Uteuzi wa Dr. Slaa wageuka mwiba mwingine kwa upinzani

nygax

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,371
865
Amani iwe kwenu,

Nadhani wengi wetu tunakumbuka namna ambavyo Dr. Wilbroad Slaa alivyoleta mshituko mkubwa katika ulimwengu wa siasa, baada ya kutangaza rasmi kwamba anastaafu siasa.

Maamuzi haya aliyafanya baada ya yeye mwenyewe kusema hakuridhishwa na mchakato mzima wa kumpokea na hatimae kumpitisha mwanasiasa `machachari' Edward Lowassa kutoka CCM, aipeperushe bendela ya CHADEMA kwa mwavuli wa UKAWA, katika uchaguzi mkuu wa 2015.

Maamuzi haya yalimfanya apokee kila aina ya matusi na kejeli, huku wengine wakimbatiza jina `Dr. mihogo', wengine wakamwita msaliti na wengine wakimtukania hata familia yake.

Baada ya taarifa za uteuzi wa Dr. Slaa kuenea katika mitandao ya kijamii, kunajambo ambalo si la kawaida limeibuka hasa ktk upande wa upinzani,
wanalalamikia mbinu za Mh. Rais kuwateuwa wapinzani katika nyadhifa mbalimbali, akiwemo slaa, kwamba ni mbinu za kuuwa ama kudhoofisha upinzani.

Swali fikirishi: Wapinzani bado walimhesabu Slaa kama mpinzani? Ama Mh. rais amekosea kumchukua Dr. Slaa kama assert?

Nawasilisha.
 
Amani iwe kwenu.
nadhani wengi wetu tunakumbuka namna ambavyo Dr Wilbroad Slaa alivyoleta mshituko mkubwa katika ulimwengu wa siasa, baada ya kutangaza rasmi kwamba anastaafu siasa.
Maamuzi haya aliyafanya baada ya yeye mwenyewe kusema hakuridhishwa na mchakato mzima wa kumpokea na hatimae kumpitisha mwanasiasa `machachari' Edward Lowassa kutoka CCM, aipeperushe bendela ya CHADEMA kwa mwavuli wa UKAWA, ktk uchaguzi mkuu wa 2015.
maamuzi haya yalimfanya apokee kila aina ya matusi na kejeli, huku wengine wakimbatiza jina `Dr. mihogo', wengine wakamwita msaliti na wengine wakimtukania hata familia yake.
Baada ya taarifa za uteuzi wa Dr. Slaa kuenea ktk mitandao ya kijamii, kunajambo ambalo si la kawaida limeibuka hasa ktk upande wa upinzani,
wanalalamikia mbinu za Mh. Rais kuwateuwa wapinzani ktk nyadhifa mbalimbali, akiwemo slaa, kwamba ni mbinu za kuuwa ama kudhoofisha upinzani!
Swali fikirishi: wapinzani bado walimhesabu Slaa kama mpinzani? ama Mh. rais amekosea kumchukua Dr. Slaa kama assert?
nawasilisha.
Kwani bado alikuwa chadema?
 
Mwiba kivipi, kwani Dr.Slaa ni kiongozi au mwanachama wa chama gani cha Upinzani? Msituzingue nendeni mkabebe maboksi ya ubalozini huko!
Sasa mbona mnalialia na teuzi? tulieni dawa iingie vizuri.
Kutoka kuwa rais mtarajiwa hadi kuwa balozi wa akiba,Kutoka kuwa na mke hadi kuwa na mchumba,hiyo ndio improvement!
Yule mzee wetu alikuwa waziri mkuu kwa miaka kumi, awamu ya tatu, mmempa uwenyekiti wa chadema kule mchangani, hayo ni maendeleo?
 
kwa hili la dr slaa limenifanya niamini kuwa ukiwa upinzani unakua na faida kubwa kuliko kuwa chama tawala. maana ukiwa mpinzani unakua na thamani. ni wangapi wapo kwenye chama chetu mashuhuri na wafia chama chetu? lakini badala na hizo nafasi kuwa zetu, wanapewa wapinzani. kwa upande wangu naona upinzani, huu ni wakati wa kujivunia maana nafasi za kuteuliwa zipo kwaajiri yao pale watakapoonyesha nia ya kuzipata
 
Mpaka sasa ngoma dro, Lowasa alitoka CCM kuingia Chadema akapata uteuzi wa kugombea urais siku hiyohiyo. Naamini Dr Slaa na hata CCM waliomkata waliumizwa na hilo. Leo ni zamu Dr Salaa kupiga vigelegele, wengine nao wanaumia. Siasa zinachoma
 
..aha wapi...hamna cha mwiba wala nini....maana watu kama slaa tayari walikua ma reject tangu 2015...mwiba kivipi mtu alifikia hata kuosha vyombo ulaya!!...muasi wa upinzani hawezi kuwa mwiba....kwa msiojua kusoma nyakati hamjajua kuwa mkakati wa sasa utawala huu ni kuwapata waasi kwa namna yoyote..hata ikibidi kuwanunua ili ikifika 2020 watumike kwenye kampeni.. Maana kuna kila dalili watu makini wakatoka ccm hapo 2020....
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom