Uteuzi Mkurugenzi wa TBC, Katibu Mkuu na Naibu Makatibu Wakuu

Picha+no+3.JPG
 
'Bwana Hab Mkwizu ameteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu Menejimenti ya Utumishi wa Umma. Kabla ya uteuzi wake, Bwana Mkwizu alikuwa Karani wa Baraza la Mawaziri.'

wakuu ukiwa karani baraza la mawaziri unakuwa na majukumu gani? je ni tofauti na makarani wengine nimepata utata kidogo ,kutoka ukarani hadi unaibu katibu mkuu

karani si kazi yake kubeba mafaili na kuchemsha chai au
 
Clement Mshana ni mtu makini sana. Hajui na hana siasa za maji taka. ataipeleka TBC na Nchi mbali sana. Mungu amjalie afya njema. nawapongeza wengine ingawa sina UHAKIKA sana na utendaji wao ila naamini sio "mashemeji".

Mhh sidhani kama una uhakika na uyasemayo juu ya huyu jamaa "Mshana". Muda mfupi tu aliokaa kama kamishna hapo wizara ya habari, amejionesha kuwa ni mtu wa mfumo wa serikali, ni mtu anayefanya kulingana na nini serikali inataka. Kwa huyu jamaa kuwa pale TBC, vyama vya upinzani vilie tu, masuala ya airtime hayatakuwa sawa na ile ya CCM. Kama nchi nafikiri imerudi nyuma hatua zaidi ya mia kwa kumtosa TIDO MHANDO, alijitahidi kuibadilisha TBC angalau ikaonekana kama ipo kwa ajili ya watanzania wote.
 
Tido Mhando pengine uliweka viwango vya juu saaana katika tasnia ya habari nchini kwa namna ambayo woote huonekana kupwaya hata kwa kutajwa tu. Kweli ni sawa tu na viwango alivyoviweka Mwl Nyerere katika taasisi ya Urais barani Afrika mpaka kufanya wanaokuja nyuma yake kuonekana tu kama vioja vile.

Pamoja na yote, huyu mtaalam mpya aliyepata kazi anajulikana kuwa ni closed-minded person mwenye kujihisi yuko juu ya dunia nzima afadhali ya mhaya yeyote mwenye majigambo uliyewahi kumfahamu, mwingi wa ushabiki wa kiitikadi za CCM katika chombo cha Umma wa Tanzania, uendeshaji wa chombo cha habari kama shirika la Scotland Yard dhidi ya sauti huru na ni mkabila wa kutupwa na mzaha katika mambo ya kitaaluma sawa yake na 'Jaji' Werema.

Hakika sasa TBC ni njia nyeupe kuelekea uendeshaji wa ki-ujima ujima kweli kweli.
 
Clouds kama kawaida yao.....wameshamdandia na maswali yasiyo muelekeo!!ameyajibu kiufasaha sana
 
Kamishna wa Nishati, Ndugu Bashir Mrindoko naye achukuliwe hatua za kinidhamu kwa kushindwa kumshauri Katibu Mkuu wake mpya kuhusu udhaifu wa Richmond Development Company LLC ambao ulijulikana dhahiri na Wizara mwaka 2004 kwenye Mradi wa bomba la mafuta. Ndugu Mrindoko ndiye aliyeiandikia barua Kampuni hiyo kusitisha Mkataba wake na Serikali mwezi mmoja tu kabla ya mchakato wa Zabuni ya umeme wa dharura haujaanza tusiwe warahisi kusahau !
Ukiwa gamba utang'angania magamba wenzako.
Hongera Bwana Clement Senzota Mwete Mshana, Nenda kafanye alichokutuma aliyekuteua usije ukafuata ya Tido yeye huenda alikuwa hajajua vizuri TBC ni mali ya nani ndiyo maama akaruhusu mijadala nchi nzima japo wamiliki hawakushiriki.
Akawarudishie wenye magamba TVT yao.
 
Injinia Bashir J. Mrindoko ameteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu katika Wizara ya Maji. Kabla ya uteuzi wake, Bwana Mrindoko alikuwa Kamishna wa Nishati na Mafuta ya Petroli.

huu uteuzi kichwa mafuta?? maji akafanye nini injinia huyu maskini???

...Nishati na mafuta ya petroli! Tofauti ya Nishati na mafuta ya petroli ni nini? Mbona mafuta ya taa na diseli hakuna kamishna? Au ndo mambo ya Makanjanja wetu?
 
ila jamaa kaenda shule,tatizo ni kufuata nini wakuu wanataka,hilo hatoweza kukwepa,kwani ndilo lililomwondowa Tido,alikataa kunyenyekea
 
Kikwete kateua Manaibu makatibu wakuu 10.
1.Waliokuwepo zamani wamepigwa chini? staafu? au ni magamba?
au
2. Ametengeneza ajira kumi? Hivi vyeo katika wizara hizo vilikuwepo kabla?
Naomba kueleweshwa.
 
Kuhamisha Maji kutoa Mtoni Kupeleka Ziwani...ndo Mtindo wa Kikwete ..What changes will it bring?
 
Tido Mhando pengine uliweka viwango vya juu saaana katika tasnia ya habari nchini kwa namna ambayo woote huonekana kupwaya hata kwa kutajwa tu.

Kweli ni sawa tu na viwango alivyoviweka Mwl Nyerere katika taasisi ya Urais barani Afrika mpaka kufanya wanaokuja nyuma yake kuonekana tu kama vioja vile.

Pamoja na yote, huyu mtaalam mpya aliyepata kazi anajulikana kuwa ni closed-minded person mwenye kujihisi yuko juu ya dunia nzima afadhali ya mhaya yeyote mwenye majigambo uliyewahi kumfahamu, mwingi wa ushabiki wa kiitikadi za CCM katika chombo cha Umma wa Tanzania, uendeshaji wa chombo cha habari kama shirika la Scotland Yard dhidi ya sauti huru na ni mkabila wa kutupwa na mzaha katika mambo ya kitaaluma sawa yake na 'Jaji' Werema.

Hakika sasa TBC ni njia nyeupe kuelekea uendeshaji wa ki-ujima ujima kweli kweli.
 
Back
Top Bottom