Utetezi wa Gazeti la Raia Mwema kabla ya kufungiwa

Tanzania ikiwa na viongozi wa hovyo kama Msiba hatutaendelea.Hawa jamaa wa Guinea wakija bongo watu kama akina msigwa ni Moto tu.
 
Tusisahau kwamba nchi yetu imeharibika kimaadili kwa ujumla.Kwa hiyo mambo mengi ni maamuzi ya 'kushinikizwa' na wakubwa.Utawala wa sheria ni hadaa tu za watawala wetu.
 
Tatizo taasisi zote za umma zina report kwa CCM. Bila katiba mpya Taifa hili linakwenda shimoni.

Check ✔ and balance katika nchii hii ni ndogo sana..nachokiona mimi ni ukandamizwaji mkubwa wa wanao kwenda kinyume na matakwa ya CCM.

CCM iliyo wa wafuasi kama 6m wanataka nchi nzima watu wote 60m tufikiri kama wao, hii si sahihi na haitokaa iwezekane.
 
Nimeona Gerson Msigwa ameposti clip anasonga ugali kama alivyoita nguna nikajua huyu ni mchumia tumbo! Anaangalia sana tumbo lake na hii imekuwa ni kasoro kubwa sana Serikali kujaza Vila.za badala ya watu wenye ueledi!
Kwa mtu aliyesoma vizuri na anayejua sheria vizuri, kwa utetezi wa Gazeti la Raia Mwema inabidi Serikali iwalipe na si kuwafungia ama Serikali ndo ingejifungia kwa kukosa watu wenye ueledi wa kuisemea!
 
Maserikali mabovu mabovu ndio kazi yake hiyo, kufungia magazeti, kuzima internet kwa wananchi, kutumia intelligence na police kuzima uhuru wa kuongea na kuwaua raia wake,kubambikia watu kesi za kipuuzi, hayawezi kuongoza nchi ni kutishia tuu ili yakae madarakani na mwisho wake ni umaskini tuu wa Taifa lote
 
Oh wewe kweli ni akili nene kweli nasi akili kubwa
Ni ngumu kwa uwezo wako mdogo kujua maana ya akilinene.
Jiulize wewe u member humu tangu Jan.2021 lakini bado ni just a member, hata Senior member hujapata wakati mimi nina hardly mwezi mmoja tu humu lakini nimeshakuwa JF Expert Member!! Ndiyo utajua maana ya akili nene.
 
Hebu someni wenyewe utetezi na adhabu ndio utajua kuwa watu walikuwa na adhabu tayari kabla ya utetezi.

Tanzania bana End justify means badala ya means kujustify end View attachment 1925481View attachment 1925482View attachment 1925484View attachment 1925485
Jamaa wanazidi kuthibitisha kuwa hawana umakini na wamefungiwa kwa haki. Angalia tarehe ya barua yao ni 5 Agost 2021 wakati wanajibu barua iliyowafungia ya tarehe 3 Septemba 2021. Watu wa ajabu kabisa. Yaani walijibu hoja kabla hata hawajafungiwa?
 
Back
Top Bottom