fredmlay
JF-Expert Member
- Apr 30, 2008
- 1,849
- 388
Hiyo ni kweli mkishikamana na kuwa na chombo kimoja cha uwakilishi kwa wote itaongeza nguvu na kusukuma maendeleo mbele kwa haraka zaidi..Mwanaharaki Ponda.
Kwa nini kila wakati unakuwa against Bakwata?
Tulikuwa tunalilia kupata Mufti na tayari tumempata,huoni kama hii ni hatua moja mbele?
Mara nyingi nimekuwa sikuelewi kwani unaelekea kuwa mtu wa shari kuliko kusaidia jami ambayo ipo chini.
Wenzetu wanaitumia nafasi vizuri na wamejaza vyuo vikuu sisi hata sekondari za kuhesabu na tukitoka hapo ni kulia kuonewa kama yatima.
Tutumie fursa na tuwe waadilifu tutapata maendeleo.
Kama una hoja nenda kaongee na Sheikh Mkuu lakini kwangu nashindwa kukuelewa.
Hebu Ponda mtizame Kijana Arfu wa Islamic foundation mambo anayosimamia,huu ni mfano wa kuigwa sio kila wakati kupinga wenzio.