Cynic
JF-Expert Member
- Jan 5, 2009
- 5,144
- 1,648
Msolla aunda kamati ya kuchochea sayansi
James Magai
WAZIRI wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Profesa Peter Msolla ameunda Kamati ya ushauri katika masuala ya Teknolojia na Mawasiliano ambayo pamoja na majukumu mengine itaishauri Serikali namna ya kuwavutia vijana wasome masomo ya sayansi.
Prof. Msolla alisema hayo ofisini kwake jana, kabla ya uzinduzi wa Kamati ya ushauri wa masuala ya Teknolojia na Mawasiliano ambayo iliundwa hivi karibuni.
Wajumbe wa Kamati hiyo ni Profesa Mathew Luhanga , Profesa Burton Mwamila, Profesa Suzan Nchimbi Msolla, Profesa Keto Mshigeni na Margareth Munyagi.Wengine ni Dk.Tito Mwinuka na Margareth Komba ambao mi wajumbe wa sekretarieti.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye ni Makamu Mkuu Mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Profesa Luhanga, alsema Kamati yake itatumia uwezo wake utakaoisaidia Wizara katika utendaji wake kwa ajili ya maendeleo ya Taifa na kwamba wiki ijayo watakaa kutafakari namna ya kutekeleza majukumu hayo.
Tuma maoni kwa Mhariri
© Mwananchi Communications Ltd 2006- 2009
Hivi hakuna wanasayansi wanaofaa kuwepo kwenye kamati hii kutoka kwinginepo? Na wote ni wakristo!
James Magai
WAZIRI wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Profesa Peter Msolla ameunda Kamati ya ushauri katika masuala ya Teknolojia na Mawasiliano ambayo pamoja na majukumu mengine itaishauri Serikali namna ya kuwavutia vijana wasome masomo ya sayansi.
Prof. Msolla alisema hayo ofisini kwake jana, kabla ya uzinduzi wa Kamati ya ushauri wa masuala ya Teknolojia na Mawasiliano ambayo iliundwa hivi karibuni.
Wajumbe wa Kamati hiyo ni Profesa Mathew Luhanga , Profesa Burton Mwamila, Profesa Suzan Nchimbi Msolla, Profesa Keto Mshigeni na Margareth Munyagi.Wengine ni Dk.Tito Mwinuka na Margareth Komba ambao mi wajumbe wa sekretarieti.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye ni Makamu Mkuu Mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Profesa Luhanga, alsema Kamati yake itatumia uwezo wake utakaoisaidia Wizara katika utendaji wake kwa ajili ya maendeleo ya Taifa na kwamba wiki ijayo watakaa kutafakari namna ya kutekeleza majukumu hayo.
Tuma maoni kwa Mhariri
© Mwananchi Communications Ltd 2006- 2009
Hivi hakuna wanasayansi wanaofaa kuwepo kwenye kamati hii kutoka kwinginepo? Na wote ni wakristo!