Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

Tanganyika haikuwahi kuwa zao la watu wa Tanganyika; vinginevyo wazee wasingetaka uhuru kutoka kwa Mwingereza. Tanganyika ni zaidi ya nchi au mipaka au jina. Labda watu warudi nyuma na kujifunza historia yetu kidogo. Tanganyika ilizaliwa katika misingi yake ambayo mtu aliposema "Mtanganyika" ilijulikana anamaanisha nini. Labda watu mrudi na kusoma hotuba za kuelekea Uhuru, ya siku ya Jamhuri na Hotuba ya Nyerere Umoja wa Mataifa baada ya maadhimisho ya Uhuru. Misingi ambayo ilikamilika katika Tanzania. Tanzania ni zao la njozi ya Tanganyika.

Inanishangaza watu wanatukuza "Tanganyika" lakini hawataki kuangalia misingi ya Tanganyika ilikuwa nini na wengine hata hawajui ilikuwa ni nini. Huwezi kuwa na Tanganyika bila kurudia misingi yake! Ni sawa na mtu ambaye anataka kurudia nyumba aliyokuwa nayo lakini bila kurudia alipoijengea. Aidha utakachopata sicho - japo inaweza kufanana na ukaita ni chako. Tanganyika na Tanzania haviwezi kutenganishwa. Hata bila Zanzibar - Tanzania inaweza kuwepo kwa sababu Tanzania ni zao la Tanganyika.

Kinyume na watu wengi wanavyosema wakati wa Muungano Tanganyika haikupoteza utambulisho wake, iliukamilisha na inapaswa kuendelea kuukamilisha kwa kuelekea Shirikisho la Afrika ya Mashariki. Kuirudia Tanganyika ni kurudia kitu ambacho tulikiacha na kutaka kurudia nyuma ya historia. Ndio maana huwezi kuwakuta wazee waliofahamu uhuru na harakati za uhuru wanalilia Tanganyika - kama wapo wachache tu.
 
Tanganyika haikuwahi kuwa zao la watu wa Tanganyika; vinginevyo wazee wasingetaka uhuru kutoka kwa Mwingereza. Tanganyika ni zaidi ya nchi au mipaka au jina. Labda watu warudi nyuma na kujifunza historia yetu kidogo. Tanganyika ilizaliwa katika misingi yake ambayo mtu aliposema "Mtanganyika" ilijulikana anamaanisha nini. Labda watu mrudi na kusoma hotuba za kuelekea Uhuru, ya siku ya Jamhuri na Hotuba ya Nyerere Umoja wa Mataifa baada ya maadhimisho ya Uhuru. Misingi ambayo ilikamilika katika Tanzania. Tanzania ni zao la njozi ya Tanganyika.

Inanishangaza watu wanatukuza "Tanganyika" lakini hawataki kuangalia misingi ya Tanganyika ilikuwa nini na wengine hata hawajui ilikuwa ni nini. Huwezi kuwa na Tanganyika bila kurudia misingi yake! Ni sawa na mtu ambaye anataka kurudia nyumba aliyokuwa nayo lakini bila kurudia alipoijengea. Aidha utakachopata sicho - japo inaweza kufanana na ukaita ni chako. Tanganyika na Tanzania haviwezi kutenganishwa. Hata bila Zanzibar - Tanzania inaweza kuwepo kwa sababu Tanzania ni zao la Tanganyika.

Kinyume na watu wengi wanavyosema wakati wa Muungano Tanganyika haikupoteza utambulisho wake, iliukamilisha na inapaswa kuendelea kuukamilisha kwa kuelekea Shirikisho la Afrika ya Mashariki. Kuirudia Tanganyika ni kurudia kitu ambacho tulikiacha na kutaka kurudia nyuma ya historia. Ndio maana huwezi kuwakuta wazee waliofahamu uhuru na harakati za uhuru wanalilia Tanganyika - kama wapo wachache tu.

Tueleweshe hiyo historia ili tupate kusherehekea uhuru wa miaka 50 ya Tanzania ambayo haikuwepo miaka 50 iliyopita.

Btw, tungeomba ufanyie marekebisho tungo yako ili kuondoa makosa ya maneno uliyoyatumia kinyume na maana yake sahihi
 
Hivi Tanganyika ni nchi ya nani? Kwanini watu wanalilia nchi ya mkoloni?
Sawa, na iwe ya mkoloni, lakini tunatetea ukweli, tunakataa kupotoshwa. Unachokosea, unataka kulazimisha kwamba Tanzania ina miaka 50, ambao ni uongo wa chiriku, alisema Nyerere, ambae wewe ni zealot wake, kwamba "Ukweli haupendi kudharauliwa" ndio maana unaona kila ukijaribu usanii wa miaka 50 ya Tanzania, kunakuwa na mapingamizi mengi. Hata ingerembwa kwa beti za ngonjera.
 
