa.

Kilichobaki kwa wenzangu mlio bado kwenye ajira msimame kidete kuangalia maslahi yenu, wanasiasa na vyama vya wafanyakazi hawana maana kwenu, waondosheni kwa kutumia utaratibu wa kidemokrasia - ondoa wanasiasa kwa kura na ondoa viongozi wa vyama vya wafanyakazi kwa kura. Mtaniona mimi mwoga - sawa mie mwoga lkn mwaka huu hata Chama changu cha Mapinduzi naona sitakipa kura.

Nimeamua hata kama sitagombea lakini nitapigia kura upinzani isipokuwa tu pale mgombea wa CCM mwenye moyo wa dhati kuyaondoa hayo atajitokeza na kwa sura yake nikaamini anaweza kufanya kitu. Tusipofanya uamuzi mzuri kina Mkuchika wataendelea tu na maneno yao yasiyo na msaada wowote.

Asanteni na Mwenyezi Mungu azidi kutuepusha na balaa la #COVID19

Keep distance and please vaa Barakoa.

Its Tila Lila2 me
 
Kila siku watumishi wa umma wamekuwa wa kulialia, huu ni ujinga uliopitiliza! Kila siku kila siku as if hakuna maswala mengine zaidi ya maslahi yao, mbaya zaidi ukienda kuhudumiwa na hao watumishi wa umma ndipo utapochoka kabisa wamejaa viburi dharau za kila aina!
Nasemaje, Magu kanyaga twende wabane hivyo hivyo hadi akiki ziwakae sawa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kila siku watumishi wa umma wamekuwa wa kulialia, huu ni ujinga uliopitiliza! Kila siku kila siku as if hakuna maswala mengine zaidi ya maslahi yao, mbaya zaidi ukienda kuhudumiwa na hao watumishi wa umma ndipo utapochoka kabisa wamejaa viburi dharau za kila aina!
Nasemaje, Magu kanyaga twende wabane hivyo hivyo hadi akiki ziwakae sawa

Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe inawezekana ni kama wale niliokuwa nafanya nao kazi ambao kwa kuwa walikuwa na magodfather ambao wapo kwenye system basi wakahamishiwa Ofisi zinazolipa vizuri kama kule TCRA, EWURA, SSRA TPA, REA, TRA, PSPF, TIRA na BOT. Tunawajua wote hao na ngoja tu muda ufike.
 
Ukweli niliamua kuacha kazi mwishoni mwa Mwaka 2016 na nikaamua kurudi kijijini na nyumbani kwetu Idukilo Shinyanga na kuanza kazi zangu za biashara. Kilichonifanya niache kazi ni kutokana na tu na maamuzi ya kibabe ya watu wenye mamlaka kuamua kibabe kuhusu mambo ya mtumishi wa umma hata kama hajapenda. Kwa kifupi nilihamishwa kibabe kutoka mkoa amba tayari nilishawekeza na kutokana na mshahara mdogo wa utumishi wa umma basi kipato changu cha ziada kikawa kinanifanya niishi vizuri.

Hilo likawakera binadamu wenzangu wakanisema vibaya na kuniundia majungu tu hadi nikahamishwa kupelekwa Dar. Dar yao ikanishinda - pamoja na kushawishiwa sana kwamba mambo yataniendea vizuri nikaona siwezi kumudu nikaacha kazi na kwa umri wangu ulivyo nisingeweza kustaafu kwa hiari. Naambiwa eti vihela vyangu vya pensheni nisubiri nifikishe miaka 55 - halaula nimebakiza miaka minne sasa kuifikia hiyo 55 - Mwenyezi Mungu anijalie nisife angalau nivipate hivyo vihela.

Pamoja na kutokuwa kwenye ajira kwa kweli kadri siku zinavyoenda naona watumishi wenzangu waliobaki bado wanaendelea kunyanyasika sana sana. Kuna mambo kadhaa ambayo yamejitokeza katika awamu hii ambayo yanaonekana kama kuboresha utumishi lakini kumbe yanakandamiza:

1. Kwa sasa hivi watumishi wa umma hawafikiriwi kabisa kwenye mambo ya uhamisho - mtu anaomba uhamisho lkn hajibiwi na utumishi wapo kimya tu. Yule ambaye hajaomba uhamisho anahamishwa kibabe - tena anahamishwa bila hata kupewa stahili zake za kiutumishi anaambia atalipwa malimbikizo.

2. Watumishi wengi wameandikiwa barua za kupandishwa vyeo lakini mabadiliko kwenye mishahara yao hayafanyiki. Kinachofanyika sasa ni kuziandika barua hizo kwa tarehe ya mbele ili wasidai malimbikizo - mwenyewe mpaka ninaacha kazi mwishoni wa 2016 sikuwa nimerekebishiwa mshahara pamoja na kuwa nilishapata barua ya kupandishwa cheo kwa miezi zaidi ya 8 nyuma. Nasimuliwa na wenzangu tangu niondoke wamebadilishiwa barua za kupandishwa vyeo mara kibao ili kuzuia wasidai malimbikizo.

