Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,176
- 25,446
Lengai Ole Sabaya, aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, ameanza kujitetea kwenye kesi yake ya jinai yenye sura ya uporaji, kujeruhi na kutesa.
Soma hapa >> Utetezi wa Sabaya: Amwangushia zigo Hayati Magufuli na kudai Gavana Luoga na Makamu wa Rais Dkt. Mpango walifahamu
Utetezi wake, kadiri nilivyomsikiliza, naugawa kwenye sehemu zifuatazo.
Mosi, yapo aliyoyakiri. Amekiri kufika sehemu ya tukio kwa kutaja jina hilohilo na mahali palepale. Na akamtaja mmiliki huyohuyo ambaye ametajwa kwenye mashtaka na ushahidi. Hapa, ana kazi ya kukanusha kiushahidi kutofanya yote anayoshtakiwa nayo.
Pili, amesema kuwa alifanya aliyoyafanya akitekeleza maagizo ya mamlaka ya uteuzi. Ameeleza kuwa alikuwa sehemu ya tukio kutekeleza maagizo ya mamlaka ya uteuzi. Hapa, Sabaya atapaswa kuwasilisha maagizo hayo ili kuona kuwa hakuvuka mipaka. Maagizo husika lazima yawasilishwe mahakamani ili aaminike. Nyaraka au sauti ni muhimu hapa.
Tatu, amejipambanua mahakamani kuwa yeye alikuwa zaidi ya Mkuu wa Wilaya. Kuwa yeye alikuwa akiongoza au kushiriki operesheni mbalimbali zilizokuwa zikiagizwa na mamlaka yake ya uteuzi. Hapa ndipo alipowataja Makamu wa Rais na Gavana wa Benki Kuu kama watu waliofahamu operesheni mojawapo iliyofanyika Dar es Salaam.
Kimsingi, hapo Sabaya anapaswa kuwasilisha ushahidi wa hilo kwa maana ya uteuzi wenye hadidu rejea za operesheni hizo pamoja na kuwapata aliowataja kama mashahidi wake. Waliotajwa wanapaswa kuja kukiri kufahamu operesheni hiyo ya Dar ambayo hatahivyo haisaidii wala haina uhusiano wowote na kesi husika huko Arusha.
Nne, Sabaya amedai kuwa yeye bado ni mtumishi wa serikali. Hakusema ni kwa nafasi ipi na ana majukumu gani. Hilo nalo anapaswa aliweke sawa kwa ushahidi.
Kiujumla, utetezi wa Sabaya umetanua sana uwanja na kumuweka kwenye kazi ngumu sana kuchomoka kwenye kesi yake. Ameanzisha mambo mengi yanayohitaji ushahidi. Na ushahidi mwingine wa maneno hautapatikana kwakuwa yeye mwenyewe amekataa kuwataja alioambatana nao kwenda sehemu ya tukio siku husika. Pia, mamlaka yake ya uteuzi haipo tena.
Mahakamani kunahitajika ushahidi wa kuthibitisha unachokisema. Unaweza kuwa wa nyaraka, maneno au vyote. Ushahidi mzuri ni wa wengine wanaokuja kuushadidia ushahidi wako. Kunapokosekana ushahidi, maneno yanabaki porojo isiyo na maana yoyote.
Soma hapa >> Utetezi wa Sabaya: Amwangushia zigo Hayati Magufuli na kudai Gavana Luoga na Makamu wa Rais Dkt. Mpango walifahamu
Utetezi wake, kadiri nilivyomsikiliza, naugawa kwenye sehemu zifuatazo.
Mosi, yapo aliyoyakiri. Amekiri kufika sehemu ya tukio kwa kutaja jina hilohilo na mahali palepale. Na akamtaja mmiliki huyohuyo ambaye ametajwa kwenye mashtaka na ushahidi. Hapa, ana kazi ya kukanusha kiushahidi kutofanya yote anayoshtakiwa nayo.
Pili, amesema kuwa alifanya aliyoyafanya akitekeleza maagizo ya mamlaka ya uteuzi. Ameeleza kuwa alikuwa sehemu ya tukio kutekeleza maagizo ya mamlaka ya uteuzi. Hapa, Sabaya atapaswa kuwasilisha maagizo hayo ili kuona kuwa hakuvuka mipaka. Maagizo husika lazima yawasilishwe mahakamani ili aaminike. Nyaraka au sauti ni muhimu hapa.
Tatu, amejipambanua mahakamani kuwa yeye alikuwa zaidi ya Mkuu wa Wilaya. Kuwa yeye alikuwa akiongoza au kushiriki operesheni mbalimbali zilizokuwa zikiagizwa na mamlaka yake ya uteuzi. Hapa ndipo alipowataja Makamu wa Rais na Gavana wa Benki Kuu kama watu waliofahamu operesheni mojawapo iliyofanyika Dar es Salaam.
Kimsingi, hapo Sabaya anapaswa kuwasilisha ushahidi wa hilo kwa maana ya uteuzi wenye hadidu rejea za operesheni hizo pamoja na kuwapata aliowataja kama mashahidi wake. Waliotajwa wanapaswa kuja kukiri kufahamu operesheni hiyo ya Dar ambayo hatahivyo haisaidii wala haina uhusiano wowote na kesi husika huko Arusha.
Nne, Sabaya amedai kuwa yeye bado ni mtumishi wa serikali. Hakusema ni kwa nafasi ipi na ana majukumu gani. Hilo nalo anapaswa aliweke sawa kwa ushahidi.
Kiujumla, utetezi wa Sabaya umetanua sana uwanja na kumuweka kwenye kazi ngumu sana kuchomoka kwenye kesi yake. Ameanzisha mambo mengi yanayohitaji ushahidi. Na ushahidi mwingine wa maneno hautapatikana kwakuwa yeye mwenyewe amekataa kuwataja alioambatana nao kwenda sehemu ya tukio siku husika. Pia, mamlaka yake ya uteuzi haipo tena.
Mahakamani kunahitajika ushahidi wa kuthibitisha unachokisema. Unaweza kuwa wa nyaraka, maneno au vyote. Ushahidi mzuri ni wa wengine wanaokuja kuushadidia ushahidi wako. Kunapokosekana ushahidi, maneno yanabaki porojo isiyo na maana yoyote.