Uteuzi Mchanganyo wa Watendaji Waleta hofu juu ya Umakini Uliopo

Chakaza

JF-Expert Member
Mar 10, 2007
39,747
71,105
Muhimbili ulipotokea mchanganyo wa operation (jambo ambalo ni la muhimu) na kusababisha mgojwa wa mguu kupasuliwa kichwa na wa Kichwa kupasuliwa mguu, kulitokea hofu kubwa juu ya umakini uliopo kwenye utendaji wa Hospitali yetu kuu.
Hofu hiyo sasa imehamia kwa watendaji wakuu wanao husika na teuzi (jambo ambalo ni la msingi kwa shughuli za serikali) kuwa jee kweli wako makini? Mkanganyiko uliojitokeza katika teuzi za Madc, MaDas na wakurugenzi wa halmashauri umeleta picha kuwa kuna watu wanafanya kazi bila kuwa makini.
Jee ni mangapi yanayofanyika kwa mtindo huu bila kufahamika? Kuna mikataba mingapi inayopita kwa mtindo huu na kuja kutuathiri baadae? Sio ajabu baada ya miaka miwili ijayo tukajikuta kwenye matatizo makubwa sana. Bahati mbaya hatupendi kukosolewa bali kusifiwa tuu.
 
Huyu jamaa pia anachangia kuwa na wafanyakazi hewa.....cheo kimoja watu wawili
 
Na mbaya zaidi uzembe na kukosa umakini unatokea kwenye ofisi ya juu kabisa nchini.

Nina mashaka na umakini kwenye kupitia kwenye mikataba ya kimataifa.
 
ingekuwa ni uamuzi wangu...

ningeweka sheria wasomi wote baada ya kumaliza chuo wakaajiriwe big 4 proffessional firms angalau for 3 years ndio waajiriwe serikalini... huko wakajifunze kazi na accountability...

mtu unakosea hata kupanga majina kwenye excel kweli??

kitu simpo tu kama hicho nacho unakosea kweli??.. just a spreadsheet unaijaza na ukimaliza una sort kukagua kama kuna jina limejirudia au umeandika vibaya..

kiukweli tuko nyuma sana na Tanzania ya viwanda haiwez kuja kama tuna uzembe mwingi hivi hadi wa kuchapa majina...

hivyo viwanda hiyo mitambo ya uzalishaji itakufa siku mbili tu kwa uzembe
 
Mtu yeyote mwenye basic skills za MS Excel hiyo wala isingekuwa issue. Ni suala la kuyaingiza hayo majina kwenye Excel then with simple formula inakuonesha duplicates zote.
 
JAMANI MSISABABISHE MTU AKATWANGWA TENA MUMSAMEHE JAMANI
Bora watwangwe tuu, kama watumishe wenyewe ndio wa aina hii sijui itakuwaje kwenye mikataba. Na sio ajabu ndio maana kuna mikanganyiko hata kwenye budget.
Naanza kupata mashaka na katibu wetu Kiongozi bw Kijazi kama haya yanatokea ofisini kwake naye yuko kimya tuu.
 
Maamuzi au taarifa yoyote kutoka Ofisi Kuu ya Nchi yanatakiwa yawe 99.999% error-free kwa kila kitu kuanzia usahihi wa taarifa yenyewe, lugha, grammar, spelling, etc. etc. Ni taarifa ambayo haitakiwi kutiliwa shaka ya aina yoyote kutokana na usahihi wake na ambayo hata wanafunzi vyuoni na kwingineko wanaweza kuitumia kama reference ya mfano wa taarifa bora kabisa. Inatakiwa kuwa aina ya taarifa ambayo kuikosoa ni ma-profesa bobezi pekee ndio wanaoweza kutoa dosari; dosari ambayo ni "negligible" or "immaterial".

Lakini haya mambo ya wateule kuombwa kutoka nje kwa sababu waliingia ukumbini (Ikulu) kwa "makosa" kwa kweli hapana; ni aibu. Kuna tatizo la msingi mahali; tatizo ambalo kuna siku litaligharimu taifa.
 
Hii ndo Tanzania yangu katika Serikali ya Awamu ya Tano.

VIONGOZI WANACHOTAKA NI SIFAAAA TU.
 
Na mbaya zaidi uzembe na kukosa umakini unatokea kwenye ofisi ya juu kabisa nchini.

Nina mashaka na umakini kwenye kupitia kwenye mikataba ya kimataifa.

Ikulu, utumishi, rais, msemaji, na katibu hawakai pamoja kushauriana kucompile or any activity that show unity among them
 
Back
Top Bottom