Utitiri wa malori barabarani yanayoendelea kukatisha maisha ya Watanzania

kumusoma

JF-Expert Member
Feb 3, 2014
566
889
Ndugu wana bodi habari ya leo.

Niende kwenye mada. Malori ya mizigo yamekuwa mengi sana barabarani kuliko magari ya aina nyingine. Ukibahatika kusafiri kutoka DSM kwenda Mwanza, malori haya yamejaa. Ukisafiri kwenda Mbeya mpaka Iringa malori haya yamejaa. Ukisafiri kutoka Ruvuma kwenda Lindi au Mtwara malori yamejaa. Yaani utitiri wa haya malori ni mwingi sana.Hata Ukiwa hapa DSM, malori haya ni mengi sana.

AJALI
Ajali za malori haya zimekuwa nyingi sana na mara nyingi tunaambiwa kuwa Lori hilo limefeli breki. Je, hizo breki kila siku zitakuwa zinafeli na kuuwa abiria wasio na hatia? Huu ni uhuni na ugaidi wa kisirisiri unaofanywa na baadhi ya watu. Hata wewe unayesoma hii taarifa yangu siku moja ndugu yako au rafiki yako atagongwa na Lori na tutaambiwa kwa urahisi tu kuwa breki zimefeli. Mama Samia, kama utapata nafasi ya kusoma huu uzi Tafadhali tunaomba uchukue hatua kutusaidia sisi wananchi wako.

MATUKIO YA AJALI
Mwezi Machi Lori kubwa la mizigo liligonga basi la Ahmed lililokuwa linafanya safari za kutoka Tanga kwenda Mbeya na kuua watu 23. Mwezi Machi: Lori la mizigo liliacha njia na kwenda kugonga nyumba iliyo karibu na barabara na kuua watu watatu, Morogoro Mikumi.

Mwezi March mwishoni Profesa wa Mzumbe aliangukiwa na kontena kutoka juu ya Lori na kufariki: Mwezi wa tisa: Mkurugenzi wa Igunga akitoka Mbeya gari yao ilivamiwa na Lori, kwa madai ya kukosa breki.
 
Ndugu wana bodi habari ya leo. Niende kwenye mada. Malori ya mizigo yamekuwa mengi sana BARABARANI kuliko magari ya aina nyingine. Ukibahatika kusafiri kutoka Dsm kwenda Mwanza, malori haya yamejaa. Ukisafiri kwenda Mbeya mpaka Iringa wezi wa tisa:Mkurugenz wa Igunga akitoka Mbeya gari yao ilivamiwa na Lori ,kwa madai ya kukosa breki.
Wewe una maoni gani tubebe mizigo kichwani au tutumie punda ili tuepukane na malori?
 
Ndugu wana bodi habari ya leo.

Niende kwenye mada. Malori ya mizigo yamekuwa mengi sana barabarani kuliko magari ya aina nyingine. Ukibahatika kusafiri kutoka Dsm kwenda Mwanza, malori haya yamejaa. Ukisafiri kwenda Mbeya mpaka Iringa malori haya yamejaa.

Huyo mkurugenzi mtoe kwenye hesabu
 
Kama nchi tumeshindwa kuangalia faida ya kutumia reli kama njia rahisi na ya uhakika kwa nchi, uwezo wa kubeba mzigo mkubwa kwa wakati mmoja

Pia wanasiasa ndio haohao wamiliki wa malori unatemea nini
 
Wewe una maoni gani tubebe mizigo kichwani au tutumie punda ili tuepukane na malori?
Serikali ingeimarisha usafirishaji wa mizigo kwa njia ya treni, ili kupunguza utitiri wa haya malori barabarani.

Changamoto ipo kwenye utekelezaji wake! Maana wamiliki wengi wa hayo malori ni Wanasiasa na wafanyabiashara wakubwa; wakiwemo wabunge, nk. Hivyo wataweka tu nongwa ili hilo zoezi lisifanikiwe
 
Back
Top Bottom