Uteuzi wa Nehemia Mchechu: Tunamchekea Rais Samia, lakini hapa ameonyesha udhaifu mkubwa

Ebu niambie mbali na Dar kulikojengwa maghorofa ya mchongo kwa matajiri tu, achana na yale yaliyojengwa Magomeni enzi ya Magufuli. Ni mkoa gani mwingine ulionufaika na ujenzi wa majengo ya kisasa? Ni wapi wananchi wa kawaida walinufaika na NHC chini ya uongozi wa Nehemia?

Sitaki kuongelea mamilioni ya fedha aliyokuwa anajilipa, na mashule alojenga, majumba anayomiliki, ambayo kabla ya kuwa meneja hakuwa navyo. Sitaki kuongelea alivyokuwa anamwaga fedha mamillioni. Ilikuwa bahati yake. Sitaki kuwa na wivu nae.
Mie nakumbuka NHC ya zamani ilijenga nyumba Tanzania nzima. Tena wengi waliofaidika ni watu wa chini. Mashirika kama haya nchi nyingine yamekuwa na REAL ESTATES kubwa na kuendezesha miji.

Siyo miaka ya Nehemia na vile vigorofa vya Morocco, basi tukaona amefanya kazi, na kuwa na kipindi. Nimetembelea Ethiopia, shirika la nyumba, limejenga majengo ya ghorofa nchi zima na nimazuri. Na bei nafuu sana nyumba zao. nchi inajengeka utazani Singapore.
NHC haijapata mtu alonavision ya kuwasaidia watanzania. NHC ilitakiwa ibadili madhari ya miji mingi Tanzania, si kuishia Dar es Salaam kujenga vigorofa viwili wanatumia hela nyingi kupoteza muda ati kipindi cha Nyumba! Ha ha ha!

Nehemia, hana tena jipya, kama miaka alotumia, hakufanya cha maana anaporejeshwa sasa atafanya nini? Kikubwa ni madili kujenga maghorofa machache Dar na kuwapa alionao michongo, wamiliki, nao wapangishe kwa matajiri.

Mfano pale mwanza milimani, Dar es Salaam maeneo ya Manzese, Mburahati na kadhalika, haya ni maeneo ambayo NHC ingeingia ubia na wananchi na kujenga majumba au maghorofa ya makazi, kisha wananchi hawa kupangishwa na baadae kuuziwa.

Hata vijijini, NHC ingekuwa na maono kusaidia wananchi wa vijijini kuwajengea makazi bora kwa makubaliano maalum, na kuondoa vijumba vya ajabu na vile vya nyasi. Nampongeza Rais wa kwanza wa Zanzibar Abeid Karume, alikuwa na akili sana huyu, vijijini au shamba kama wanavyoita wa Zanzibar alijenga maghorofa akaweka umeme na maji, mbali na yale maghorofa ya Michenzani, naongelea ya vijijini kama Bambi na kadhalika. Alitaka wananchi wa hali ya nchini wapate makazi safi. Hadi leo hakuna Rais alofanya kazi kama ya Marehemu Karume.

Nehemia hana jipya tena. Hivi nchi yetu haina watu wengine? Hivi hawa ndo tu walio na brain kuliko watanzania wengine? Mie nadhani Nehemia angepewa nafasi nyingine za uteuzi lakini si kumrudisha palepale ambapo kwa kuangalia hakuwa na perfomance nzuri kulinganisha na maono ya NHC.

Ni kiitazama Tanzania naona imesimama, naona hakuna maono yoyote, ipo ili mradi tu iende na tujue kuna Taifa la Tanzania. Siku hizi tunavijana wengi, wanaujuzi katika masuala ya Real estates na niwabunifu. Serikali inawaweka pembeni, inampa mtu aendelee kuwa katika shirika hadi atafikisha miaka 20 ktk shirika, lkn hakuna jipya zaidi ya upigaji na kutumia mamillioni ya fedha kujitangaza.
Huyo ambaye mlimweka alifanya nini zaidi kurudisha nhic nyuma zaidi...watu wanayoijua nhic ilipokuwa kabla ya Msechu na alipoifikisha Msechu hawawezi kamwe kubeza kazi nzuri aliyoifanya..mnyonge mnyongeni haki yake mpeni..na Msechu kilichomtoa nhic si kingine ni wapika majungu waliokuwa na interest binafsi..na mzee baba akaingia king
 
Nijibu swali hili: Je, Mchechu alifunguliwa mashtaka ya Ubadhilifu wa mali/pesa za umma?
Kama hajafunguliwa basi wewe ni maiti na ndondocha nambari 1, maana uliiona Ubadhilifu wa mali za umma ukifanyika na ulikaa kimya hukwenda mahakamani wala kwenda polisi kutoa taarifa.
Una haki kama mwananchi kuzilinda mali za umma kwa namna yoyote na si kuja kulalamika mitandaoni
Magufuli aliyajua madhambi ya Mchechu lakini akamuogopa Kikwete. Angemgusa Mchechu kwa namna moja ama nyingine angekuwa anamgusa JK, ikabidi amuondoe tu kwenye kile cheo.
 
Ni aibu kwamba nchi ambayo tuliaminishwa kwamba watu fulani ni wezi ni watendaji wabovu sasa wanarudishwa kwenye nafasi zao, utadhani hakuna kilichofanyika.

Yawezekana kweli walionewa, lakini iweje Rais wa nchi awarudishe kwenye nafasi zile zile bila maelezo kwa wananchi? Hii haina maana.

Mchechu alisifika sana kwa ubadhirifu, sasa anarudi NHC kwa nafasi ile ile. Huu ni uongozi au uhuni uliokithiri? Je, haya ndo matokeo ya urafiki na Kikwete au ni sababu gani ya ziada?

Rais Samia na Mzee Kikwete au watu wa Kikwete wana urafiki gani wa ziada? Hawa watu wana sifa zipi ambazo Watanzania wengine hawana? Yaani wananchi hatuna thamani kiasi hiki kwa viongozi wetu!
Tatizo hutaji huo "ubadhirifu" wa Mchechu,

Hebu punguza povu kidogo fafanua kuhusu ubadhirifu wa Mchechu😀
 
Ninavyojua hawa wapigaji walikuwa na network, sasa ni kama Magufuli alikuja kukata ile network ila amekuja huyu naona anaunganisha tena network.

Niandike tu kwa kifupi; Katiba Mpya (Rasimu ya Warioba) ndio suluhisho la kudumu.
Magufuli aliondoa network ya Kikwete akiweka ya kwake
 
Tuache kukurupuka mamlaka za uteuzi kabla kufanya maamuzi lazima wapitie mafaili hawaji na majina yao mfukoni lazima kamati ya vetting impelekee taarifa kamili ya muhusika ndio aamue. kama alikuwa na makando kando huyu asigerudi.
 
Mchechu hakuwa na tatizo lolote katika uendeshaji wa NHC uenda alikataa kuhamishia miradi mikubwa ya NHC kuleeee jamaa akamtimua.
 
Tatizo hutaji huo "ubadhirifu" wa Mchechu,

Hebu punguza povu kidogo fafanua kuhusu ubadhirifu wa Mchechu😀
Ingia JF, fanya reference. Kama huwezi kufanya literature review unataka nani ahangaike kueleza mara nyingine tena. Hiyo ni hadithi ambayo iko JF kwa miaka mingi na kwa anayejua kusoma na kuandika unachouliza ni uzembe mkubwa.
 
Hela za kampeni 2025 jombaa! Ukute JPM naye mrija wake ulikuwa Tanroads na kule kwenye matanzanite na magold. Mkandarasi yeyote aliyekataa kupeleka mgao kupitia kwa Mfugale aliona cha mtema kuni. Eng. Lema Wa Elerai construction hatakaa asahau🤣
Lema ni mkandarasi siyo Eng.
 
Ninavyojua hawa wapigaji walikuwa na network, sasa ni kama Magufuli alikuja kukata ile network ila amekuja huyu naona anaunganisha tena network.

Niandike tu kwa kifupi; Katiba Mpya (Rasimu ya Warioba) ndio suluhisho la kudumu.
Rasimu ya Warioba bado ina mapungufu, inasema Rais akishindwa kuendelea na Urais kwa sababu yoyote ile basi Makamu wa Rais atakuwa Rais Kwa kipindi kilichobaki,

Hii haiko Sawa,
Ilipaswa iwe kama muhula wake umebaki Kwa chini ya miezi 12 basi Makamu achukue nafasi yake Kwa kipindi kilichobaki mpaka uchaguzi, Ila zaidi ya hapo ndani ya siku 90 hasa siku ya 90 uitishwe uchaguzi mkuu kum-replace marehemu. Siyo hii ya sasa. Haitoi fursa ya awamu kuzaliwa!
 
Hivi hizi hasira tutazimalizia wapi na lini maana tunataka kupasuka kwa ukuda unaofanyika kuna hii ishu ya mgao Nani ana taarifa??
 
Ingia JF, fanya reference. Kama huwezi kufanya literature review unataka nani ahangaike kueleza mara nyingine tena. Hiyo ni hadithi ambayo iko JF kwa miaka mingi na kwa anayejua kusoma na kuandika unachouliza ni uzembe mkubwa.

Umejibu vizuri sana Mkuu!
 
...........haongozwi na chuki.
NImemkumbuka Ndugai!
Ndugai aliyewaapisha COVID 19 kwenye garage na kutusababishia bunge la hovyo katika historia ya Tanzania, kuna mtu kweli bado ana dadisi alitokaje?
 
Back
Top Bottom