Utuezi wa ma-DED wapya, kuna ma-DED hawakuripoti kazini uteuzi wa Julai?

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
48,776
102,138
Habari wakuu wa kazi?
Kuna uteuzi wa wakurugenzi wa Halmashauri 13 umetangazwa jana. Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, uteuzi huo unafanyika kujaza nafasi zilizo wazi.
Ikumbukwe kwamba ni mwezi Julai 2016 tu uteuzi makini wa Rais wetu mpendwa John Joseph Pombe Magufuli aka JPM alifanya uteuzi wa wakurugenzi wapya. Katika utafiti wangu mdogo ni kwamba nafasi zilizojazwa jana zilikuwa na wakurugenzi walioteuliwa Julai 2016 kama jedwali linavyoonesha.


Halmashauri Aliyeteuliwa Julai Aliyetueliwa Sasa

Wilaya ya Bukoba Mwantumu Dau Abdalaaziz Jaad

Wilaya ya Ukerewe Tumaini Sekwa Shija Frank Bahati

Mji wa Mbulu Anna Philip Mbogo Hudson Kamoga

Wilaya ya Nsimbo Joachim Jimmy Nchunda Mwailwa Pangani

Wilaya ya Mkalama Martin Msuha Mtanda Godfrey Sanga

Wilaya Ulanga Audax Christian Rukonge Yusuph Daudi

Wilaya Nachingwea Bakari Mohamed Bakari Bakari Kasinyo

Mji wa Tarime Hidaya Usanga Elias Nturihungwa

Wilaya Kibondo Shelembi Felician Manolo Juma Ally

Wilaya ya Moshi Emalieza Sekwao Butamo Nuru

Wilaya ya Karatu Banda Kamwande Sonoko Waziri Mourice

Wilaya ya Bagamoyo Azimina A. Mbilinyi Fatuma Omari


SWALI: Je, kuna wakurugenzi hawakuripoti kazini? Mwenye taarifa za kina atuletee. Kwa bahati mbaya sana tangazo la Ndg.Msigwa halikusema ni kivipi nafasi hizo zipo wazi pamoja na kuwa uteuzi wa halamashauri hizohizo ulifanyika Julai 2016.

Kumbukumbu zangu zinaonyesha kuwa Mama Azimina Mbilinyi aliyekuwa DED Bagamoyo alitumbuliwa kwa utendaji mbovu mwezi uliopita. Kwa wale wasio na kumbukumbu labda nitumie tukio kuwakumbusha; ilikuwa kile kipindi cha hukumu ya uchaguzi jimbo la Mlimba ''Suzan Kiwanga'' na Kilombero ''Mh.Asenga''. Na Bi.Hidaya aliyekuwa bosi Mji Tarime aliondolewa baada ya kuteuliwa kimakosa.
Naomba msaada, sina ugomvi na mtu
Orodha ya wakurugenzi wa Halmashauri - TBC.go.tz
 
toka dunia iumbwe hii ni mara ya kwanza kwa miaka yote wale wakuu wa idara ndani ya halmashauri ndio wanao kaimu hiyo nafasi mara nyingi iwapo mkurugenzi akiwa njee ya ofisi na hao ndio wanapewa hizo nafasi kuwa ma ded kwa kuwa wanakuwa na uelewa mkubwa na uziefu pia inakuwa ni nafasi nzuri kwao kujisikia bora zaidi kwani wanapanda cheo na inakuwa ni faraja kwa wafanya kazi wengine wafanye kazi kwa kujituma sana sasa kwa mwaka huu mambo tofauti mtu anatoka nje ya halmashauri na kuja chukua nafasi wakati wazoefu wapo hii inashusha sana molari ya kazi
 
yup!!!! miaka mitano itaisha akiwa bado ana jaribu kupandikiza watu wake kila mahala ili 2020 wamsaidie kuiba kura za upinzani. UKAWA mlitizame na hili pia na muandae mkakati madhubuti kulishinda. ikifika 2020 huyu jamaa tumsomeshe namba, walahi atatembelea magoti kuomba kura na hatapata kitu.
 
