Utopolo msijisifu saana, wenyewe Simba tunaojua mambo ya ndani tunajua haikutaka kushinda derby ya jana

Utopolo msijisifu saana, wenyewe Simba tunaojua mambo ya ndani tunajua haikutaka kushinda derby ya jana

DELETED ACCOUNT

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
9,805
Reaction score
15,472
Inashangaza sana kuona mtu anakaa kudai eti Yanga imeshinda kwa ubora. Ukweli ni kwamba kuna mambo ya ndani kwa ndani huko Simba yanayopelekea kupigisha timu shoti na hata mgomo baridi wa wachezaji.

Turudi mechi ya nusu fainali dhidi ya Singida. Hivi unahitaji akili kubwa kiasi gani kujua Simba haikutaka kushinda ile mechi? Waliona chaka la uchovu lipo wakaamua kulitumia ila hiyo siyo sababu ya kweli.

Njoo mechi ya mwisho dhidi ya Kagera. Ile mechi ni bahati mbaya tu au kukosa umakini kwa wachezaji wa Kagera ila mipango ilikuwa iishe sare. Hili nalo kwa waliotazama mechi hauhitaji akili kubwa sana kulitambua.

Tuje sakata zima la derby. Ukweli ni kwamba Simba ilikimbia derby ya 08/03. Sababu kubwa ni kuogopa kufungwa kungeharibu morali ya timu katika mashindano ya CAF na Yanga angeweza kutangaza ubingwa mapema sana. Sababu hiyo ikakutana na sababu za kisiasa na pande hizi mbili zilipoungana kila mmoja akimtegemea mwenzake ndiyo kikapelekea kile kilichotokea.

Ukija mechi yenyewe ya jana. Baada ya kushindwa kupata sare katika mechi ya Kagera, jana hauhitaji akili kubwa kujua Simba hakuingia kwa hamu na shauku ya kutafuta ushindi. Tuweke mihemko pembeni, tuangalie kile kilichokuwa kinafanyika uwanjani toka kipindi cha kwanza, sub za Simba zilizofanyika, magoli yaliyofungwa, nk. utagundua mazingira yalitengenezwa na Simba wenyewe wasishinde ile mechi.

Wenyewe wanajua nini kinasababisha haya yote.
 
Inashangaza sana kuona mtu anakaa kudai eti Yanga imeshinda kwa ubora. Ukweli ni kwamba kuna mambo ya ndani kwa ndani huko Simba yanayopelekea kupigisha timu shoti na hata mgomo baridi wa wachezaji.

Turudi mechi ya nusu fainali dhidi ya Singida. Hivi unahitaji akili kubwa kiasi gani kujua Simba haikutaka kushinda ile mechi? Waliona chaka la uchovu lipo wakaamua kulitumia ila hiyo siyo sababu ya kweli.

Njoo mechi ya mwisho dhidi ya Kagera. Ile mechi ni bahati mbaya tu au kukosa umakini kwa wachezaji wa Kagera ila mipango ilikuwa iishe sare. Hili nalo kwa waliotazama mechi hauhitaji akili kubwa sana kulitambua.

Tuje sakata zima la derby. Ukweli ni kwamba Simba ilikimbia derby ya 08/03. Sababu kubwa ni kuogopa kufungwa kungeharibu morali ya timu katika mashindano ya CAF na Yanga angeweza kutangaza ubingwa mapema sana. Sababu hiyo ikakutana na sababu za kisiasa na pande hizi mbili zilipoungana kila mmoja akimtegemea mwenzake ndiyo kikapelekea kile kilichotokea.

Ukija mechi yenyewe ya jana. Baada ya kushindwa kupata sare katika mechi ya Kagera, jana hauhitaji akili kubwa kujua Simba hakuingia kwa hamu na shauku ya kutafuta ushindi. Tuweke mihemko pembeni, tuangalie kile kilichokuwa kinafanyika uwanjani toka kipindi cha kwanza, sub za Simba zilizofanyika, magoli yaliyofungwa, nk. utagundua mazingira yalitengenezwa Simba isishinde ile mechi.

Wenyewe wanajua nini kinasababisha haya yote.
Kwahiyo Simba siyo timu ya mpira??

Maana siku hizi Simba kucheza mpira ni kama mnalazimishwa.
 
Hakuna kipindi kigumu kwa mashabiki wa Simba kama hiki. Timu yao imeonekana kama ilikuwa inaikimbia Yanga ili wasicheze nayo, timu yao imeonekana haina mamlaka wala msimamo, wamefungwa mara tano mtawalia na watani wao wa jadi na wamemaliza msimu bila kombe lolote. Inauma sana
 
Kwa maana hiyo simba hatutaki makombe ?

Ni mpumbavu pekee atasema jana au siku zote simba haitaki kushinda Daby.. tukubali tu kwa sasa Simba hatuna timu ya kucompete navyura wametuzidi uongozi,fitna,quality ya wachezaji na nguu ya ushawishi.
 
Back
Top Bottom