3. Hata watumishi ambao wanakaimu nao wanakaimishwa zaidi hata ya miaka miwili bila kulipwa stahiki zao na wanapotolewa kwenye nafasi za kukaimu hawana tena nafasi ya kudai maslahi waliyokaimia.

4. Kwa sasa hata Sheria ya Utumishi inadaiwa imebadilishwa na Katibu Mkuu wa utumishi anaweza kukuhamisha popote pale, kukupunguza cheo au hata kukupandisha tu cheo hata kama hustahili na hawezi kufanywa chochote.

5. Wanasiasa kama kina Mkuchika kwa sasa wanawachukia watumishi wa umma - kumekuwa na mpambano ambao upo indirect, wanasiasa hawaongelei kabisa maslahi ya wafanyakazi katika mtazamo chanya. Juzi Mkuchika kaongelea kuhusu kucheleweshwa kwa mafao ya wastaafu lakini hakuongelea kabisa kuhusu wafanyakazi ambao bado wapo kazini na wana madai kibao. Hakuongelea kuhusu nyongeza za mishahara, hakuongelea kuhusu manyanyaso ya uhamisho wa kibabe, hakuongelea kuhusu ajira mpya na za wazi ambazo hawataki kuziziba, hakuongelea kuhusu, kuthibitisha wale ambao wanapandishwa vyeo, hakuongelea kuhusu malimbikizo ya madai mbalimbali ya watumishi km malipo ya uhamisho, nyongeza za mishahara, nyongeza za pensheni, nk.

Kwa ujumla wanasiasa na viongozi wa vyama vya wafanyakazi wamekuwa kitu kimoja. Wanawanyanyasa na kuwanyonya watumishi wa umma. Watumishi wa Umma wanawafanyia wanasiasa kazi zao, wanawalipa viongozi wa vyama vya wafanyakazi ada zinazowajaza matumbo yao lakini wanasiasa na viongozi wa vyama vya wafanyakazi wamenyamaza kimywa. Hii sio haki, tena sio haki kabisa.

Kilichobaki kwa wenzangu mlio bado kwenye ajira msimame kidete kuangalia maslahi yenu, wanasiasa na vyama vya wafanyakazi hawana maana kwenu, waondosheni kwa kutumia utaratibu wa kidemokrasia - ondoa wanasiasa kwa kura na ondoa viongozi wa vyama vya wafanyakazi kwa kura. Mtaniona mimi mwoga - sawa mie mwoga lkn mwaka huu hata Chama changu cha Mapinduzi naona sitakipa kura. Nimeamua hata kama sitagombea lakini nitapigia kura upinzani isipokuwa tu pale mgombea wa CCM mwenye moyo wa dhati kuyaondoa hayo atajitokeza na kwa sura yake nikaamini anaweza kufanya kitu. Tusipofanya uamuzi mzuri kina Mkuchika wataendelea tu na maneno yao yasiyo na msaada wowote.

Asanteni na Mwenyezi Mungu azidi kutuepusha na balaa la Cov. 19 - keep distance and pls vaa barakoa.

Its Tila Lila2 me
Kuhusu kupandishwa na mishahara, tatizo ni maafida utumishi, hao ndiyo mchwa na wanastahili kufungwa au kufukuzwa kazi.
 
Hakuna kazi ngumu kama kumtetea Jiwe.
Wanaharibu Dar akina Makonda anawasema tu basi adhabu imetosha, wanaharibu wanasiasa anawatumbua tu basi, watumishi hata wanakuwa hawajaharibu anawatumbua, peleka PCCCB, anawakejeli na maneno mabaya kuntu na anapokutoa wewe anapachika homeboy mwenzetu (hii sio sawa - kwa lafudhi ya Nape wkt akitetea korosho).
 
Na wamegoma kabisa kuwalipa wazee wetu wastaafu. Ingawa Mimi napenda uoto lakini hapa kwa kweli sitoweza kuvumilia.
Hata wasio watumishi wa umma wanaathirika na manyanyaso haya. Wengi wetu ni extended family na mimi nilipoacha kazi nyumbani kwetu ilikuwa kama msiba lkn niliamua kwa dhati na nimeshaizoea hali hiyo na wao wanafurahi tunavyotafuta maisha
 
Mkuchika unamwonea tu, na yeye yupo yupo bora mshahara wake analipwa.

Kiini cha Tatizo ni "Chatu wa Chato"

Mimi nnadhani Hoja ingefungiwa hapa Mkuu ,umegusa mule mule hasa nikiikumbuka ile Kauli ya anatamani Watu waishi kama Mashetani sina hamu kabisa na Jiwe.

Poleni sana Watumishi wa Umma kwa kutumika bila ya kufaidi hata zile Haki zenu za Msingi na za kisheria.
 
Back
Top Bottom