Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu Tanzania FAKIHI JUNDU [Miaka 65] anatarajiwa kustaafu mapema mwezi July 2014. JUNDU amedumu katika nafasi hiyo tangu mwaka 2009.
Habari nilizozipata kutoka kwa jamaa fulani ni kwamba Rais atamteua Mwanamama MWANAISHA ATHUMANI KWARIKO [Jaji Mfawidhi - Songea] kuwa Jaji Kiongozi.
Endapo tetesi hizi ni za kweli, inatarajiwa Jaji huyo kuwa mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huo.
Bado nafatilia kujua wasifu wake na endapo ana sifa zinazofaa kuwa Jaji Kiongozi. Baadhi ya watu nimesikia wakiwa na mawazo tofauti kwamba uteuzi huo huenda usifae na kukubalika kwa majaji wakongwe katika Mahakama Kuu ya Tanzania.
Ikumbukwe kwamba kwa mujibu wa Katiba ya mwaka 1977, Jaji Kiongozi ndio Mkuu wa Mahakama Kuu na ni msaidizi namba moja wa Jaji Mkuu katika kuongoza Judiciary.
Habari nilizozipata kutoka kwa jamaa fulani ni kwamba Rais atamteua Mwanamama MWANAISHA ATHUMANI KWARIKO [Jaji Mfawidhi - Songea] kuwa Jaji Kiongozi.
Endapo tetesi hizi ni za kweli, inatarajiwa Jaji huyo kuwa mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huo.
Bado nafatilia kujua wasifu wake na endapo ana sifa zinazofaa kuwa Jaji Kiongozi. Baadhi ya watu nimesikia wakiwa na mawazo tofauti kwamba uteuzi huo huenda usifae na kukubalika kwa majaji wakongwe katika Mahakama Kuu ya Tanzania.
Ikumbukwe kwamba kwa mujibu wa Katiba ya mwaka 1977, Jaji Kiongozi ndio Mkuu wa Mahakama Kuu na ni msaidizi namba moja wa Jaji Mkuu katika kuongoza Judiciary.