Inanambo
JF-Expert Member
- Jun 26, 2011
- 3,985
- 2,770
Mimi ni secretary nimefanya kazi serikalini miaka 20. Kutokana na changa moto za maisha na elimu ya sasa hivi nikatamani nijisomee nipate degree ya kwanza ya marketing. Nimeleta vyeti vyangu kazini wamesema kwa kuwa umebadili kazi moja kwa moja utaanza kwenye hiyo posting ya marketing kwenye entry point. Mshahara niliokuwa nao kama secretary ni mkubwa kuliko wa marketing officer anayeanza. Wakanipa waraka wa katibu mkuu wa december 2009 eti hata mshahara binafsi sitapewa kwa kuwa nimeamua kusoma kitu si fanyii kazi natakiwa kuanza moja kwa kuwa sina uzoefu.
Hoja yangu.utumishi hakuna chuo kinachotoa degree ya secretary, je ningeacha kujiendeleza kwa kuhofu kutopewa mshahara wangu niliokuwa nao? Kazi nataka kufanya hapa hapa ambapo nimekulia miaka 20 na najua nje na ndani ya organization hii. Hii siyo sifa ya kunifanya nisiondolewa mshahara wangu? Nilitaka kusoma hadi nipate phd kwa kuwa nina miaka 13 kabla sijastaafu. Hamuoni mnanikatisha tamaa ya kujiendeleza zaidi. Naona hata nikijiendeleza ni bure utumishi hawathamini kusoma kwangu. Wengine tumeamua kuijendeleza ili tupate sifa za kuwa wanasiasa kama wabunge, marais na hata wakuu wa mikoa. Iko wapi ile dhana ya'internal recruitment' kabla ya external recruitment au masomo tu ili ufaulu mtihani?
Hoja yangu.utumishi hakuna chuo kinachotoa degree ya secretary, je ningeacha kujiendeleza kwa kuhofu kutopewa mshahara wangu niliokuwa nao? Kazi nataka kufanya hapa hapa ambapo nimekulia miaka 20 na najua nje na ndani ya organization hii. Hii siyo sifa ya kunifanya nisiondolewa mshahara wangu? Nilitaka kusoma hadi nipate phd kwa kuwa nina miaka 13 kabla sijastaafu. Hamuoni mnanikatisha tamaa ya kujiendeleza zaidi. Naona hata nikijiendeleza ni bure utumishi hawathamini kusoma kwangu. Wengine tumeamua kuijendeleza ili tupate sifa za kuwa wanasiasa kama wabunge, marais na hata wakuu wa mikoa. Iko wapi ile dhana ya'internal recruitment' kabla ya external recruitment au masomo tu ili ufaulu mtihani?