Nchi yetu Tanganyika,
Sisi tunahuzunika,
Jinsi walivyo kuzika,
Bila sisi kuridhia.

Hakika umetutoka,
Moyo umehuzunika,
Daima twakukumbuka,
Ni lini utarejea?

Mwenzio wa ushirika,
Ambaye uliridhika,
Mzazi wa uhakika,
Bado anaendelea.

Mkazaa Tanzania,
Wewe ukatokomea,
Ulezi ukakimbia,
Kumwacha Zanzibaria.
 
Tueleweshe hiyo historia ili tupate kusherehekea uhuru wa miaka 50 ya Tanzania ambayo haikuwepo miaka 50 iliyopita.

Btw, tungeomba ufanyie marekebisho tungo yako ili kuondoa makosa ya maneno uliyoyatumia kinyume na maana yake sahihi

LOL, vina na mizani vitapwaya - labda aandike errata mwisho wa tenzi na kukushukuru mhariri mahiri !
 
Hizi sherehe hizi ni bora serikali izitishe au la kama wanategemea watu wataachana na
haya mambo sherehe zikimalizika lakini naona kama wanafungua pandorabox.
 
LOL, vina na mizani vitapwaya - labda aandike errata mwisho wa tenzi na kukushukuru mhariri mahiri !

Nilijua imeandikwa kwa kutumia mfumo wa Magharibi flani hivi manake kwa mfumo wa mizani ya kwetu Waswahili, kama ishapwaya tayari. Na ndo maana nikauliza :D
 
Mimi sioni uhuru, mbona tunarudi nyuma?
Kwangu uhuru udhuru, uhuru kwa wanochuma,
Kwa wengi hii kufuru, twaishi kinoma noma,
Uhuru gani tunao, iwapo twarudi nyuma.

Uhuru kwangu msemo, ni silaha ya siasa,
Humo ndimo tuliwamo, tubadilikeni sasa,
Umma ufanye mgomo, udai uhuru sasa,
Uhuru uuimbao, si uhuru ni udhuru.

Twaliwa na mafisadi, twajidai tuko huru,
Twaendeshwa kwa ahadi, ahadi za makufuru,
Wachache wanafaidi, kaumu haina nuru,
Uhuru uusifuo, si uhuru ni udhuru.
 
Nilijua imeandikwa kwa kutumia mfumo wa Magharibi flani hivi manake kwa mfumo wa mizani ya kwetu Waswahili, kama ishapwaya tayari. Na ndo maana nikauliza :D

Si unajua kuna tofauti kati ya utenzi na shairi, hilo la Mwanakijiji ni tenzi kama hii za Mwalimu Nyerere, si unajua tena mambo ya ufuasi:


Msidhani Tanzania
si sawa na Somalia,
ati mtaitabanga,
msihiliki kwa janga

Hivi Waha wa Kigoma
na Wakurya wa Musoma
na Wazaramo wa Pwani
watabaki majirani?

Wafipa wa Sumbawanga,
na Wasegeju wa Tanga,
wawatenge Waunguja,
wao wabaki wamoja?"

Wa Pemba mkiwatenga
na ndugu zao wa Tanga,
mtaacha wa Tabora
wadumu na wa Kagera?

Wa Pwani na wa Unguja
mkiona si wamoja,
mtaona wa Mtwara
ni wamoja na wa Mara?

Mbegu mbaya imepandwa,
lakini hatujashindwa,
tunaweza kuing'oa,
na nchi tukaokoa

Akipendezwa Jalia,
itadumu Tanzania,
Amina tena Amina!
Amina tena Amina!

JK Nyerere - Tanzania ! Tanzania !
 
Companero hayo maneno ya Mwalimu huwa yananigusa every time. Najiuliza kwanini Wamarekani wa Alaska, Texas, na Hawaii na hata wa Michigan wanasherehekea sherehe ya Uhuru wakati uhuru wa US ulipokuja wao hawakuwepo kwenye original 13! Bado sijapewa jibu kwanini Lousiana wanasherehekea uhuru wa Marekani au hata California!
 
