Utumishi wa umma: Sheria hii ni mbovu

Darren2019

JF-Expert Member
Nov 23, 2019
1,112
2,379
Habari zenu wadau,

Nimejitokeza kwenye hili jukwaa kuwasilisha moja miongoni mwa kero zinazopatikana katika utumishi wa umma hasa ualimu. Kuna kipengele cha kwenda likizo ya siku 28 kwa mwaka, wanasema utapewa nauli kwa interval (yaani ukipewa awamu hii, awamu ijayo unajitegemea).

Sasa kero yangu iko wapi? Mtu hadi uambatanishe cheti cha ndoa kinahusu nini? Kwani mimi kuoa hadi niwe na cheti? Mke ambaye sijafunga naye ndoa hana matumizi?

Ok, tufanye hilo tumelipotezea, umeamua kuhesabika kama bachela, eti nauli unayotakiwa kuomba ni ya kwenda nyumbani kwenu ulipozaliwa kama ulivyojaza kwenye mkataba wa ajira, sasa najiuliza hivi na umri huu kweli likizo ni nyumbani tu?

Unaweza usinielewe, hebu chukua mfano wewe ni mwanaume umeajiriwa Mtwara na kwenu ni Mtwara ila una mke kwao ni Mbeya na wewe unapenda Mbeya na mna mpango wa kuishi Mbeya au tayari mna makazi Mbeya na ndiko mke aliko japo wewe kikazi uko Mtwara, hivyo likizo ni lazima ufunge safari ya Mtwara - Mbeya, pesa ya nauli wanakupa ya Mtwara - Mtwara, huu utaratibu uliwekwa kwa malengo gani?
 
Mkuu cheti cha ndoa ni muhimu kama una ndoa. Wengi wetu tunaogopa vitimbwi vya wanawake wawekezaji na kuganawana mali. Lakini ili kukufanya usipate tabu kama hii, basi nenda wilayani kasajili ndoa yako mkuu.
 
Kuna misheria mingi ya ajabu kwenye utumishi,Kila mwaka ukiomba likizo lazima uweke vyeti vya ndoa,kwani mke anabadilika?
 
Mimi naona kupewa nauli kwa ajili ya mapumziko ni matumizi mabovu ya fedha.
 
Ni namna ya kudhibiti matumizi ya fedha!
Ni kanuni kabisa duniani kote kihasibu iko hivyo!
Kila pesa inayotumika lazima iwe na kiambatanisho cha ushahidi wa matumizi!

Kaa wajuvi wakuelezee upate kuelewa!
 
Sasa nikuulize kila atakaesema ana mke yuko mbali bila ushahidi wa cheti cha ndoa nae alipwe nauli bila kuwa na ushahidi wa nyaraka yeyote?

Kienyeji kienyeji tu kirahisi hivyo?

Uko siriasi kweli kwenye hili?
 
Mkuu kuambatanisha cheti cha ndoa kama umeoa au kuolewa ni kuthibitisha maombi yako.

vinginevyo kila mtumishi atadai ana ndoa ili apate nauli mara 2. Vile vile watumishi wangekuwa wanaomba nauli za masafa marefu.
 
Sasa nikuulize kila atakaesema ana mke yuko mbali bila ushahidi wa cheti cha ndoa nae alipwe nauli bila kuwa na ushahidi wa nyaraka yeyote?

Kienyeji kienyeji tu kirahisi hivyo?

Uko siriasi kweli kwenye hili?
Mkuu fikiria vizuri, kwani wanalipa kwa wake wawili? Wanatambua watoto sasa hao watoto hawana mama?
 
Sasa nikuulize kila atakaesema ana mke yuko mbali bila ushahidi wa cheti cha ndoa nae alipwe nauli bila kuwa na ushahidi wa nyaraka yeyote?

Kienyeji kienyeji tu kirahisi hivyo?

