MAMMAMIA
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 3,811
- 1,603
Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayotumika sasa, kifungu kifuatacho kinasema:
Na kwa mujibu wa Katiba hiyo, kifungu kifuatacho kinasema:
Lakini kwa mujibu wa Katiba hiyo hiyo katika kifungu hiki:
Kutokana na kifungu hiki cha mwisho, Raisi anapewa uwezo wa kutengua lile sharti la kuwa na sifa maalum kwa muda usiopungua miaka mitano na kumteua mtu huyo kuwa Jaji wa Mahakama Kuu lakini sio kutengua sifa ya kuwa mwanachama wa chama cha siasa.
Kwa hivyo, kwa mujibu wa Kifungu 113A cha Katiba, kwa maoni yangu, uteuzi wa AG Werema si halali kwa sababu kwenye CV yake Mheshimiwa huyu amejithibitisha mwenyewe kuwa ni mwanachama wa chama cha siasa, yaani CCM.
Wenzetu mnaojua sheria, naomba mtusaidie zaidi kwa hili.
113A. Itakuwa ni marufuku kwa Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jaji wa Mahakama Kuu, Hakimu wa ngazi yoyote kujiunga na chama chochote cha Siasa, isipokuwa tu kwamba atakuwa nahaki ya kupiga kura iliyotajwa katika ibara ya 5 ya Katiba hii.
Na kwa mujibu wa Katiba hiyo, kifungu kifuatacho kinasema:
59 (2) Mtu yeyote hatastahili kuteuliwa kushika madaraka ya Mwanasheria Mkuu isipokuwa tu kama kwa mujibu wa Katiba hii ana sifa maalum, kama ilivyofafanuliwa katika ibara ya 109(8) zinazomwezesha kuteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano au Jaji wa Mahakam Kuu ya Zanzibar, na amekuwa na mojawapo ya hizo sifa maalum kwa muda usiopungua miaka mitano.
Lakini kwa mujibu wa Katiba hiyo hiyo katika kifungu hiki:
108(9) Iwapo Rais atatosheka kwamba ijapokuwa mtu mwenye sifa mojawapo ya hizo sifa maalum hakuwa nayo sifa hiyo kwa muda usiopungua miaka mitano, lakini mtu huyo ana uwezo, ujuzi na kwa kila hali anafaa kukabidhiwa madaraka ya Jaji wa Mahakama Kuu na kuna sababu za kumfanya mtu huyo astahili kukabidhiwa madaraka hayo, basi Rais aweza kutangua lile sharti la kuwa na sifa maalum kwa muda usiopungua miaka mitano, na baada ya kushauriana na Tume ya Kuajiri ya Mahakama, Rais aweza kumteua mtu huyo kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.
Kutokana na kifungu hiki cha mwisho, Raisi anapewa uwezo wa kutengua lile sharti la kuwa na sifa maalum kwa muda usiopungua miaka mitano na kumteua mtu huyo kuwa Jaji wa Mahakama Kuu lakini sio kutengua sifa ya kuwa mwanachama wa chama cha siasa.
Kwa hivyo, kwa mujibu wa Kifungu 113A cha Katiba, kwa maoni yangu, uteuzi wa AG Werema si halali kwa sababu kwenye CV yake Mheshimiwa huyu amejithibitisha mwenyewe kuwa ni mwanachama wa chama cha siasa, yaani CCM.
Wenzetu mnaojua sheria, naomba mtusaidie zaidi kwa hili.