Uteuzi wakurugenzi: Rais hakufuata sheria ya utumishi wa umma?

Sheria ya nini? Sisi tunataka kazi tu. Halo ya sheria ni ya Kwenu. Kwani kuna sheria kubwa kuliko Katiba? Mbona nayo hatuiogopi? Hapa ni kazi tu!
 
Nivyema nafasi za wakurugenzi wapewe wenye taaluma sio makada wa vyama

Kiukweli, Nilimuona Mh. raisi Magufuli akiwa kioo pia mfano kwa hawa maraisi wanaotuzunguka pia wanaofutalia kinachojiri katika nchi yetu ya Tanzania ila kwa haya washauri wake wanamissLEAD kabisa, ukurugenzi ni taaluma na si ushabiki kama hasa lengo linavyodhaniwa na washauri wake mkuu.

mwendelezo wa haya ni pamoja na kuwa uDED watu wenye qualifications kama za Hotel attendant n.k. Nakuomba Mh. Raisi Tangaza hizi kazi na uwachague watu makini katika interview ili watu wenye sifa waweze kuwa na tija pia wapate nafasi za kulisaidia taifa hili chonde chonde Mh. Magufuli.

Mwisho nimesikitika kuziona picha za DED wa SAME, natumaini mtaziona na mtasikitika kama mimi na real kama Mh. hakumpiga chini nitasikitika sana, na haya ni matokeo ya washauri wake ambao real wanamissLEAD mheshimiwa.
Mheshimiwa raisi waepuke mashabiki wanaokupa ushauri wa kishabiki ili Tanzania isonge mbele O.W sisi wabongo bado sana au we are here to stay.
Ni Ushauri tu jamani
 
Uteuzi wa wakurugenzi wa halmashauri za majiji, wilaya, manispaa, miji unekuwa na tafrani miongoni mwa wananchi hususan kwenye mitandao kila mtu akieleza lake, kama ni makada, ni watumishi, hawana sifa, kuna upendeleo kuna ubaguzi n.k

Hivyo ni vema tukaliweka wazi kwani hawa wanaoteuliwa ni watumishi wa umma daima watatumikia umma mpaka watakapofika mwisho wa mkataba wao na sio kutenguliwa katka teuzi hizi, malalamiko hayo yanatakiwa kuzingatia yanajibu sheria ya utumishi wa umma ya 2002 na marekebisho yake ya 2009
Na sheria ya masuala ya kiutumishi ya mwaka 2007 kwani tunategemea raisi aliteua hawa MADAS NA WAKURUGENZI kwa kufuata sheria hizo kama sio yeye basi wizara ya utumishi kama walifanya kwa shinikizo bila kufuata sheria tujue.

Kama ni ajira mpya haziwezi kuanza na watu wenye vyeo vikubwa na inavyojulikana hizi sio nafasi za kuomba ni promotion hivyo ni zawadi kwa watumishi watendaji wanaotumikia wananchi kulingana na maadili ya kazi pia wenye weledi wa kutosha na wachocheaji wa maendeleo hivyo daima wanatakiwa kuwa huru kulingana na imani na dini zao.

Naomba sasa tuweke sawa juu ya uteuzi huu je umefuata sheria hizo za utumishi wa umma pia mifano.
Lakini unazijua sheria za utumishi wa Umma na mamlaka ya Rais kwa kila teuzi? Kama hujui utajuaje watakao kwambia kama wana kudanganya au lah?
 
Mie mashaka yangu yako kwa huyu Katibu mkuu kiongozi. Kwa mujibu wa sheria za kazi yeye ndiye mkuu wa utumishi serikalini, lakini kama haya yanatokea naye hamshauri ipasavyo bosi wake basi hatufai.
Lazima hapa jukwaani wapo watu wanamfahamu Kijazi na wamewahi kufanya nae kazi. Hebu watupatie uelewa wao kuhusu huyu mtu
 
M
Kama umeangalia kwa undani mfumo uliopo wa sheria na taratibu unachelewesha kasi ya Rais Magufuli.Alishasema yeye sio mtu wa kungojea michakato. Hivyo wakati mwingine inabidi azipinde sheria.. Suluhisho hapa ni Katiba Mpya tu..
Mbona hii ya sasa imekiukwa hiyo mpya itasalia sasa!
 
Sheria inaelekeza kwamba nafasi za uongozi katika utumishi wa umma zinatakiwa kujazwa kwa kupandishwa vyeo watumishi wa umma waandamizi wenye utendaji mzuri wa kazi pamoja na elimu inayostahili
Kuajiriwa kwa watu wenye sifa hizo je? Kama mtu alikua private sector anazo sifa hatakiwi kuajiriwa?
 
MTEMI umeongea kwa uchungu sana. Lakini sheria zipo ili kutulinda na kutuongoza. Kama zina mapungufu, zimepitwa na wakati au hazifai kuna njia ya kuzipinga, mahakamani, kuzirekebisha au kuzifuta, bungeni. Sheria yo yote inabana uhuru binafsi. Kama kila aionaye sheria haifai akaiasi, matokeo yake ni fujo.
 
Nijuavyo mimi mkuu wa nchi huwajibika kwa wananchi kupitia katiba yao bila kujali ubora au udhaifu wake na kwayo aliipia kuilinda kwa nguvu na mamlaka aliyokasimishwa kwa katiba hiyo.
Kwa mwenendo wa hizi teuzi inaonyesha pasi na shaka kuwa anawaweka watu wake wa karibu. Ile miongozo iliyopo ya utumishi wa umma imetupwa. Kwa maana nyingine katiba imesiginwa kwa kisingizio cha sheria hizo kupitwa na wakati. Najiuliza, inakuwaje sisi tuendelee kuzitii sheria mbovu na raia namba moja azidharau? Suluhisho hapa ni moja, katiba mpya.
Na wanasheria mnakaa kimya mkimaanisha kuunga mkono katiba kuvunjwa au mna maslahi katika hili? Hebu igeni mazuri ya wanasheria wa Kenya. Pale kosa linapofanyika wenzenu huenda mahakamani kutaka tafsiri na ikibidi kuzuia. Hebu badilisheni utendaji wenu vinginevyo hamuwasaidii wananchi na mnakosa uzalendo.
 
Rais upo sahihi kabisa kufanya uteuz wa wakurugenzi. Hao wataweza tu. Kwani kwenye ukurugenzi kuna kuandika dissertation?
 
Kama umeangalia kwa undani mfumo uliopo wa sheria na taratibu unachelewesha kasi ya Rais Magufuli.Alishasema yeye sio mtu wa kungojea michakato. Hivyo wakati mwingine inabidi azipinde sheria.. Suluhisho hapa ni Katiba Mpya tu..
akizipindisha wananchi nao wazifanyeje ?
maana inapotokea anazipindisha ili kuwanufaisha makada wenzake..
kudadedek, kuna watu tangu wazaliwe maisha yao yanategemea CCM kuwepo madarakani..
 
Kuajiriwa kwa watu wenye sifa hizo je? Kama mtu alikua private sector anazo sifa hatakiwi kuajiriwa?
Elikuwaga hivyo, sheria ikabadilishwa kwa a sasa nafasi hizo zinatakiwa kujazwa na watumishi wa umma tu, haruhusiwi mtu kutoka nje ya utumishi.
Sijui tunakwenda wapi, na nakuakikishia watumishi hao wapo, hao wanasiasa wamechomekwa kimakosa
 
Kama umeangalia kwa undani mfumo uliopo wa sheria na taratibu unachelewesha kasi ya Rais Magufuli.Alishasema yeye sio mtu wa kungojea michakato. Hivyo wakati mwingine inabidi azipinde sheria.. Suluhisho hapa ni Katiba Mpya tu..
Nini umuhimu wa kuwa na sheria.

Umesahau ule msemo wa wazir mkuu pinda kuwa nchi inaongoza kwa kanuni na taratibu za kisheria ukifanya fujo lazma upigwe.
 
Mtemi umeongea kwa dhati ya moyo wako. you have expressed your true heartfeelings bila kuona aibu. safi sana.
 
mkifanya mikutano tunawasweka ndani,magamba tu ndo yanaruhusiwa kufanya mikutano....utumishi wa umma unaelekea kuwa tawi la lumumba,hii ni mpya!!!!
 
Kama umeangalia kwa undani mfumo uliopo wa sheria na taratibu unachelewesha kasi ya Rais Magufuli.Alishasema yeye sio mtu wa kungojea michakato. Hivyo wakati mwingine inabidi azipinde sheria.. Suluhisho hapa ni Katiba Mpya tu..
Utashi ndiyo suluhisho sio katiba mpya! Kwani katiba ya sasa inaruhusu haya!
 
hajafuata kabisa.anyway who care?ccm haiwezi kamwe kuleta maendeleo katika nchi hii.na Magufuli ndo rais wa ajabu kuwahi tokea tanzania na africa kwa ujumla.subiri tuone
CCM haiwezi kuleta maendeleo ? Nchi hii ilikuwa hivi miaka 30 iliyopita ? Halafu eti nchi hii tuwakabidhi watu wapumbavu kama wewe. Haitatokea hadi dunia hii inakwisha
 
Kimsingi taratibu ndio hazikufuatwa.
Taratibu zinaelekeza kwamba ili kuteuliwa kuwa mkurugenzi wa halmashauri ni lazima muhusika awe ameshafanya kazi serikalini kwa zaidi ya miaka 12 na pia lazima awe ameshakuwa mtumishi mwandamizi hususani mkuu wa idara pamoja na elimu ya shahada ya uzamili.
Kwa ma days ni lazima awe na uzoefu wa zaidi ya miaka 12 na kuwa mtumishi mwandamizi (afisa utumishi au utawala) wizarani, mkoani ndio wengi walikuwa wanatolewa au kwenye halmashauri.
Nafasi hizo ziliondolewa kujazwa kwa watu kutoka nje ya utumishi wa umma, mabadiliko ya sheria ya utumishi wa umma yalifanyika na kufanya nafasi hizo kuwa za promotion kwa watumishi wa umma wanye utendaji mzuri.
Kitendo cha kuwaibua makada wa ccm ambao hawajawahi kamwe kufanya kazi serikalini ni kosa kwa mujibu wa sheria ya utumishi wa umma. Na pia inawashusha mori watumishi wa umma ambao ndio walikuwa na sifa za kupewa nafasi hizo.
Namalizia kwa kusema kilichofanyika ni upuuzi na ushenzi uliopita mipaka.
Huu ni wakati wa kuvunja, kuharibu na kubomoa uozo wote kisha kujenga nchi mpya. Keep it up JPM.
 
Back
Top Bottom