Uchaguzi 2020 Uteuzi wa Wagombea Ubunge CCM ni tishio na funzo kubwa kwa Upinzani

Mati Mkenda

Senior Member
Mar 4, 2018
171
211
Siku ya Jana CCM ilitangaza majina ya Watu watakaopeperusha bendera ya chama hicho katika nafasi ya ubunge kwenye majimbo yote, Bara na Visiwani, katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 28 mwaka huu. Uteuzi huo unaweza kutazamwa kwa sura mbili, yaani sura ya kwanza kuwa ni tishio na ile pili kuwa ni funzo kubwa kwa vyama vya upinzani hapa nchini.

Tishio: Vyama vya upinzani almost vyote, tayari vilikuwa vimeshatangaza majina ya watu ambao watapeperusha bendera za vyama vyao katika baadhi ya majimbo. Walifanya “Professional Guess” zao za kukadiria uwezo wa wapinzani wao, hasa kutoka chama tawala, wakaja na majina ya wale walioona kuwa wana uwezo wa kushindana na washindani wao hao. Kitendo cha CCM kuja na sura nyingi mpya kinaweza kuwa ni tishio kubwa sana kwa upinzani kwani kuna wagombea wapya wengi ambao hata upinzani hawakutajia kama wangepitishwa na chama hicho.

Hivyo hata kama watarudi kwenye “Drawing Board” na kuanza kujadili sura mpya hizo haitasaidia kwani kuwaondoa wagombea wao waliopitishwa ambao wanaweza kuwa na udhaifu fulani kiasi cha kutoa nafasi kwa CCM kushinda, kunaweza kuleta mpasuko mkubwa ndani ya vyama vyao. Hivyo upo uwezekano CCM wakawa wamecheza na loophole hiyo, kwa kuwaleta wagombea wenye ushawishi mkubwa kuzidi ule wa wapinzani wao.

Funzo: CCM imeteua wagombea kwenye majimbo yote, kitendo ambacho hakijawezekana kwa vyama vya upinzani. Hii inaonyesha kuwa CCM ina hazina kubwa ya wanachama waliojengeka kiuongozi. Kitendo cha sura tulizozizoea ndani ya CCM kuwekwa pembeni tunaweza sema chama kimefanya kitu kinachoitwa “Breaking the status quo”, hali ambayo hata wapinzani hawakutegemea kama ingetokea.

Hali hiyo imetoa funzo kuwa bila fulani na fulani, bado chama kinaweza kusimama na kusonga mbele. Ni wakati sasa wa upinzani kuiga mfano huo mzuri wa CCM kwa kuandaa hazina ya viongozi, ili kuweza kuwa na uwezo wa kusimamisha wagombea katika majimbo yote, ambao wana uwezo mkubwa wa kushawishi na si mar azote kuwaleta watu wale wale ambao kila kukicha wanadidimiza maendeleo ya vyama hivyo. Lazima vyama vihame kutoka kumilikiwa na watu wachache hadi kumilikiwa na umma.
 
Ni kweli kaka:

TISHIO:

1. Wamewatisha na kuwaondoa wale woote wasiounga mkono "zidumu fikra za Mwenyekiti hata kama hazikisaidii chama". TISHIO
2. Watoto wa viongozi wastaafu na wake zao wameendelea kupewa vyeo hivyo kujenga umwinyi - TISHIO
3. Wanaounga juhudi za Mwenyekiti wakitokea upinzani ni muhimu kuliko wanachama kindakindaki CCM wanaokifahamu na kukipenda chama kwa dhati-TISHIO
4. Maendelezo ya chuki dhdi ya wanaCCM wakongwe waliopishana au kumpiga Mwenyekiti kipindi kabla hajawa Mwenyekiti wa chama (Kapuya na wengine) -TISHIO
5. Mapendekezo ya Wajumbe kura za Maoni hayana umuhimu tena kinachozingatiwa ni jinsi gani Mwenyekiti ameamkaje siku ya kupitisha majina-TISHIO


FUNZO

1. Siku zoote wanachama tusiamini kauli za viogozi wetu.kwa mfano ile misemo ya serikali haina chama au viongozi lazima mlizike na nafasi zenu za uteuzi. -Funzo
2. Wajumbe kura za maoni hawana umuhimu hata kidogo kama hujamfurahisha Mwenyekiti jinsi atakavyo hata ukiongoza kura za maoni wewe ni fala tu -FUNZO
3. Ukiunga juhudi mkono kwa kutokea upinzani kwa njia yoyote ile wewe una uhakika wa kupata nafasi ya kogombea ubunge CCM -FUNZO
4. Ukiwa Mtoto wa kiongozi mstaafu.Ubunge ni guaraateed- FUNZO


Tusibiri tuoe matokea ya kura za ubunge arafu ndio uje na andiko lako hili tena tujadili
 
Mleta mada kujifanya kujua kwingiiiii, na kuweka mawazo ya kijinga. Upinzani walikuwa na mchakato wao baada ya kuwa CCM walifanya wao na washindi kujulikana.

