Uteuzi wa AG Werema ni BATILI au halali?

MAMMAMIA

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
3,811
1,603
Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayotumika sasa, kifungu kifuatacho kinasema:
113A. Itakuwa ni marufuku kwa Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jaji wa Mahakama Kuu, Hakimu wa ngazi yoyote kujiunga na chama chochote cha Siasa, isipokuwa tu kwamba atakuwa nahaki ya kupiga kura iliyotajwa katika ibara ya 5 ya Katiba hii.


Na kwa mujibu wa Katiba hiyo, kifungu kifuatacho kinasema:
59 (2) Mtu yeyote hatastahili kuteuliwa kushika madaraka ya Mwanasheria Mkuu isipokuwa tu kama kwa mujibu wa Katiba hii ana sifa maalum, kama ilivyofafanuliwa katika ibara ya 109(8) zinazomwezesha kuteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano au Jaji wa Mahakam Kuu ya Zanzibar, na amekuwa na mojawapo ya hizo sifa maalum kwa muda usiopungua miaka mitano.

Lakini kwa mujibu wa Katiba hiyo hiyo katika kifungu hiki:
108(9) Iwapo Rais atatosheka kwamba ijapokuwa mtu mwenye sifa mojawapo ya hizo sifa maalum hakuwa nayo sifa hiyo kwa muda usiopungua miaka mitano, lakini mtu huyo ana uwezo, ujuzi na kwa kila hali anafaa kukabidhiwa madaraka ya Jaji wa Mahakama Kuu na kuna sababu za kumfanya mtu huyo astahili kukabidhiwa madaraka hayo, basi Rais aweza kutangua lile sharti la kuwa na sifa maalum kwa muda usiopungua miaka mitano, na baada ya kushauriana na Tume ya Kuajiri ya Mahakama, Rais aweza kumteua mtu huyo kuwa Jaji wa Mahakama Kuu.

Kutokana na kifungu hiki cha mwisho, Raisi anapewa uwezo wa kutengua
lile sharti la kuwa na sifa maalum kwa muda usiopungua miaka mitano na kumteua mtu huyo kuwa Jaji wa Mahakama Kuu lakini sio kutengua sifa ya kuwa mwanachama wa chama cha siasa.

Kwa hivyo, kwa mujibu wa Kifungu 113A cha Katiba, kwa maoni yangu, uteuzi wa AG Werema si halali kwa sababu kwenye CV yake Mheshimiwa huyu amejithibitisha mwenyewe kuwa ni mwanachama wa chama cha siasa, yaani CCM.

Wenzetu mnaojua sheria, naomba mtusaidie zaidi kwa hili.
 
Hili nalo neno. Kanunni za bunge zinasemaje kuhusu mtu baki kupeleka hoja binafsi bungeni? Nadhani ni muda sasa wananchi tupate fursa ya kuhoji mambo mbalimbali moja kwa moja bungeni.
 
Kuna Judge moja albino kule Kenya juzi juzi tu katengua uteuzi wa 47 county commissioners amesema taratibu hazikufuatwa.
And the government has appealed against the court ruling.

lakini hapa kwetu hakuna judge mwenye ubavu huo
 
Katika tafsiri ya kisheria,uteuzi wa Jaji Werema kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni halali.Kwanza,Werema si Jaji tena(limebaki jina tu).Pili,Werema alikuwa na sifa za kuwa Jaji hivyo kuwa na sifa za kuteuliwa kuwa Mwanasheria Mkuu.

Tatu, ibara zilizotajwa zazungumzia mambo mawili tofauti:uteuzi wa Jaji na ule uteuzi wa Mwanasheria Mkuu.Ibara hizo zikisomwa vyema,hazikatazi Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwa na chama.

Swali linalobaki labda ni hili: Werema ana uwezo wa kuwa na cheo alichonacho? Jibu langu ni hapana.Aliteuliwa kwa kuwa alikuwa Mamluki tangu akiwa Jaji Mahakama Kuu.Wapo wengi tu wanaomzidi.Ni kichwa maji...
 
Katika tafsiri ya kisheria,uteuzi wa Jaji Werema kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni halali.Kwanza,Werema si Jaji tena(limebaki jina tu).Pili,Werema alikuwa na sifa za kuwa Jaji hivyo kuwa na sifa za kuteuliwa kuwa Mwanasheria Mkuu.

Tatu, ibara zilizotajwa zazungumzia mambo mawili tofauti:uteuzi wa Jaji na ule uteuzi wa Mwanasheria Mkuu.Ibara hizo zikisomwa vyema,hazikatazi Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwa na chama.

Swali linalobaki labda ni hili: Werema ana uwezo wa kuwa na cheo alichonacho? Jibu langu ni hapana.Aliteuliwa kwa kuwa alikuwa Mamluki tangu akiwa Jaji Mahakama Kuu.Wapo wengi tu wanaomzidi.Ni kichwa maji...
Maelezo yako yananishawishi niamini kuwa uko sahihi, ndio maana nikawataka wanaojua hizi sheria watueleze.

Hoja imekaa kisiasa na kikereketwa zaidi
Inawezekana, kwani Tanzania bila ya ukereketwa haiwezekani.
 
Kuna Judge moja albino kule Kenya juzi juzi tu katengua uteuzi wa 47 county commissioners amesema taratibu hazikufuatwa.
And the government has appealed against the court ruling.

lakini hapa kwetu hakuna judge mwenye ubavu huo

Mkuu hapo kwenye wekundu wakina Shaymaar na Under the same sun watakushukia?
 
Mmmmmmmmmmmmmhhhhhh, sijui kama kuna mtu serikalini wakukusiliza hoja yako hii. Waliompotosha watang'ang'ania hakuna tatizo.
 
Sasa anasubiri nn kujiuzuru,wanasheria tusaidieni huu nao udhaifu wa jambazi kuu
 
Back
Top Bottom