Uko siriasi kweli kwenye hili?
Hoja hii hii ingefaa kutumiwa na serikali kwenye makato kama ya BIMA, kuwa mtumishi A hana mke wala mtoto, akatwe asilimia chache kuliko mtumishi B ambaye ana mke na watoto 4 (watumishi wote hao wapo ngazi sawa ya mshahara).
 
Mkuu kuambatanisha cheti cha ndoa kama umeoa au kuolewa ni kuthibitisha maombi yako.

vinginevyo kila mtumishi atadai ana ndoa ili apate nauli mara 2. Vile vile watumishi wangekuwa wanaomba nauli za masafa marefu.
Hizi posho za likizo na uhamisho zilikuwa rahisi sana kupigiwa bajeti pindi unapoajiriwa. Ingependeza kujiwekea mapema kuwa nafasi (slot) zilizopo kwa mwajiriwa ni 5 kwa maana ya mke/mume 1 na watoto 4.

Wakizidi 5 inakuwa ni suala la mtumishi mwenyewe kujua atafanyaje na wakipungua 4 basi inakuwa faida yake mwenyewe.

Hizo ishu za vyeti vya kuzaliwa, umuhimu wake ilikuwa ni kwenye likizo za uzazi tu labda ambapo ingesaidia kwenye upangaji wa kazi (sababu mtu asipokuwepo kazini kunakuwa na upungufu wa wafanyakazi) lakini zisingeathiri kitu upande wa malipo, sababu tayari zingekuwa zimepigiwa bajeti.
 
Habari zenu wadau,

Nimejitokeza kwenye hili jukwaa kuwasilisha moja miongoni mwa kero zinazopatikana katika utumishi wa umma hasa ualimu. Kuna kipengele cha kwenda likizo ya siku 28 kwa mwaka, wanasema utapewa nauli kwa interval (yaani ukipewa awamu hii, awamu ijayo unajitegemea).

Sasa kero yangu iko wapi? Mtu hadi uambatanishe cheti cha ndoa kinahusu nini? Kwani mimi kuoa hadi niwe na cheti? Mke ambaye sijafunga naye ndoa hana matumizi?

Ok, tufanye hilo tumelipotezea, umeamua kuhesabika kama bachela, eti nauli unayotakiwa kuomba ni ya kwenda nyumbani kwenu ulipozaliwa kama ulivyojaza kwenye mkataba wa ajira, sasa najiuliza hivi na umri huu kweli likizo ni nyumbani tu?

Unaweza usinielewe, hebu chukua mfano wewe ni mwanaume umeajiriwa Mtwara na kwenu ni Mtwara ila una mke kwao ni Mbeya na wewe unapenda Mbeya na mna mpango wa kuishi Mbeya au tayari mna makazi Mbeya na ndiko mke aliko japo wewe kikazi uko Mtwara, hivyo likizo ni lazima ufunge safari ya Mtwara - Mbeya, pesa ya nauli wanakupa ya Mtwara - Mtwara, huu utaratibu uliwekwa kwa malengo gani?
1. Likizo unaruhusiwa kwenda kokote utakakako, hata nje ya nchi lakini fedha za nauli utalipwa ya kwenda kwenu ulipoandika kuwa ndio mahali pa makazi yako ya kudumu (walipo wazazi wako). Hata hivyo unaruhusiwa kubadili haya makazi kwa kuboresha (update) taarifa zako

2. Unaruhusiwa kutumia gari binafsi kwenda safari ya likizo, unaweza pewa hela ya mafuta ya kutosha safari yako kwenda na kurudi badala ya kupewa nauli ya basi. Hutakiwi kurejesha chochote (risiti au tiketi) kuthibitisha kuwa ulisafiri

3. Kanuni za utumishi wa umma zipo vizuri tu, sema matatizo ni kwa wanaozisimamia na kuzitafsiri, huwa wanaweka tafsiri ambazo sio na muda mwingine huweka kanuni zao binafsi (kama za kumtaka mtumishi alete tiketi baada ya likizo, au ile ya kumtaka mtumishi aende likizo halafu akirudi ndio alipwe tena akionesha na tiketi za safari).
 
Back
Top Bottom