Ulipaswa kusema kuwa CCM wameondoa washindi kadhaa na kuweka wengine kadhaa walioshindwa kura ya maoni. Actually ulipaswa kusema kuwa CCM ndio imeogopa upinzani na kufanya maamuzi waliyoyafanya. Sijui hata mtu mwenye akili anawezaje kusema upinzani ndio uliogopa CCM na bado mchakato wao ulikuwa wa kwanza mpaka kuchukua form za kugombea NEC!!

Dogo unakwama wapi?
 
Mleta mada kujifanya kujua kwingiiiii, na kuweka mawazo ya kijinga. Upinzani walikuwa na mchakato wao baada ya kuwa CCM walifanya wao na washindi kujulikana.

Ulipaswa kusema kuwa CCM wameondoa washindi kadhaa na kuweka wengine kadhaa walioshindwa kura ya maoni. Actually ulipaswa kusema kuwa CCM ndio imeogopa upinzani na kufanya maamuzi waliyoyafanya. Sijui hata mtu mwenye akili anawezaje kusema upinzani ndio uliogopa CCM na bado mchakato wao ulikuwa wa kwanza mpaka kuchukua form za kugombea NEC!!

Dogo unakwama wapi?

CCM walieleza bayana mchakato utakavyokuwa. Not only once, mwenyekiti alisema kushinda kura za maoni doesn't mean ndo kuteuliwa. Sema wewe ulijiaminisha tu kichwani mwako.
 
Mleta mada kujifanya kujua kwingiiiii, na kuweka mawazo ya kijinga. Upinzani walikuwa na mchakato wao baada ya kuwa CCM walifanya wao na washindi kujulikana.

Ulipaswa kusema kuwa CCM wameondoa washindi kadhaa na kuweka wengine kadhaa walioshindwa kura ya maoni. Actually ulipaswa kusema kuwa CCM ndio imeogopa upinzani na kufanya maamuzi waliyoyafanya. Sijui hata mtu mwenye akili anawezaje kusema upinzani ndio uliogopa CCM na bado mchakato wao ulikuwa wa kwanza mpaka kuchukua form za kugombea NEC!!

Dogo unakwama wapi?
Ccm walichelewa kutoa majina kwa kuogopa wapinzani, alafu huyo pimbi analeta bla blah
 
Mleta mada kujifanya kujua kwingiiiii, na kuweka mawazo ya kijinga. Upinzani walikuwa na mchakato wao baada ya kuwa CCM walifanya wao na washindi kujulikana.

Ulipaswa kusema kuwa CCM wameondoa washindi kadhaa na kuweka wengine kadhaa walioshindwa kura ya maoni. Actually ulipaswa kusema kuwa CCM ndio imeogopa upinzani na kufanya maamuzi waliyoyafanya. Sijui hata mtu mwenye akili anawezaje kusema upinzani ndio uliogopa CCM na bado mchakato wao ulikuwa wa kwanza mpaka kuchukua form za kugombea NEC!!

Dogo unakwama wapi?
Ccm walichelewa kutoa majina kwa kuogopa wapinzani, alafu huyo pimbi analeta bla blah
 
Ni mtazamo tu mjomba, tumekusoma ! Ila utambue tu ulichoandika ni utopolo tu kwa watu wengine
 
CCM walieleza bayana mchakato utakavyokuwa. Not only once, mwenyekiti alisema kushinda kura za maoni doesn't mean ndo kuteuliwa. Sema wewe ulijiaminisha tu kichwani mwako.

Mie sio hata mwanasiasa, ninajaribu kutumia logic hapa. Umeshasikia sehemu nyingi hapa duniani ambazo zinatumia primaries zikafanya hiki kilichofanywa na CCM. Ni au mchakato uwe ngazi ya chini au ubaki makao kamati kuu. Na jambo zuri ingekuwa ni kumwondoa mshindi na kuitisha primary mpya. Unapofikia kumuacha hata wa pili ukachukua wa tatu - iko shida.
 
Back
Top Bottom