Jicho
Kazi kubwa yako jicho, ni ngumu nai-husudu,
Nimefanya mchekecho, kwa ufundi na utundu,

Naamini nisemacho, kazi yako waimudu,

Jicho limeona mengi, uhuru wa Tanganyika ,


Huenda ni mpekecho, niliyofanya akidu,
Nili-sifiapo jicho,tumbo usifanye ndundu,

Tunza chakula kilicho, ndani usifanye pindu,
Jicho limeona mengi, madini ya Tanganyika.

Kila wewe uonacho, Mnyama au mdudu,

Ubongo wampa hicho, ugawanye kama ladu,

Ulimi ampe hicho, kujua kama ungwadu.
Jicho limeona mengi, Ufisadi Tanganyika.

kama wazi ni kiwekwacho,chaonwa kama kidundu,

Au kilicho maficho,hata kama vipo dundu,

Ukianza na mchakacho, utaona hadi kidu,

Jicho limeona mengi, Umasikini Tanganyika,

Ila- kini tatizacho, huchagui ka madudu,
Waona hata kilicho ,kichafu ama kibudu,

Hata haramu kilicho, kwanza ona kasha mbwedu

Sheria hazifuatwi, Tanganyika imekwisha.


Tamati namalizia, kuchambua Tanganyika,
Mengi tumejionea, wachache kunufaika,
Sheria zimesimama, kuwatetea vibaka,
wananchi masikini, Tanganyika omba omba.

Dr Hamza Yousuf Al Naamani.( Barubaru)
H/No 3513, Umm Hays block.
Minal al ameen.
Doha. Qatar

Safarini Tanzania 08/12/2011,kuelekea mazikoni Usoke Tabora.

 
Companero hayo maneno ya Mwalimu huwa yananigusa every time. Najiuliza kwanini Wamarekani wa Alaska, Texas, na Hawaii na hata wa Michigan wanasherehekea sherehe ya Uhuru wakati uhuru wa US ulipokuja wao hawakuwepo kwenye original 13! Bado sijapewa jibu kwanini Lousiana wanasherehekea uhuru wa Marekani au hata California!

It doesn't tally with our own mix-up!
 
Tanganyika hili jina
kwani twaliogopeani?
hili jina twalikana
hivi twaogopa nini?.


Eti Tanzania Bara!
Ni jina la nchi gani?
Historia barabara
nchi hii haijulikani!

siipingi Tanzania
ila nataka ukweli
tukubali historia
hatutakuwa dhalili!
 
Watanzania tuwe makini, hizi juhudi za kuisahaulisha tanganyika zina lengo gani? Hawa watu mi siwaelewi kabisa. Hivi wanadhani tanzania itadumu hadi lini? Tanzania ni zao la muungano wa tanganyika na zanzibar hivyo siku muungano huo ukivunjika tunadhani tutabaki na jina gani? Tuendelee kulienzi jina la tanganyika maana kuna siku litakuja kukumbukwa na kutumika kama ilivyokuwa kabala ya 9 desemba 1961.
 
I sense the call for Tanganyika is coming! Where does it come from???

The issue here is not the name or the structure in which it is in. The issue here is, nothing significant has been done. It is a fool who will believe that "tumethubutu, tumeweza na tunasonga mbele". Let us be realistic guys, we are messing up our country, we have ruined it, watu hawana hope. Umasikini na taabu imekuwa ndio way of life. Ni asilimia moja tu ya watanzania ndio wananufaika na nchi hii wengine wengi wako hoi, ni kudanganyana kusema kuwa tumethubutu na kuweza. labda ni wawili tu wamethubutu nakuweza.
 
Mimi sioni uhuru, mbona tunarudi nyuma?
Kwangu uhuru udhuru, uhuru kwa wanochuma,
Kwa wengi hii kufuru, twaishi kinoma noma,
Uhuru gani tunao, iwapo twarudi nyuma.

Uhuru kwangu msemo, ni silaha ya siasa,
Humo ndimo tuliwamo, tubadilikeni sasa,
Umma ufanye mgomo, udai uhuru sasa,
Uhuru uuimbao, si uhuru ni udhuru.

Twaliwa na mafisadi, twajidai tuko huru,
Twaendeshwa kwa ahadi, ahadi za makufuru,
Wachache wanafaidi, kaumu haina nuru,
Uhuru uusifuo, si uhuru ni udhuru.
Kama ingekuwa si kwa kuheshimu vina:
Uhuru uusifuo, si uhuru ni uhuni ingefana zaidi.
 
Back
Top Bottom