toka dunia iumbwe hii ni mara ya kwanza kwa miaka yote wale wakuu wa idara ndani ya halmashauri ndio wanao kaimu hiyo nafasi mara nyingi iwapo mkurugenzi akiwa njee ya ofisi na hao ndio wanapewa hizo nafasi kuwa ma ded kwa kuwa wanakuwa na uelewa mkubwa na uziefu pia inakuwa ni nafasi nzuri kwao kujisikia bora zaidi kwani wanapanda cheo na inakuwa ni faraja kwa wafanya kazi wengine wafanye kazi kwa kujituma sana sasa kwa mwaka huu mambo tofauti mtu anatoka nje ya halmashauri na kuja chukua nafasi wakati wazoefu wapo hii inashusha sana molari ya kazi

Labda serikalini hakuna kitu kinachoitwa scheme of service au wameiunganisha na ile ya chama, kama ipo.
 
Habari wakuu wa kazi?
Kuna uteuzi wa wakurugenzi wa Halmashauri 13 umetangazwa jana. Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, uteuzi huo unafanyika kujaza nafasi zilizo wazi.
Ikumbukwe kwamba ni mwezi Julai 2016 tu uteuzi makini wa Rais wetu mpendwa John Joseph Pombe Magufuli aka JPM alifanya uteuzi wa wakurugenzi wapya. Katika utafiti wangu mdogo ni kwamba nafasi zilizojazwa jana zilikuwa na wakurugenzi walioteuliwa Julai 2016 kama jedwali linavyoonesha.


Halmashauri Aliyeteuliwa Julai Aliyetueliwa Sasa

Wilaya ya Bukoba Mwantumu Dau Abdalaaziz Jaad

Wilaya ya Ukerewe Tumaini Sekwa Shija Frank Bahati

Mji wa Mbulu Anna Philip Mbogo Hudson Kamoga

Wilaya ya Nsimbo Joachim Jimmy Nchunda Mwailwa Pangani

Wilaya ya Mkalama Martin Msuha Mtanda Godfrey Sanga

Wilaya Ulanga Audax Christian Rukonge Yusuph Daudi

Wilaya Nachingwea Bakari Mohamed Bakari Bakari Kasinyo

Mji wa Tarime Hidaya Usanga Elias Nturihungwa

Wilaya Kibondo Shelembi Felician Manolo Juma Ally

Wilaya ya Moshi Emalieza Sekwao Butamo Nuru

Wilaya ya Karatu Banda Kamwande Sonoko Waziri Mourice

Wilaya ya Bagamoyo Azimina A. Mbilinyi Fatuma Omari




SWALI: JE, kuna wakurugenzi hawakuripoti kazini? Mwenye taarifa za kina atuletee. Kwa bahati mbaya sana tangazo la Ndg.Msigwa halikusema ni kivipi nafasi hizo zipo wazi pamoja na kuwa uteuzi wa halamashauri hizohizo ulifanyika Julai 2016.

Kumbukumbu zangu zinaonyesha kuwa Mama Azimina Mbilinyi aliyekuwa DED Bagamoyo alitumbuliwa kwa utendaji mbovu mwezi uliopita. Kwa wale wasio na kumbukumbu labda nitumie tukio kuwakumbusha; ilikuwa kile kipindi cha hukumu ya uchaguzi jimbo la Mlimba ''Suzan Kiwanga'' na Kilombero ''Mh.Asenga''. Na Bi.Hidaya aliyekuwa bosi Mji Tarime aliondolewa baada ya kuteuliwa kimakosa.
Naomba msaada, sina ugomvi na mtu
Orodha ya wakurugenzi wa Halmashauri - TBC.go.tz
Waawali hawakwenda mfano mmoja wapo ni huyo wa Moshi hakuripoti kabisa mpaka saizi
 
tatizo kubwa msimu huu wa fiesta kila kitu kinafanywa na nyumba nyeupe mbona vipindi vya nyuma hatujawai koana ded das wakitangaziwa headquarter bali hayo mambo yalikuwa yanafanywa na TAMISEMI
Utetadikti
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom