Uteuzi wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali 2010

Maxence Melo

JF Founder
Feb 10, 2006
4,086
12,277
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Jaji Frederick Mwita Werema kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuanzia leo, Jumamosi, Novemba 6, 2010.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Mheshimiwa Phillemon Luhanjo inasema kuwa Jaji Werema ataapishwa saa 11 jioni leo katika shughuli itakayofanyika Ikulu.

Kabla ya uteuzi wake, Jaji Werema alikuwa anashikilia nafasi hiyo hiyo ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Hivyo, anaendelea na wadhifa huo.

Rais Kikwete amefanya uteuzi huo saa chache baada ya kuwa ameapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kipindi cha pili cha miaka mitano katika sherehe iliyofanyika Uwanja wa Uhuru mjini Dar es Saalam.

Imetolewa na
:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM
.


06 Novemba, 2010
 

We can

JF-Expert Member
Sep 4, 2010
678
46
Ok, happy to him. He has to be fair and protect out Constitution in no ones benefit but the PUBLIC...
 

Jamco_Za

JF-Expert Member
Jul 14, 2007
1,330
193
Serikali yaanza kuundwa sasa, tunasubiri mawaziri. Hivi watatoka wapi? Let wait and see
 

Mfamaji

JF-Expert Member
Nov 6, 2007
6,632
1,913
majaji kama MAKAMAE wAMEPOTEZA CREDIDIBILTY YAO TULIYOWAPA HADI UZEE HUU KWA KUWANYIMA RAIA HAKI ZAO ZA KUCHAGUA WAMPENDAO
 

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
14,423
12,861
Hehe hivi rais anapomaliza urais wake anakuwa pia ana-afect ajira za wateule wake wote? I mean wakuu wa wilaya, mikoa, AG na kadhalika?

Au werema aliapishwa kwa mkataba mfupi? Ina maana na jaji mkuu mpya ataapishwa punde?
 

faithful

JF-Expert Member
Aug 10, 2010
378
32
Hehe hivi rais anapomaliza urais wake anakuwa pia ana-afect ajira za wateule wake wote? I mean wakuu wa wilaya, mikoa, AG na kadhalika?

Au werema aliapishwa kwa mkataba mfupi? Ina maana na jaji mkuu mpya ataapishwa punde?

jibu ni ukweli anaunda serikali mpya mwanasheria mpya,waziri mkuu mpya....anashirikiana na waziri mkuu kuteua mawaziri wapya na wakuu wa mikoa wapya mwisho kabisa anamalizia na wakuu wa wilaya!si ajabu kukutana na sura mpya nyingi kuliko zile za kale
 

Kasheshe

JF-Expert Member
Jun 29, 2007
4,696
782
mambo fasta fasta,JK hana jipya

Mama 5J's;

Ni issue ya Katiba: Mtu wa kwanza kabisa kuteuliwa na Rais kabla ya wengine ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali... nadhani ni ili aweze kumsaidia Rais asijevunja katiba.... especially kwa kuwa sio lazima Rais kuwa mwanasheria by professional a.k.a ueledi.
 

TIMING

JF-Expert Member
Apr 12, 2008
22,951
8,843
ngoja tusubirie mawaziri

nina hamu ya mapya lakini hisia zangu zinashindwa kukwepa hawa... Kawambwa, vita, ngeleja, nchimbi, kombani, mwakyusa, mwinyi, makamba, pinda, lowassa, labda na wawili watatu wapya... Mawaziri kama stini, na washikaji vyeo kama laki
 

PigaKuraYako

Member
Oct 28, 2010
21
6
fredericwere.jpg



Rais Jakaya Kiwete amemteua rasmi jaji frederick mwita werema kuwa mwanasheria mkuu wa serikali muda mfupi baada ya kuapishwa kwake leo katika uwanja wa uhuru jijini dar.Jaji werema anapata nafasi hiyo kwa mara nyingine kuendelea na wadhifa huo ambao alikuwa nao hapo awali.

KUNA MTU ANAJUA CV YA HUYU MTU ?
 

Kasheshe

JF-Expert Member
Jun 29, 2007
4,696
782
This is not news... guys... sio kila kitu kujadiliwa Jaji Werema piga mzigo twende mbele!
 

Gurtu

JF-Expert Member
May 15, 2010
1,237
318
fredericwere.jpg



Rais Jakaya Kiwete amemteua rasmi jaji frederick mwita werema kuwa mwanasheria mkuu wa serikali muda mfupi baada ya kuapishwa kwake leo katika uwanja wa uhuru jijini dar.Jaji werema anapata nafasi hiyo kwa mara nyingine kuendelea na wadhifa huo ambao alikuwa nao hapo awali.

KUNA MTU ANAJUA CV YA HUYU MTU ?

Poa tu, lakini ajitahidi sana maana bunge la safari hii lina Tundu. Asije akafanya kazi kwa mazoea kama katika kipindi kilichopita ambapo alikuwa anasaidiwa na Andrew Chenge kujibu maswali. Isije ikawa ujaji wake nao ni wa kuchakachuliwa
 

Ochu

JF-Expert Member
May 13, 2008
975
45
state attorney, mkurugenzi wa katiba na haki za binadamu ofisi ya mwanasheria mkuu, jaji wa mahakama kuu na mwanasheria mkuu wa serikali.
 

Mwanamageuko

JF-Expert Member
Oct 31, 2010
8,607
5,565
Hehe hivi rais anapomaliza urais wake anakuwa pia ana-afect ajira za wateule wake wote? I mean wakuu wa wilaya, mikoa, AG na kadhalika?

Au werema aliapishwa kwa mkataba mfupi? Ina maana na jaji mkuu mpya ataapishwa punde?
KAATIBA:tape:
 
0 Reactions
Reply
Top Bottom