Utumishi wa umma miongozo yenu inakusudia kujenga au kubomoa?

Inanambo

JF-Expert Member
Jun 26, 2011
3,985
2,770
Mimi ni secretary nimefanya kazi serikalini miaka 20. Kutokana na changa moto za maisha na elimu ya sasa hivi nikatamani nijisomee nipate degree ya kwanza ya marketing. Nimeleta vyeti vyangu kazini wamesema kwa kuwa umebadili kazi moja kwa moja utaanza kwenye hiyo posting ya marketing kwenye entry point. Mshahara niliokuwa nao kama secretary ni mkubwa kuliko wa marketing officer anayeanza. Wakanipa waraka wa katibu mkuu wa december 2009 eti hata mshahara binafsi sitapewa kwa kuwa nimeamua kusoma kitu si fanyii kazi natakiwa kuanza moja kwa kuwa sina uzoefu.
Hoja yangu.utumishi hakuna chuo kinachotoa degree ya secretary, je ningeacha kujiendeleza kwa kuhofu kutopewa mshahara wangu niliokuwa nao? Kazi nataka kufanya hapa hapa ambapo nimekulia miaka 20 na najua nje na ndani ya organization hii. Hii siyo sifa ya kunifanya nisiondolewa mshahara wangu? Nilitaka kusoma hadi nipate phd kwa kuwa nina miaka 13 kabla sijastaafu. Hamuoni mnanikatisha tamaa ya kujiendeleza zaidi. Naona hata nikijiendeleza ni bure utumishi hawathamini kusoma kwangu. Wengine tumeamua kuijendeleza ili tupate sifa za kuwa wanasiasa kama wabunge, marais na hata wakuu wa mikoa. Iko wapi ile dhana ya'internal recruitment' kabla ya external recruitment au masomo tu ili ufaulu mtihani?
 
naona unajutia kusoma kwako sasa!hii ndio tz,akili kumkichwa!pole sana ndugu kwani sina la kusema zaidi
 
ni kweli unataka marketing na wewe experienc yako ni secretary kivp usipewe mshahara wa kuanzia wa marketing? kutokuwa na mwendelezo wa usecretary sio excuse. hata private sector ukihama field lazima uanze na mshahara wa kuanzia kwani ile ni kazi mpya kwako. unataka kusema mfagizi akisona bachelor ya uhasibu alipwe hela sawa na mhasibu wa muda mrefu kazini simply coz na yeye amefanya ufagizi kwa muda mrefu(no disrespect) . tujaribu kuwa fair kwa serikali sometimes.just accept may be itakuwa rahisi kwa promotion yako.
 
Nadhani kuna fairness kwenye huo waraka wa Luhanjo wa December 2009. Lengo ni kulinda wale walioanza miaka mingi iliyopita kwa level hiyo ya Elimu (Degree ya Marketing)
 
Back
Top Bottom